smarte_r
JF-Expert Member
- Nov 8, 2013
- 4,538
- 11,868
Ilifika wakati kumpigania jpm hapa JF haikuwa jambo rahisi. ilihitaji kujitoa ufahamu.
Ni kazi iliyohitaji utumie nguvu, mikwara, vitisho na kupindisha ukweli.
Nilijipa kazi ya kumtetea baada tu ya kuapishwa kwake mwaka 2015. kwa hiyari yangu niliamua kuwa mwana propaganda wa wa JPM almaarufu "mataga".
niliamua kuwa mataga wa hiyari kwasababu nilivutiwa na sera zake na dhamira aliyoionyesha kuhusu kukomesha ufisadi nchini.
Niliunga mkono juhudi kwa kushangilia kila kauli aliyozungumza na kila maamuzi aliyofanya bila kujari madhara yake.
Baadae nikaja kujitafakari na kugundua kumbe nilikuwa sehemu ya kushabikia na kuhamasisha uovu, hii ni baada ya kuanza kwa matukio ya watu kuuwa, kutekwa, kubambikiwa kesi, kutishwa hadharani, kuminya vyombo vya habari na jeuri/majivuno kutoka kwa baadhi ya viongozi aliowateua.
Mwaka 2017 tukiwa katika taharuki iliyotokana na tukio la kupigwa risasi Tundu Lissu, niliacha rasmi kushabikia mijadala iliyokuwa inaunga mkono utawala wa Magufuli.
Ni kazi iliyohitaji utumie nguvu, mikwara, vitisho na kupindisha ukweli.
Nilijipa kazi ya kumtetea baada tu ya kuapishwa kwake mwaka 2015. kwa hiyari yangu niliamua kuwa mwana propaganda wa wa JPM almaarufu "mataga".
niliamua kuwa mataga wa hiyari kwasababu nilivutiwa na sera zake na dhamira aliyoionyesha kuhusu kukomesha ufisadi nchini.
Niliunga mkono juhudi kwa kushangilia kila kauli aliyozungumza na kila maamuzi aliyofanya bila kujari madhara yake.
Baadae nikaja kujitafakari na kugundua kumbe nilikuwa sehemu ya kushabikia na kuhamasisha uovu, hii ni baada ya kuanza kwa matukio ya watu kuuwa, kutekwa, kubambikiwa kesi, kutishwa hadharani, kuminya vyombo vya habari na jeuri/majivuno kutoka kwa baadhi ya viongozi aliowateua.
Mwaka 2017 tukiwa katika taharuki iliyotokana na tukio la kupigwa risasi Tundu Lissu, niliacha rasmi kushabikia mijadala iliyokuwa inaunga mkono utawala wa Magufuli.