Kwanini mamba hamfanyii fujo Kiboko?

Kwanini mamba hamfanyii fujo Kiboko?

We ushaona lile domo la kiboko na ile mijino yake kama nondo? Ni mamba gani mwenye ujasiri wa kulisogelea lile domo KUBWAA lililojaa visu na mashoka?

Ni lidude kubwa lile sio la mchezo! Akifungua lile domo lake ana uwezo wa kummeza mamba mzima mzima!

Mamba wana utambuzi wa asili kwamba Kiboko ni kiboko kweli kweli... THEIR FEAR AND RESPECT TO HIPPOS IS PRINTED IN THEIR DNA.

Hawathubutu hata siku moja kumsogelea kiboko! Hata kwa bahati mbaya!
THEIR FEAR AND RESPECT TO HIPPOS ^IS^!??? PRINTED IN THEIR DNA.

Why unaharibu Kiswahili hivyo!???
 
Jina kiboko limetokana na vile mamba hawezi kumfanya chochote akiwa hai (kiboko akijifia analiwa na mamba)

Nadhani umepata picha kuwa kiboko Ni kiboko
 
Kile kitu Kiboko alichowahi kumfanyia Mamba....!
Ndo Chanzo cha neno KIBOKO, Utasikia Kiboko yake! Kiboko yao n.k

Kiboko ni Kiboko ya Mamba.
Kwahiyo kiboko ndo kiboko au mamba ndo kiboko?
 
Huwa najiuliza sana, Mamba anakula nyama na Kiboko anakula nyasi, lakini wanaishi sehemu moja. Kwa tabia ya Mamba anakula mnyama yoyote anayekatiza mbele yake. Sasa mbona hamtafuni Kiboko na yuko nae muda mwingi?
Some time huwa mamba anavizia anakamata mtoto, na kuna wakati wanalianzishaga, kuna Video moja jivi ngoja niisake nilikuwa nayo ikionyesha Kiboko wakileteana nodma na Mamba,
 
Mamba akikosea step akawatibua viboko kwa namna yoyote ile, hilo dimbwi halitakalika...lazima watafute kwingine pa kukaa. Nafikiri mabifu yao huwa hayachukui muda mrefu, baada ya hasira kushuka watarudi kukaa pamoja.
 
Back
Top Bottom