Kwanini kitambulisho cha ujasiriamali hakina risiti, jina, picha wala anuani?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,146
Mjadala wa uhalali na umuhimu wa kitambulisho cha Ujasiriamali umeibuka upya baada ya Lissu kukikosoa vikali na hapo hapo Magufuli kukitetea kwa nguvu zote.

Kuna maswali ya msingi ya kuhoji na kutafakari. Kwa mfano;

1. Kwanini kitambulisho kiuzwe elfu 20, badala ya kutolewa bure?
(Kama kitambulisho cha mpiga kura na NIDA kinatolewa bure, kwanini cha ujasiriamali kiuzwe?)

2. Kwanini malipo ya kukinunua hayana risiti, wakati sheria za serikali zinataka malipo yote halali yaendane na kutoa risiti?

3. Kwanini kitambulisho hakina jina, picha wala anwani ya mhusika anayekimiliki?
(Nini mantiki ya kumiliki kitambulisho ambacho hakikutambulishi wewe unayekimili?)
 
Mjadala wa uhalali na umuhimu wa kitambulisho cha Ujasiriamali umeibuka upya baada ya Lissu kukikosoa vikali na hapo hapo Magufuli kukitetea kwa nguvu zote...
Utapeli siku zote uko hivyo!

Sasa hivi inaonekana kitambulisho ni 'fake', Kama ni kudai pesa za hicho kitambulisho utamfuata nani!?

Utamfuata DC, RC ama Rais. Je una uthibitisho gani kuwa kitambulisho ni cha kwako na umekilipia shilingi ngapi!?

Wizi mtupu!
 
Mjadala wa uhalali na umuhimu wa kitambulisho cha Ujasiriamali umeibuka upya baada ya Lissu kukikosoa vikali na hapo hapo Magufuli kukitetea kwa nguvu zote.

Kuna maswali ya msingi ya kuhoji na kutafakari. Kwa mfano...
Kilidesigniwa na Jiwe mwenyewe ambaye, kwa bahati mbaya, hana uwezo mkubwa wa kufikiri.
 
Nahisi Magufuli ana matatizo ya akili kusema kitambulisho kinaweza kutumika kuombea mikopo bank
Matatizo yake ni makubwa sana,kama mtu anaweza kusema kua kitambulisho sio cha lazima,lakini pia leo kasema kua inafaida,!
Kitambukisho kile kinafaida gani baada ya kupigwa 20,000?
 
Nchi hii Ina maajabu yaani unanunua ndege cash halafu unashindwa kuweka picha kwenye kitambulisho,mlima Kilimanjaro unaungua moto unakodi wanafunzi wakazima sijui tumelogwa
At least you can show your stupidity at JF.
 
Mjadala wa uhalali na umuhimu wa kitambulisho cha Ujasiriamali umeibuka upya baada ya Lissu kukikosoa vikali na hapo hapo Magufuli kukitetea kwa nguvu zote....
Ni uhuni wa watu fulani kukusanya fedha za maskini wa nchi hii.
 
Mjadala wa uhalali na umuhimu wa kitambulisho cha Ujasiriamali umeibuka upya baada ya Lissu kukikosoa vikali na hapo hapo Magufuli kukitetea kwa nguvu zote.

Kuna maswali ya msingi ya kuhoji na kutafakari. Kwa mfano;

1. Kwanini kitambulisho kiuzwe elfu 20, badala ya kutolewa bure?
(Kama kitambulisho cha mpiga kura na NIDA kinatolewa bure, kwanini cha ujasiriamali kiuzwe?)

2. Kwanini malipo ya kukinunua hayana risiti, wakati sheria za serikali zinataka malipo yote halali yaendane na kutoa risiti?

3. Kwanini kitambulisho hakina jina, picha wala anwani ya mhusika anayekimiliki?
(Nini mantiki ya kumiliki kitambulisho ambacho hakikutambulishi wewe unayekimili?)

Kichwa maji kabla ya kupewa kitambulisho unapewa fomu ya kujaza na kwenye fomu kuna andikwa yote haya na picha ya muhusika
 
Back
Top Bottom