Kwanini Polisi hawafugi ndevu?

Kwanini Polisi hawafugi ndevu?

The unpaid Seller

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2019
Posts
2,206
Reaction score
6,615
Oy hope mko fiti.

Ebhana kuna vitu hua tunajua vipo namna fulani lakini sababu hasa hua hatujui, binafsi sijawahi kupata ufafanuzi kwanini askari wetu hawaruhusiwi kuwa na ndevu.

Hebu Leo tupate ufafanuzi itakua poa sana kama moja wa wadau ambae ni askaari wetu akatupa ufafanuzi kwa lengo la kujifunza na kutanua maarifa. Peace
 
Ukikutana na poti barabarani msimamishe muulize ilo swali atakujibu vizuri sana majibu ya uhakika..

Onyo: awe peke yake akiwa zaidi ya mmoja kazi utakuwa nayo
 
Moja ya sababu ni Ndevu zinaweza kuzuia mask za gesi na vifaa vya kupumulia "Raspiratory" visipitishe hewa vizuri,so itakua ni hatari kwa ulinzi wao hasa kwenye matukio ya kemikali au gesi ya sumu,ukivaa mask na una ndevu inakua ni rahisi hewa ya nje kuingia mwilini mwako kwenye uvutaji hewa wako.
 
Oy hope mko fiti.

Ebhana kuna vitu hua tunajua vipo namna fulani lakini sababu hasa hua hatujui, binafsi sijawahi kupata ufafanuzi kwanini askari wetu hawaruhusiwi kuwa na ndevu.

Hebu Leo tupate ufafanuzi itakua poa sana kama moja wa wadau ambae ni askaari wetu akatupa ufafanuzi kwa lengo la kujifunza na kutanua maarifa. Peace
Hawana sababu ya msingi zaidi ya ushetani tu.

Unamkataza vipi mtu kunyoa ndevu wakati ndevu ni katika maumbile na sifa anuai ya haraka ya uanaume.
 
Moja ya sababu ni Ndevu zinaweza kuzuia mask za gesi na vifaa vya kupumulia "Raspiratory" visipitishe hewa vizuri,so itakua ni hatari kwa ulinzi wao hasa kwenye matukio ya kemikali au gesi ya sumu,ukivaa mask na una ndevu inakua ni rahisi hewa ya nje kuingia mwilini mwako kwenye uvutaji hewa wako.
Mbona wa marekani, ulaya na uarabuni wana ndevu au wao bado hawajagundua teknolojia ya maksi za gas?
 
Mbona wa marekani, ulaya na uarabuni wana ndevu au wao bado hawajagundua teknolojia ya maksi za gas?
Sio department zote,
Ina depends on the specific police department's policy,mfano Scotland wanafuga ndevu na hii issue ipo kwenye debate kubwa sana,wengine wanaamini ni issue ya kidini,so hata ukimwambia ni safety issue bado kunakua na mkwaruzano,

Hiyo sababu niliyoiweka ni mojawapo tu,na wewe unaweza kushare unachokijua kuhusu hii issue.
 
Kwa polisi sijui, lakini JW wako watu wanazo ndevu kama mtu wa uraiani hao ni wa kwenye majukumu maalum na Hili la jeshi si la kushangaza kule Kwa wenzetu zile special forces Kwa ground wote huruhusiwa kuwa na mindevu kama beberu, mfano Special forces tier one kama Delta force, Seal team six, Ranger huko US Wana mindevu ukikutana nalo Kwa ground unazimia maana ni show Tu hii ni hasa wale wa middle east deployment, mfano SAS wa Uingereza wao ndo waanzilishi wa Haya mambo hasa zile special forces...Naamini Polisi wetu wapi wenye midevu lakini huwa ni kwaajili ya kazi maalum Tu, lengo kujiingiza kwenye jamii husika. Huwezi kwenda kwenye misheni hivi hivi lazima uwe na muonekano wa kukubalika na jamii unayoenda kupiga kazi....ila hawa tunaowaona na magwanda ni mwendo wa kioo ikizidi sana ni za brashi.
 
Back
Top Bottom