Nilishawahi kuweka mada ya mbuzi wa ndafu kuwa ni ibada ya kishetani, mjadala ulikuwa mzito na nilishutumiwa sana mpaka pm, hii ni kwa sababu iligusa Mila na tamaduni za makabila ya watu.
Kulikuwa pia na mada ihusuyo mbuzi wanaozurura mitaani, wanaitwa wa laana ikawa nayo ni mjadala uliogusa hisia za wengi
Si mara moja au mara mbili kusikia kuhusu mbuzi wa shughuli... Ni shughuli gani hiyo??? Kwanini asiwe kondoo au punda au Ng'ombe?
Mbuzi hasa beberu ni alama ya kuzimu, ni alama ya shetani na imani za kishetani na dunia ya giza, ndio maana laana na mapepo yote hutupiwa mbuzi kwakuwa kule ni Kama nyumbani kwao.
Mbuzi hawa wanaoitwa kwa jina lingine mbuzi wa albadiri hawafi hawaugui hawagongwi na magari na kamwe huwezi kuwakuta kwenye sehemu zisizo na watu, kamwe huwezi kukuta Mzoga wa hawa wanayama, na kama ukiukuta basi huyo alikuwa kenge kwenye msafara wa mamba.
Waganga wengi wa kienyeji na mambo ya Kiza humtumia Sana mbuzi Kama sehemu ya kafara na kinachochukuliwa ni damu na Kichwa tuu, hiki ndio hutengeneza muungano na nguvu za kuzimu.
Cha kushangaza ni kwamba mapepo huwaingia wanawake zaidi kuliko wanaume, na kwa wanyama mbuzi ndio hutumika zaidi kuliko wanyama wengine unajua ni kwanini?
Mniwie radhi kwa picha nitakayoweka, ni sehemu ya kuelimishana na kujuzana visivyosemwa, Nina Heshima na adabu kwa kila mtu, hasa mama zetu, picha hii isitafsiriwe Kama dhihaka... Nimetoa angalizo hili mapema.
Mfanano wa via vya uzazi vya mwanamke na kichwa cha mbuzi beberu ndio vinatengeneza colabo ya ajabu unaovutia nguvu za kuzimu na mapepo