The Monk
Platinum Member
- Oct 12, 2012
- 20,318
- 46,060
naona mnadanganyana sasa!
SIMU 2000 ilikuwa ni kampuni iliyokuwa inahodhi mali za serikali wakati wa ubinafsishaji awamu ya tatu ya ben mkapa, hii kampuni ilimaliza kazi zake mwishoni wa awamu ya tatu na kazi zake nafikiri siku hizi zinafanya na consolidate holding corporation wapo pale mirambo st opposite na ofisi za world bank tanzania ,pia nilisikia CHC muda wake wakufanya kazi ulitakiwa uishe mwaka huu wa fedha,pia kulikuwa na kampuni nyingine zinazofanana na SIMU 2000 kama LART, ATHCO
kwa hiyo kile kituo kipya cha mabasi kilikuwa kinaodhiwa na hiyo kampuni inayoitwa SIMU 2000 Tanzania ltd ndio maana bado panatambulika kama eneo la kampuni tajwaa iliyohodhi eneo hilo
hilo swala la vibaka kuiba simu na kuuza shilingi 2000 wapate pesa ua unga ni uongo mkubwa,
unaweza kupata info za kampuni ya SIMU 2000 kupitia tovuti ya ::CHC Homepage::
Nafikiri hili ndio jibu sahihi