GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,554
- 108,895
Rais wa Uganda Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni leo amelazimika kukatisha Ziara yake alipokuwa akihudhuria Sherehe za Kuwakumbuka Mashujaa wa Kiimani nchini humo ( wenyewe mnaita Hija ) na kukimbia Hospitalini kwenda Kumtembelea Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere ambaye ameugua ghafla. Ikumbukwe kuwa Mama Maria Nyerere yupo nchini humo kwa Mwaliko wa Mheshimiwa Rais Museveni ili nae awe sehemu ya hizi Sherehe.
Nasikitika kwamba wenye Mama yetu ( Watanzania ) hadi hivi sasa hatujajulishwa juu ya hili na ' Mamlaka ' husika nazo zipo Kimya tu. Na mpaka Mheshimiwa Rais wa Uganda ameamua Kukatisha Ziara yake na kuwahi Hospitalini inawezekana Mjane Mama Maria Nyerere labda hali yake si nzuri kiasi hasa ukizingatia ya kwamba kwa muda sasa amekuwa akiuguaugua japo inafanywa Siri na sijui ni kwanini.
Nawasilisha.
Chanzo Taarifa: NTV Uganda.
Nasikitika kwamba wenye Mama yetu ( Watanzania ) hadi hivi sasa hatujajulishwa juu ya hili na ' Mamlaka ' husika nazo zipo Kimya tu. Na mpaka Mheshimiwa Rais wa Uganda ameamua Kukatisha Ziara yake na kuwahi Hospitalini inawezekana Mjane Mama Maria Nyerere labda hali yake si nzuri kiasi hasa ukizingatia ya kwamba kwa muda sasa amekuwa akiuguaugua japo inafanywa Siri na sijui ni kwanini.
Nawasilisha.
Chanzo Taarifa: NTV Uganda.