Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Nimekuwa nikimfuatilia kada wa CCM Humphrey Polepole kuanzia alipotoa barua yake ya kujiuzulu ubalozi wa Tanzania nchini Cuba; mazungumzo yake na Waandishi wa Habari na hata sasa (mazungumzo yake ya mwisho ameyafanya na Jenerali Ulimwengu).
Pamoja na mambo mengine, Polepole amekuwa akizungumzia desturi ya CCM ya kwamba aliyewahi kuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Spika hawapaswi kugombea Urais ndani ya CCM. Na sababu anayoisema ni kukosa jipya kwa watu hao mbele ya wapigakura wakati wa uchaguzi.
Ni ukweli ulio wazi kuwa Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa Makamu wa Rais. Kama angemaliza na Rais Magufuli, na kama CCM ingefuata 'desturi' hiyo, Rais Samia asingegombea Urais kupitia CCM. Lakini, Polepole hasemi jambo moja: Rais Samia hakuwa tu Makamu wa Rais, ndiye Rais aliye madarakani tangu mwaka 2021.
Kwahiyo, 'desturi' hiyo iliyosemwa na Polepole haimuhusu Rais Samia. Rais Samia ni sawa na marais wengine waliotangulia, ambao wote walitokana na CCM, waliopitishwa na chama chao kutetea nafasi yao ya Urais. Hadi hapo, Rais Samia hawezi kuzuiliwa na 'desturi' hiyo ya Polepole.
Kwanini hili halisemi? Bahati mbaya au makusudi?
Pamoja na mambo mengine, Polepole amekuwa akizungumzia desturi ya CCM ya kwamba aliyewahi kuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Spika hawapaswi kugombea Urais ndani ya CCM. Na sababu anayoisema ni kukosa jipya kwa watu hao mbele ya wapigakura wakati wa uchaguzi.
Ni ukweli ulio wazi kuwa Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa Makamu wa Rais. Kama angemaliza na Rais Magufuli, na kama CCM ingefuata 'desturi' hiyo, Rais Samia asingegombea Urais kupitia CCM. Lakini, Polepole hasemi jambo moja: Rais Samia hakuwa tu Makamu wa Rais, ndiye Rais aliye madarakani tangu mwaka 2021.
Kwahiyo, 'desturi' hiyo iliyosemwa na Polepole haimuhusu Rais Samia. Rais Samia ni sawa na marais wengine waliotangulia, ambao wote walitokana na CCM, waliopitishwa na chama chao kutetea nafasi yao ya Urais. Hadi hapo, Rais Samia hawezi kuzuiliwa na 'desturi' hiyo ya Polepole.
Kwanini hili halisemi? Bahati mbaya au makusudi?