Makerubi hawajaelewa bado
Nilikuwa nikiona mada za Zumaridi humu naziruka, hivyo nilikuwa sielewi kitu, nimemfuatilia.
Nimekutana na dada anaitwa Diana, she is very bold amd brave, nimependa sana. Kuna sehemu anaingizia ishu ya Marehemu Kanumba, kwamba amewasiliana nae kwa simu, na kwamba roho yake, Yeye Zumaridi ameshaiondoa kule kuzimu, A bold move..
Pia siku nyingine anahojiwa na kusema ameongea na Mungu kwa sauti, kuhusu issue ya HIV/AIDS, anotheer bold move..
Unaweza ukadharau lakini hizi issues ndio zimewatajirisha Gwajima na Babu wa Loliondo respectively.. na zinaendelea kumtajirisha Mwamposa na kuhani Mussa japo wao wanazihubiri indirectly..
Kwa hiyo kukuta binti mdogo kama Diana(Mfalme Zumaridi)ana uthubutu mkubwa kiasi hicho nimependa, maisha bila kuwa Bold and Brave utakufa masikini, Kwa sababu huyu dada anaonekana ana pesa nyingi(inashangaza anazitoa wapi), atafute wanasheria wazuri wamchomoe kwanza kwenye huu msala, halafu wawe kama washauri wa kumguide anapoendelea na kanisa lake asiteleze katika loopholes za kijinai, awarob rob hata baadhi ya akina nanii huko wasimsumbue sumbue, and if that happens.., this girl is a billionaire in the making!! DIANA BUNDALA njoo usome ushauri huku uendelee kupiga hela.