Byakatonda
JF-Expert Member
- Oct 14, 2021
- 412
- 765
Kiukweli nimebahatika kutembelea majiji yote ya nchi hii na mengine nimekaa ila Mbeya dah! ni hujuma tupu kwanza haina chaneli za barabara za mitaa za uhakika. barabara mfano ya kwenda chunya ni mashimo tupu kuanzia isanga mpaka mwansenkwa ni hatari kama sio dereva mzuri jiandae kufa. Maji wanakata muda mwingi. Lazima uwe na dyaba ndani limejaa maji.
Watu wanasema maisha ni magumu kwenye majiji kama dodoma lakini nimegundua hapa mbeya ni magumu zaidi ya dodoma. Dom unaweza pata samaki wa kuanzia miambili kitaa mpaka buku ila hapa mbeya kama huna buku kwenda juu hujapata samaki. Na vingine vingi hii nazungumzia kwa raia wabangaizaji.
Ndizi dodoma zinatoka bukoba lakini ni nafuu tofauti na mbeya zinatoka tukuyu ila ni gharama na hazipatikani za uhakika.
Jiji lenyewe ni linear sio scattered, halijasambaa ukilinganisha na majiji kama Tanga, mwanza na Dodoma . Kuna foreni ya hatari kuanzia mbalizi kuja mpaka kabwe hiyo kuanzia jioni ya dar nafuu.
Utaratibu wa raia kuwekewa vivuko barabarani hamna kabisa maeneo yote ya Mwanjelwa to kabwe utegemee huruma za madereva.
Miaka ijayo kwa hali hii ya vumbi watu wajiandae kuumwa macho tu maana watu wengi wa hapa ukiwacheki macho muda mwingi yana matongotongo kibao.
Mji una tozo nyingi lakini maendeleo hamna. Kuna wakusanya hela za taka wanapita Kila chumba Cha mpangaji kuchukua buku mbili eti za taka, lakini hamna la maana linalofanywa.
Watu wanasema maisha ni magumu kwenye majiji kama dodoma lakini nimegundua hapa mbeya ni magumu zaidi ya dodoma. Dom unaweza pata samaki wa kuanzia miambili kitaa mpaka buku ila hapa mbeya kama huna buku kwenda juu hujapata samaki. Na vingine vingi hii nazungumzia kwa raia wabangaizaji.
Ndizi dodoma zinatoka bukoba lakini ni nafuu tofauti na mbeya zinatoka tukuyu ila ni gharama na hazipatikani za uhakika.
Jiji lenyewe ni linear sio scattered, halijasambaa ukilinganisha na majiji kama Tanga, mwanza na Dodoma . Kuna foreni ya hatari kuanzia mbalizi kuja mpaka kabwe hiyo kuanzia jioni ya dar nafuu.
Utaratibu wa raia kuwekewa vivuko barabarani hamna kabisa maeneo yote ya Mwanjelwa to kabwe utegemee huruma za madereva.
Miaka ijayo kwa hali hii ya vumbi watu wajiandae kuumwa macho tu maana watu wengi wa hapa ukiwacheki macho muda mwingi yana matongotongo kibao.
Mji una tozo nyingi lakini maendeleo hamna. Kuna wakusanya hela za taka wanapita Kila chumba Cha mpangaji kuchukua buku mbili eti za taka, lakini hamna la maana linalofanywa.