mchemsho
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 3,230
- 935
Kilichotokea na kushuhudiwa kwenye kampeni ya leo viwanja vya Gymkhana Bukoba, naamini CCM leo hawalali usingizi..lazima wamechanganyikiwa. Kama ilivyotarajiwa umati ulojitokeza kupindukia ulikuwa gumzo..hakukuwa na malori, ma bus wala hakuna aliyeletwa kwa shuruti kuhudhuria mkutano.
Kilichoshangaza zaidi ni pale Lowassa aliposimama ili aanze kuhutubia...haikuwa hali ya kawaida, umati huo kwa maelfu walipiga makelele ya kushangilia kwa takribani dakika 3, huku Lowasa mwenyewe akijitahidi kuwashusha munkari umati huo. Wengine walisikika wakisema hata usijichoshe kuongea...kwa kweli hamasa ilikuwa kubwa sana. Ni kweli nimeamini maelfu ya watu wana"Mahaba" na Lowassa.
USHAURI WA BURE KWA CCM:
Jumatatu kwenye mkutano wenu, ambao na nyie kama kawaida yenu kuiga mmeuhamishia kwenye viwanja vilvyibatizwa leo "Lowasa Grounds" msitaje jina la Lowassa, wala msitaje neno mabadiliko, MTAUMBUKA.
Kasombeni watu na malori kama kawaida yenu kutoka Kemondo, Katerero, Maruku,hata kutoka Kyaka ili nanyie mjaze UMATI.
Pia msisahau kuleta wasanii wale wakali zaidi ili angalau wakazi wa bukoba waje kushuhudia burudani ya bure.
Mwisho..chonde chonde msizungumzie meli kwasababu mkapa aliahidi mwaka 2000, Kikwete 2005,Kikwete 2010..na mpaka leo bila bila.
Nilikuwa nayasikia tu ila kwa leo nimeamini,
LOWASA IS UNSTOPABLE.
Kilichoshangaza zaidi ni pale Lowassa aliposimama ili aanze kuhutubia...haikuwa hali ya kawaida, umati huo kwa maelfu walipiga makelele ya kushangilia kwa takribani dakika 3, huku Lowasa mwenyewe akijitahidi kuwashusha munkari umati huo. Wengine walisikika wakisema hata usijichoshe kuongea...kwa kweli hamasa ilikuwa kubwa sana. Ni kweli nimeamini maelfu ya watu wana"Mahaba" na Lowassa.
USHAURI WA BURE KWA CCM:
Jumatatu kwenye mkutano wenu, ambao na nyie kama kawaida yenu kuiga mmeuhamishia kwenye viwanja vilvyibatizwa leo "Lowasa Grounds" msitaje jina la Lowassa, wala msitaje neno mabadiliko, MTAUMBUKA.
Kasombeni watu na malori kama kawaida yenu kutoka Kemondo, Katerero, Maruku,hata kutoka Kyaka ili nanyie mjaze UMATI.
Pia msisahau kuleta wasanii wale wakali zaidi ili angalau wakazi wa bukoba waje kushuhudia burudani ya bure.
Mwisho..chonde chonde msizungumzie meli kwasababu mkapa aliahidi mwaka 2000, Kikwete 2005,Kikwete 2010..na mpaka leo bila bila.
Nilikuwa nayasikia tu ila kwa leo nimeamini,
LOWASA IS UNSTOPABLE.