mkuu nafkiri hili la hardware integration Microsoft wapo juu sasa hivi, wamefanya kazi pamoja na intel kwa generation kama tatu sasa hivi kuna vitu kibao vipo kwenye windows au windows inavifanya vizuri zaidi vitu kama directx 12, intel speedshift etc, tunaishi katika ulimwengu ambao pc za windows ambazo ni nyembamba na zenye nguvu zaidi zinakaa na chaji kuliko ,mac nene ambazo ni dhaifu, angalia pc kama dell xps 13, asus zenbook series, hp spectre series etc zamani ulikuwa ukitaka ultrabook inayokaa na chaji ni macbook tu ila sasa hivi kuna laptop hata 50 zinafika zinazoipita mac kila idara.
na nna uhakika hujatumia defender na windows 10 na ant virus ya zamani ya microsoft kwenye windows za zamani inaitwa microsoft security essential, hii defender ni mpya.unless wewe ni mfanyabiashara mwenye sensitive data huna haja ya kutumia zaidi ya defender na windows 10. 2017 mkuu bado unawataja mcafee na norton? atleast kidogo ungesema kina malware bytes na kaspesky kidogo wanaweza kufight zaidi ya virusi, malware mbali mbali ambao ni smart.
pia kwenye mac huna antvirus ila zikitokea vulnerability unafanyaje? mpaka updates? wakati pc una update tu ant virus database, nakumbuka zile loop za java watu wa mac walikoma sana sababu fate ya pc zao wote wanasubiria oracle aiupdate java.
Mkuu nakubaliana na wewe baadhi ya vitu, hio defender upya wake ni from which year, kwa sababu hio defender imekuja shipped with windows 7, kweli sijatumia windows 10 with defender, lakini am pretty sure nimetumia windows 7 with defender with an additional anti virus ya Mcafee. And huwezi ukadharau Mcafee na Norton, hawa ni still big players in security.
Kwenye Mac hakuna anti virus?! nani Kasema? Kuna Bitdefender, ESET, AVG,NORTON, hio Kaspersky uloisifia, so sijajua labda umekusudia nini hapo. And guess what basi, mkuu mi tangu nianze kutumia Mac, sijawahi kufikiria kuweka anti virus, mpaka sasa sijapata any issue, i can't say that to the windows pc i have experienced, must have anti virus.
Hio karspesky tulikuwa tunatumia kwenye desktop ya ofisini iliyorun windows 7, siku 1 ilitumwa email kumbe ilikuwa na malware ndani yake wale wa ransomware, kwa bahati mbaya manager akaifungua kutaka kujua nini ndipo shughuli ilipoanza, tulipoteza kla file iliyopo kwenye doc, xls, pdf, ppt, n.k, tukampelekea IT expert akasema hawezi kuzirudisha kwa sababu hio malware ni mpya na bado haijapatikana solution, alichotufanyia katuwekea back up ya file zetu zilizokuwa encrypted na huyo maalware ili itakapotoka update ya kufix hio issue tutumie kuzirudihsa, tulipoteza data nyingi sana, hivi sasa ofisini tume update to windows 10, na jamaa ame recommend tutumie BitDefender