Kwanini kulaumiana wanawake/wanaume katika suala la ndoa?

Kwanini kulaumiana wanawake/wanaume katika suala la ndoa?

Anonymous

Senior Member
Joined
Apr 6, 2006
Posts
129
Reaction score
358
Habari wana JF,

Nimekuwa nikishuhudia sana tena kwa kiasi kikubwa mnoo kulaumia baina ya wanawake na wanaume katika suala zima la mausiano(ndoa),iwe ktk jamii huku tunakoishi au humu JF..

Wanawake huwalaumu wanaume na wanaume huwalaumu wanawake.

Sasa leo naomba niongelee lawama haswa za wanaume kwa wanawake,Wanaume huwalaumu kwa kiasi kikubwa zaidi wanawake na kuwaachia mabaya yote kuwa wao(wanawake) ndio huwa chanzo cha mivurugano mingi ktk mahusiano na ndoa kwa ujumla.

Mifano dhahiri ni humu ndani, endapo mwanaume ataleta uzi kuhusu tatizo ktk mahusiano yake lawama zoote humwagwa kwa wanawake(hasa wanaume), na watu huenda mbali zaidi na kutoa ushauri kama "achana naye asikusumbue wanawake ni wengi sana" na ushauri wa aina hii ndio huwa mwingi zaidi kutoka kwa wanaume.

Iwapo mwanamke atatoa uzi pia juu ya matatizo katika mahusiano yake basi wanaume wengi kwa kiasi kikubwa humuona huyo mwanamke ndiye mwenye matatizo yaliyopelekea mgongano au hata kuvunjika kwa mahusiano yake.

Utasikia "jichunguze wewe utakuwa ndiye mwenye tatizo"
Na wengine husema wanawake hujisahau sana ktk mahusiano na ndoa kwa ujumla, hivyo anapaswa kuwa mbunifu,mvumilivu,nk. Je wanaume hawajisahau? Au wao wamekamilika hawana tatizoblolote?

Jamani hivi mahusiano huwa ni ya mwanamke peke yake au mwanamke na mwanaume? Je mwanaume hapaswi kuwa mbunifu,mvumilivu,mwenye heshima,nk kwa mkewe/mpenziwe?Sisi sote ni binadamu,hatujakamilika, hivyo twapaswa kurekebishana, kusaidiana na kuvumiliana kwa yale ambayo hatujakamilika kwayo.

Hata mwanaume anapochepuka, husingizia kuwa "mwanamke ndiye chanzo" hawataki kabisa kukubali fault yao ktk suala hili, jamani sisi sio malaika na tuna mioyo yenye nyama kama yenu, kwanini kila lawama mtutupie ilihali nanyi mna mapungufu mengi tu tunayoyavumilia?

Wanawake kwa kiasi kikubwa nimeshuhudia wakishauriana sana juu ya "uvumilivu" na masuala mengine ambayo yataongezea chachu ktk mahusiano/ndoa zao, ila kwa upande wa wanaume hili ni nadra sana kulikuta, zaidi ya "achana naye" au "tafuta mchepuko" "mpuuze" je kweli hii ndio suluhisho pekee kwenu? Na wengine huenda mbali na kuona kuwa kuoa ni hisani tu kwa mwanamke!!

Na kadri muda unavyozidi kwenda ndio bala zaidi linaongezeka, mahusiano/ndoa walaaa hayana uzito tena, hivyo kupelekea hata kizazi tunachokitengeneza tunakilaumu wakati sisi ndio tumesababisha kiwe hivyo.Familia ndio base ya kila kitu, pakiharibika hapo basi hatutokuwa na jamii,taifa na dunia salama.

Play yo part men, hizi lawama ni zetu wote.

Karibuni kwa maoni na mafunzo zaidi ili tuweze kuwa na mahusiano yaliyo imara.

#peace#
 
Sababu kubwa ni ubinafsi, kila mmoja anajiona yuko sahihi kuliko mwenzake, hii inapelekea kibri cha kujiona uko sawa ata ukifanya kosa, ili kumaliza upinzani huu mnatakiwa kushirikiana katika mambo yote, julishaneni na kubalianeni, mtajikuta mnaenda sawa
 
My boss unajua katika hili me na wewe ni wamoja daima.

Naamini na Najua kuwa mke ndo anabeba kusudi la mume wake, ndiye msaidizi wa mume wake na hivyo hatima ya ndoa nyingi ipo mikononi mwa mke. Sasa inavyoonekana ndoa nyingi mke part yake huwa inajulikana mapema, ila part ya mume imebaki kutegemea mke atakavyosimama ( wanaume wengi wana ile 50/50 myth. Yani kwamba anategea mke akiteleza tu basi mume atateleza mara 2 yake

Wanaume wamekuwa wakiishi na wake zao kwa machale sana. Sasa unapoishi kutegea mtu akosee ili upate justification ya kufanya mambo yako hata mtu awe perfect vipi hutoona mazuri yake, coz umeconcentrate na negativities tu.

Ndoa ni kubebeana mizigo. But it seems hiyo habari inahusu tu wanawake kwa wanaume still ni msamiati. Uvumilivu ni terminology inayoapply kwa wanawake zaidi. Mke atavumilia mume akiwa hana kitu, akishindwa kumzalisha, akichepuka, nguvu za kiume kushney, bado utaona mke yupo radhi kumstiri mumewe. Sasa subiri mume awe na vijicent au mke ushindwe kuzaa. Akikuheshimu sana basi ataenda kuzaa nje kimya kimya otherwise utaambiwa tu "bana mimi siku zote nilikuwa na ndoto ya kuwa baba na kuongeza ukoo wangu, hivyo siwezi kuishi bila mtoto, kwa hiyo kuna mwanamke nimeamua kuzaa naye". Tena wanaume wengine bila hata haya unakuta anaongea mbele za watu "mke wangu kanizalia watoto wa kike tupu, lazima nitafute wa kiume". Mkeo ndo anapanga jinsia ya mtoto puuuuuuuu

Mke ni msaidizi kweli sasa sijui atamsaidiaje mume asiyesimama mahali pake sahihi. Kuna ndoa / testimonies naangaliaga hadi Nabaki kujiuliza "hivi me Ntaweza kuwa kama huyu dada kwenye ndoa". Maana mke anasimulia yaliyompata kwenye ndoa, unaona kabisa hayavumiliki lakini still mke hakuacha kuibeba ndoa yake. Makanisani wanawake wamejazana mno, na wengi utakuta wapo pale kumlilia Mungu kwa ajili ya ndoa zao. Sasa mwanamke jisahau tu kidogo uone kama kesho hujaletewa mke mdogo. Nyie wanaume ndo hamumjui Mungu au? Maana nyie kuwavumilia wake zenu mnaona kama mtadharaulika mtaitwa MABWEGE ( na hiki ndo kilichowajaa zaidi),

But trust me mume na yeye akiamua akasimama kwa ajili ya ndoa yake, ndoa inasimama. Msione kama jukumu la kuipa uhai ndoa yenu ni la mke zaidi. Mke akikosea wewe ndo wakumrudisha kwenye mstari. Kabla hujaanza kuweka rekodi ya mapungufu ya mkeo, basi anza kuhesabu yake mazuri yake. Michepuko inanyenyekea tu coz inajijua ni mijizi na kuna competition. Ukiugeuza kuwa mke na wenyewe utaanza kujisahau tu (na sio kama.huwa tunajisahau makusudi, majukumu ni mengi jamani). Msiishi kama nomadic pastoralist kudhani kuwa the pasture is always greener on the other side.

Kwenye ndoa msiishi kwa kutegeana Mungu, Kila mtu akeep it 100% ( 50/50 myth inaua ndoa nyingi), hata mwenzako akiteleza utamnyanyua coz umejicommit kujenga Ndoa bora. Shirikianeni, kuna tatizo basi wasilianeni mjue mnasolve vipi matatizo yenu. Msiwe watu wa kuhesabu mabaya tu, wekeni record ya mazuri ya wenza wenu, na muwe mnasameheana kwa dhati.
 
sasa kwanini umeongelea side moja tu mamii,
 
Kutoa lawama ni njia moja wapo ya kuhamisha mzigo toka sehemu moja kwenda nyingine.
Ni kama unajiona haupo responsible kwa tatizo lililotokea.
Wanawake jifunzeni kuishi kwa akili na wanaume wenu. Usitegemee mumeo akakubali kosa moja kwa moja.
 
maandiko matakatifu yanasema mwanamke mpumbavu huivunja nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe na tunasoma jinsi wanawake walivyo na nguvu kama akiamua kuitumia nafsi yake aliyopewa na mwenyezi Mungu mbona wanaume hatukohoi bira hata kwenda kwa babu pale bagamoyo? kwa hiyo nyumba ikiharibika wa kulaumiwa ni mwanamke, na ikisimama wa kusifiwa ni mwanamke
 
mwanamke ni dereva wa mapenzi ila inategemea anaendesha mapenzi ya iana gani? wanaume hawataacha kuturushia lawama na hii ni kutokana na background zao.. baba yake alikuwa kila tatizo anamrushia mama hasa yanayohusu watoto na majukumu ya familia.. kwa hilo tu usitegemee kukutana na mwanaume atakaye tetea mwanamke hata siku moja...

muhimu kutambua ni kuwa binadamu asiyelaumika ni sawa na mnyama ... so lawama zipo mapaka mwisho wa dunia....

ila ni heri lawama kuliko fedheha
 
Hahaha. Nimependa ulivyoanza. "Nimekuwa nikishuhudia", sema umekuwa ukishiriki. Kama ningekuwa Alien nimetumwa kuja kuwachunguza wanaume duniani, na nikakutana na comments zako kuwahusu, ningepata picha ni viumbe wa ajabu sana.

Ujumbe mzuri btw. Malezi ndio kila kitu.

Halafu Heaven Sent mama, hilo gazeti nimesoma tu kwa kuwa ni Missus. Aki-post mtu mwingine post ndefu hivyo, nam-report ale ban.
 
Last edited by a moderator:
Hahaha. Nimependa ulivyoanza. "Nimekuwa nikishuhudia", sema umekuwa ukishiriki. Kama ningekuwa Alien nimetumwa kuja kuwachunguza wanaume duniani, na nikakutana na comments zako kuwahusu, ningepata picha ni viumbe wa ajabu sana.

Ujumbe mzuri btw. Malezi ndio kila kitu.

Halafu Heaven Sent mama, hilo gazeti nimesoma tu kwa kuwa ni Missus. Aki-post mtu mwingine post ndefu hivyo, nam-report ale ban.

Hahaha yani una bahati naenda sehemu, so Imebidi nifupishe hizo notes. Ningeifanya novel kabisa
 
Last edited by a moderator:
My boss unajua katika hili me na wewe ni wamoja daima.

Naamini na Najua kuwa mke ndo anabeba kusudi la mume wake, ndiye msaidizi wa mume wake na hivyo hatima ya ndoa nyingi ipo mikononi mwa mke. Sasa inavyoonekana ndoa nyingi mke part yake huwa inajulikana mapema, ila part ya mume imebaki kutegemea mke atakavyosimama ( wanaume wengi wana ile 50/50 myth. Yani kwamba anategea mke akiteleza tu basi mume atateleza mara 2 yake

Wanaume wamekuwa wakiishi na wake zao kwa machale sana. Sasa unapoishi kutegea mtu akosee ili upate justification ya kufanya mambo yako hata mtu awe perfect vipi hutoona mazuri yake, coz umeconcentrate na negativities tu.

Ndoa ni kubebeana mizigo. But it seems hiyo habari inahusu tu wanawake kwa wanaume still ni msamiati. Uvumilivu ni terminology inayoapply kwa wanawake zaidi. Mke atavumilia mume akiwa hana kitu, akishindwa kumzalisha, akichepuka, nguvu za kiume kushney, bado utaona mke yupo radhi kumstiri mumewe. Sasa subiri mume awe na vijicent au mke ushindwe kuzaa. Akikuheshimu sana basi ataenda kuzaa nje kimya kimya otherwise utaambiwa tu "bana mimi siku zote nilikuwa na ndoto ya kuwa baba na kuongeza ukoo wangu, hivyo siwezi kuishi bila mtoto, kwa hiyo kuna mwanamke nimeamua kuzaa naye". Tena wanaume wengine bila hata haya unakuta anaongea mbele za watu "mke wangu kanizalia watoto wa kike tupu, lazima nitafute wa kiume". Mkeo ndo anapanga jinsia ya mtoto puuuuuuuu

Mke ni msaidizi kweli sasa sijui atamsaidiaje mume asiyesimama mahali pake sahihi. Kuna ndoa / testimonies naangaliaga hadi Nabaki kujiuliza "hivi me Ntaweza kuwa kama huyu dada kwenye ndoa". Maana mke anasimulia yaliyompata kwenye ndoa, unaona kabisa hayavumiliki lakini still mke hakuacha kuibeba ndoa yake. Makanisani wanawake wamejazana mno, na wengi utakuta wapo pale kumlilia Mungu kwa ajili ya ndoa zao. Sasa mwanamke jisahau tu kidogo uone kama kesho hujaletewa mke mdogo. Nyie wanaume ndo hamumjui Mungu au? Maana nyie kuwavumilia wake zenu mnaona kama mtadharaulika mtaitwa MABWEGE ( na hiki ndo kilichowajaa zaidi),

But trust me mume na yeye akiamua akasimama kwa ajili ya ndoa yake, ndoa inasimama. Msione kama jukumu la kuipa uhai ndoa yenu ni la mke zaidi. Mke akikosea wewe ndo wakumrudisha kwenye mstari. Kabla hujaanza kuweka rekodi ya mapungufu ya mkeo, basi anza kuhesabu yake mazuri yake. Michepuko inanyenyekea tu coz inajijua ni mijizi na kuna competition. Ukiugeuza kuwa mke na wenyewe utaanza kujisahau tu (na sio kama.huwa tunajisahau makusudi, majukumu ni mengi jamani). Msiishi kama nomadic pastoralist kudhani kuwa the pasture is always greener on the other side.

Kwenye ndoa msiishi kwa kutegeana Mungu, Kila mtu akeep it 100% ( 50/50 myth inaua ndoa nyingi), hata mwenzako akiteleza utamnyanyua coz umejicommit kujenga Ndoa bora. Shirikianeni, kuna tatizo basi wasilianeni mjue mnasolve vipi matatizo yenu. Msiwe watu wa kuhesabu mabaya tu, wekeni record ya mazuri ya wenza wenu, na muwe mnasameheana kwa dhati.


Umeolewa???
 
Sasa unapoishi kutegea mtu akosee ili upate justification ya kufanya mambo yako hata mtu awe perfect vipi hutoona mazuri yake, coz umeconcentrate na negativities tu.

Hili ni bonge la tatizo, kwa mtazamo huu hata mtu akutendee mazuri vipi ni kazi bure
 
Heaven Sent yo totaly right my dear, mpaka nalileta hili humu have seen alot in here and out there.
Niko ktk group moja la ladies wasapp tupo 50 ladies ambao hatujaolewa ni wawili tu, mule tunajifunza alot, jamani ndoa zina mazito hizi, nikaja kugundua kuwa mostly wanawake wanahangaika sana ktk kusimamia ndoa zao pale zinapoyumba na hupokea ushirikiano mdogo sana au hakuna kabisa kutoka kwa wanaume zao, wanavumilia mengi sana ila wanaume wanasubiri mwanamke akosee tu ili apate pa kutokea.

Sisemi kuwa wanawake tumekamilika au hatuna cha kulaumiwa lkn kwanini tulaumiane wakati mahusiano ni ya wawili? Why not work out on it wote?
 
Last edited by a moderator:
Peace n love na umenena vema na sie wanaume pia kwa sehemu tusijisahau na kuwalaumu saaana tu nyie
 
sasa kwanini umeongelea side moja tu mamii,

Nimeongelea upande mmoja kwasababu nimeona ndiko penye lawama mnooo, mnatulaumu sanaaa hamtaki kabisa kukubali kuwa nanyi mnachangia sana ktk hizi vurugu za ndoa/mahusiano.

Na hata sisi wanawake inapotokea mwanamke ana tatizo kwenye ndoa yake huwa tunashauriana tujiangalie wenyewe kwanza, wakuta mwanamke anahangaika atanyenyekea na kuomba msamaha hadi kwa makosa yasiyo yake, ila wapi!! Jamani hata sisi ni binadamu, ndio maana mwisho wa siku unakutana na mwanamke anakuwa katiliii kumbe ana mengi yaloujaza moyo wake, so haoni taabu kuumiza tu.
 
Sababu za kulaumiana ni nyingi,na inahitaji hekima ya mungu kuwaonyesha walaumu kuwa wewe ni mfano,vinginevyo wake kwa waume katika ndoa zitakuwa moto kila siku
-Kuhukumu :Matendo 28:1-6
-Kuongopa Ufunuo 20;7-8
-Kukata tamaa ya maisha-Numbers 32:6-10
_Hasira za machungu ya ndoa/mwenzi kuhamishia kwa watu kama adhabu,3:19,wakorintho
_Kuchanganyana n.a. ugumu wa maisha,Matendo 19:32
_Kuhalalisha dhambi, Isaya 5:2 kwa Kupofusha akili/blind mind
_Kukosa hofu ya mungu.
_Kugawanya familia kwa ugomvi.
_Kulipa k isasi
_Kutokuheshimu Maneno ya mungu.
_Kutokusamehe
_Kutokusikia sauti ya mungu.
-Chuki Wagalatia 6-
 
Back
Top Bottom