Kwanini Mzee Kikwete alaumiwe?

Mangwea1900

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2025
Posts
2,484
Reaction score
3,269
Kelele zenye muelekeo wa lawama zimekuwa nyingi kwa Rais mstaafu kuwa anamshauri vibaya "mama" Rais aliyepo madarakani. Nabaki na butwaa nikiwa na maswali yafuatayo;
1. Je ni nani mwenye ushahidi kuwa Kikwete ndiye anamshauri SSH?
2. Je SSH (Dkt) hana washauri kwa utaratibu unaofahamika na Kikwete ni miongoni mwao?
3. Je uwepo wa Kikwete kati ya Marais waliotangulia mbele ya haki ndio sababu ya kumlaumu?
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Usitumie jazba isipokuwa ukweli wenye mashiko (facts) kuchangia hoja
 
Analikwamisha taifa. Kikwete ndiye boss wa rais
 
Mbona utawala wa kikwete hayakuwepn haya?kwnn tuseme n kikwete?
 

Wewe unafikiri ni kwa nini hasa kelele nyingi sana za lawama zinaelekezwa kwake??
 
Kitendo cha kuonekana kila sehemu hata kwenye "uzinduzi wa josho la mbuzi'
Hadi kuiwakilisha nchi kimataifa wakati waziri husika yupo, Kikwete akae ale pensheni yake ambayo ni Kodi zetu!
 
Angetulia zake kimya kama wastaafu wengine hakuna pahala angetajwa.

Tatizo ishapita takriban miaka 10 toka utawala wake lakini kutwa anaonekana yeye kila sehemu kiasi kwamba inakuwa ngumu kutofautisha nani hasa ndie raisi.

Amekuwa kimbelembele kiasi kwamba kuna wakati anajisahau kabisa kuwa hana mamlaka yeyote kwa sasa. Anajikuta anatoa mpaka matamko ya kimamlaka.
 
Duh
 
Akialikwa akatae?
 
Kitendo cha kuonekana kila sehemu hata kwenye "uzinduzi wa josho la mbuzi'
Hadi kuiwakilisha nchi kimataifa wakati waziri husika yupo, Kikwete akae ale pensheni yake ambayo ni Kodi zetu!
Mbona Mizengo anaoneka sana
 
Sababu ya marekani / USA kutoruhusu kuwa na raisi mwanamke ni hofu waliyonayo juu ya akili za kushikiwa za wanawake, anaweza akatokea mwamba huko akaja akamsugua vizuri Hilary Clinton akauza nchi kwa msuguo.
 
Yule ni jambazi wa taifa
 
 
Mkumbusheni Jakaya aelewe maana ya kustaafu!
Aige alivyokuwa Alhaji Mwinyi.
Aachane na kupiga ndogondogo kwa ajili ya mwanaye.
Am control mke wake, na kumweka mbali na kodi za wananchi.
 
Ana kimbembele sana yule mswahili, mbona kipindi cha Jiwe alikuwa anashinda Msoga akilima mananasi tuu...kwann sasa?!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…