Kwanini Lowassa amepotea baada ya kipigo uchaguzi mdogo? Ni aibu au amekata tamaa?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Mlengwa hapo juu katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mdogo na wakati wa kampeni, alipita mikoa kadhaa kwa lengo la kujenga chama chake, CHADEMA kwa madai kuwa hakina mizizi kwa wananchi. Nakumbuka alivyoweka kambi kanda ya Ziwa huku akitoa ahadi hewa mithili ya zile ahadi za mvua ya Thailand. Kwamba, ataongea na wafadhili ili washushe chakula kuwasaidia wananchi wenye njaa. Hadi sasa, mzee Lowasa hajaleta chakula cha msaada alichoahidi.

Baada ya kipigo kitakatifu ambapo CHADEMA waliambulia Kata moja tu huku wakipokonywa nyingine na CCM kati ya kata 20 zilizogombaniwa, hakika mzee sijui kajificha wapi. Haonekani kwenye media wala social media. Yaani kwa ujumla kapotea mithili ya kakakuona.

Najiuliza maswali kibao na sipati jibu. Je kupotea huku ni aibu ya kipigo hicho? Au amekata tamaa na vyama vya upinzani kwa vile anaonekana kutwanga maji kwenye kinu? Au kawasusia CHADEMA? Au kakasirika? Au kaishiwa pumzi? Au? Au? Au? Mliopo jirani na huyo mzee naomba mjitokeze na kutueleza nini kinaendelea.
 
Hakuna anayehangaika na huyo mhuni ambaye anaishi kwa kuuza mwili wake Marekani. Sisi tunahangaika na wapiga kura wetu
mbona mkitajiwa jina la mange ccm mnakanyagana, mnaogopa atavujisha madudu yenu. hiyo post yako inadhihirisha jinsi ulivyopaniki.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Mlengwa hapo juu katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mdogo na wakati wa kampeni, alipita mikoa kadhaa kwa lengo la kujenga chama chake, CHADEMA kwa madai kuwa hakina mizizi kwa wananchi. Nakumbuka alivyoweka kambi kanda ya Ziwa huku akitoa ahadi hewa mithili ya zile ahadi za mvua ya Thailand. Kwamba, ataongea na wafadhili ili washushe chakula kuwasaidia wananchi wenye njaa. Hadi sasa, mzee Lowasa hajaleta chakula cha msaada alichoahidi.

Baada ya kipigo kitakatifu ambapo CHADEMA waliambulia Kata moja tu huku wakipokonywa nyingine na CCM kati ya kata 20 zilizogombaniwa, hakika mzee sijui kajificha wapi. Haonekani kwenye media wala social media. Yaani kwa ujumla kapotea mithili ya kakakuona.

Najiuliza maswali kibao na sipati jibu. Je kupotea huku ni aibu ya kipigo hicho? Au amekata tamaa na vyama vya upinzani kwa vile anaonekana kutwanga maji kwenye kinu? Au kawasusia CHADEMA? Au kakasirika? Au kaishiwa pumzi? Au? Au? Au? Mliopo jirani na huyo mzee naomba mjitokeze na kutueleza nini kinaendelea.

Tupo kwenye HOTUBA za MABOSI wako wawili Mkullu wange na RC wa Darisalama.
 
Yani nyie wana CCM akili zenu ni za kuku pori kabisa, Lowasa akiongea mnalalamika amezeeka apumzike, akikaa kimya mnalia tena kuwa amepata kipigo.
 
mbona mkitajiwa jina la mange ccm mnakanyagana, mnaogopa atavujisha madudu yenu. hiyo post yako inadhihirisha jinsi ulivyopaniki.
Madudu gani ambayo Mange Kimambi atavujisha? Na je nini kinachomzuia huko aliko kutaja hayo madudu? Hakuna mateso makubwa kama kuishi uhamishoni huku ukitamani kurejea nyumbani.
 
Sijadhalilisha wanawake bali nimeeleza maisha halisi ya Mange Kimambi huko Los Angeles California Marekani. Kwani unajua anafanya kazi gani? Ndo hiyo niliyokutajia
usitake kujifanya unamjua wewe, au na wewe unatafuta followers wengi
 
Sijadhalilisha wanawake bali nimeeleza maisha halisi ya Mange Kimambi huko Los Angeles California Marekani. Kwani unajua anafanya kazi gani? Ndo hiyo niliyokutajia
Wewe unafanyakazi gani?
 
Mbona huulizii million 50 kila kijiji za jamaa yenu alietoa ahadi hewa
Nafikiri huwa anahisi huenda ilikuwa ndoto
 
Back
Top Bottom