Kwanini Mungu yupo?

Mzee unanitisha Sasa ...Kuna mtu unaemjua alieuliwa?.
Ila Mimi Ningeuliza Kwa Yule Mungu aliwaumba watu wote wa dini zote, wazungu Kwa wahindi Kwa waafrica.
 
Ok, Sasa hizi ibaada zipo kwaajili Gani? Na Kwa manufaa ya nani?
 
Unaposema muda unamaanisha Nini? Majira au?
Maana muda upo TU ila majira ndio Wanadamu tumeyatengeneza.

Ni sawa na umbali; Hivi vipimo vya kilometer, centimeters,maili,heka,mita, Tumevitengeneza TU sisi binadamu, ilikuwa inawezekana kabisa centimeter 1 tungeifanya Ikawa sawa na kilomita 10 au centimeter tungeiita Magufulita na maili tukaita samiamita...ni sisi na Sheria zetu TU.
Lakini haimaanishi huo umbali wa centimeter 1, kilomita 2,maili 3 haupo.....Hata tukisema tupime Kwa kamba umbali wa Maili 1 halafu tuuite kilomita 8, Bado ule umbali tulioupima haubadiliki urefu wake, hata kama Leo tuuite ni kilometer 10 na kesho tuite centimeter 3...umbali wenyewe utabaki palepale haubadiliki.
Kwahyo kwasababu hizi kilometer, metre,maili, centimeters zimetengenezwa na binadamu, isiwe kigezo Cha kusema hakuna Space, Hakuna nafasi, Hakuna Umbali...kwamba kwakuwa kilometer ilitengenezwa na binadamu basi unaweza kukanyaga Tambo Moja TU ukaupita huo umbali kwasababu hiyo nafasi haipo ni illusions TU.


Muda upo, ingawa vipimo vya sekunde,siku,masaa,mwaka,miezi vimetengenezwa na binadamu...Tungeweza kusema mwaka una miezi 10 TU yenye siku 40 kila mwezi...na kusingekuwa na shida yoyote, lakini muda unaopimwa Kwa hivyo vipimo upo....lazima matukio yaendelee...Muda ukisimama inamaanisha matukio yamesimama...
Kama hakuna muda Inamaana hakuna mabadiliko, yani mfano unapokuwa unapika Yai halitakiwi kuiva....Maana likiiva limebadilika, na likibadilika limeshaonesha kuwa kuna muda uliopita lilikuwa halijapikwa,maana kuku hatagi mayai yaliyopikwa.

Baada ya muda kupita ndio tukio la kupikwa likafanyika na Yai likaiva....Hiyo ni athari ya muda.
 

Mimi swali la je, hakujua anguko la binadamu? naweza kumsamehe hata akisema atatuambia tukifika mbinguni...

ila swali la kwanini tunamuabudu na kumsifu?...kama asipotuambia sababu za kwanini tunafanya hivyo tukiwa Bado duniani.

Inamaana anatupa command ya kufanya vitu Tena Kwa vitisho kuwa tusipovifanya anatupeleka motoni....Halafu sababu ya kufanya hivo vitu hatuambii.
.inakuwa kama anafanya udikteta Fulani usiomfaidisha yeyote...sio yeye Mungu sio sisi binadamu
 
Point yangu ni kwamba, kupitia ufafanuzi wako kuwa Mungu ni energy unakuwa umekubali kuwa Mungu sio muumba wa kila kitu.

Hilo ni jambo ambalo nataka nikuone unakubali kabla ya kuenda mbele zaidi
 
Eti mtu unataka kujua √(3) inafanywaje hali hujui 1+1 inafanywaje !!! 🤣--- elimu zingine zahitaji kupitia hatua baada ya hatua.
Basi hapo tatizo liko kwako, huna uwezo wa kumuelewesha mtu akaelewa au swali ni gumu huna majibu na hutaki kukubali kuwa hujui
 
Mungu ni creation ya mwanadamu kichwani kwake naamini ilitokana na kushindwa kujibu maswali magumu yaliyomkabiri au kutaka control ya binadamu wenzake, hakuna proof yeyote ya uwepo wa mungu, ingawaje kwa akili yetu ndogo naamini kuna kitu kimetuzidi uwezo ndio maana hatuelewi mambo mengi,infact hatujui hata tumetoka wapi tunaelekea wapi, enjoy tuu safari ya maisha labda kuna siku tutakuja kujua ukweli wa kila kitu kuanzi9a atoms mpaka galaxies na universe kwa ujumla
 
Basi hapo tatizo liko kwako, huna uwezo wa kumuelewesha mtu akaelewa au swali ni gumu huna majibu na hutaki kukubali kuwa hujui


Maana yangu ni hii kwamba mtu ajue vitu vidogo vya awali kwanza ndipo awe na msingi wa kuweza kujua vitu vikubwa.

Ameuliza kwanini Mungu yupo ilhali yeye mwenyewe hajui kwanini yeye yupo !!!--- Yeye yupo kwasababu Mungu kamuumba ili amuabudu Yeye Mungu hivyo basi Mungu yupo kwasababu, tofauti na sifa ya binadamu na vitu vingine, Yeye Mungu anayo sifa ya UMILELE, sifa inayojitambua na yenye nidhamu, sifa ya umilele ni kwamba haiumbwi na wala haina mwanzo wala mwisho na kila kitu chenye Umri (muhula) kimetokana na huo umilele isitoshe huo umilele unaweza kuumba vitu vya milele mfano Roho, Malaika na vingine tusivyovijua. Sasa jibu la swali lake kwanini Mungu yupo ni hilo kwamba Yeye yupo kwasababu ya sifa yake ya UMILELE, yaani umilele hauna mwanzo wala mwisho na ndio maana Mungu alikuwepo, yupo na atakuwepo daima.

Hivyo yampasa ajue sio tu kwamba Mungu yupo leo bali alikuwepo, yupo na atakuwepo DAIMA.
 


Kama wewe hujui usidhani na wengine ni kama wewe.
 
Kwahyo viumbe wote wa kwenye Huu ulimwengu ndio wamemfanya Mungu awepo?
Hawa viumbe wasingekuwepo na Mungu asingekuwepo?
Hapana Mungu amekuwepo hata kabla ya huu ulimwengu kuwepo, uthibisho huu ulimwengu sio binadamu ndio walianza kuumbwa bali ni majini kwanza kabla ya wanadamu

binadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu baada ya majini kugoma kumuabudu Mungu.Kabla ya majini kuwepo duniani,vipo viumbe vingine vingi pia katika sayari zingine nje ya Dunia.

Mfano UFO, malaika,nk.
Na still pana mamilioni ya sayari zingine ambazo hazijagundulika kwa macho ya sayansi ya mwanadamu.
 
Kivyovyote TU, au vyote kama unaweza please
Mungu ni undefined object,achunguziki kisayansi zaidi ya kiroho.Shetan pamoja na nguvu zake zote still hawezi fikia ukuu wa Mungu
 
unachozungumza bado ni illusion tu wakati ni sasa future ni matazamio tu ambayo bado hayajatokea , muda unapata mantic kunapokua na mwanzo na mwsho , unaposema nitachemsha yai umeitengeneza future kichwan inaweza isitokee , ila unapochemsha yai ndo kitendo kinakua sio illusion , siku ni zile zile matukio ni yale yale nanapata mantic yanapotokea now ila ukiyazania bado inakua ni illusion

muda unapimwa na kipimo , bila muda kupimwa hakuna muda , mwanzo na mwisho nikipimo cha kwanza cha mda , Huwezi kupima uwepo wa Mungu kwa muda .
 
Point yangu ni kwamba, kupitia ufafanuzi wako kuwa Mungu ni energy unakuwa umekubali kuwa Mungu sio muumba wa kila kitu.

Hilo ni jambo ambalo nataka nikuone unakubali kabla ya kuenda mbele zaidi
kma Mungu ni super energy na energy ndo imefanya maumbile yote yanayooneka na yasio uonekana yawepo katika frequence mbalimbal , nawezaje kusema hiyo energy haija umba kila kitu?

kumbuka energy hiyo ipo kwenye mwendo na frequence mbalimbali ndo maana kuna maumbile mengne sio rahis kuyaona kutokana yapo kwenye speed kubwa na frequence ha hali ya juu.
 
Haya mambo ya dini yanachangamoto nyingi.
 
Mzee unanitisha Sasa ...Kuna mtu unaemjua alieuliwa?.
Ila Mimi Ningeuliza Kwa Yule Mungu aliwaumba watu wote wa dini zote, wazungu Kwa wahindi Kwa waafrica.
Babu nadhani bado uko shule! mie sikutishi ila natamka ukweli! ......wengi wamekufa mfano Suleiman Rushdie, anatafutwa auliwe, na zawadi NONO! itatolewa mpaka sasa IKO HIVO! ukiwa na ubavu kamsake!

ameponea chupuchupu juzi alipigwa Bisu huko Manhattan USA!........Narudia, hivi ktk hao Miungu niliyo itaja! wale wanao waabudu wanaamini wao wametokana na huyo mungu wao!

nikakupa mifano Osilis Mungu wa Wa Misri aliye pambana na wana wa Israel!...mungu Baal! aliwasaidia Wafilist kumtoboa macho Samsoni! na kweli alikufa kipofu yule jamaa! pamoja na maguvu yake!

piga ua galagaza hawakumjua mungu mwingine! hata leo! kuna watu wengi ukiwamo weye unaamini mungu Mzungu huyo! Wao wazungu wanajua ndo kaumba watu wooote, waafrica wahindi nk!

sasa wewe/na wenzako ndo mtwambiye mungu wenu alivo! make baadhi yetu sisi hatumjui......
 
Mtoa mada kabla ya kujibu swali lako, ningependa kwanza nifahamu swali lako la "Kwanini mungu yupo?" Unifahamishe.

Unaposema kwanini mungu yupo, Je unamaanisha mungu yupi?
 
Mtaongea weeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!! lkn Mungu kamwe hatajulikana kwa kondoo wasio wake! kwa sababu kondoo wake wanamjua mchungaji wao!!

Na mbinguni hamwendi ng'oooooooooooo!
 
Sasa kama sio viumbe ndio wamemfanya Mungu awepo, Je sababu ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…