Kwanini Kisiwa cha Mafia sio sehemu ya Zanzibar?

Kwa mujibu wa historia na post yako inaonyesha Pwani ya kenya na kisiwa cha Lamu sultan, wa zanzibar alizikodisha kwa muingereza. Je huo muda wa kukodi haujesha na kama umeisha ni nani aidai hii sehemu, smz au jamhuri ya muungano au MRC (mombasa republican council).
Hadi uhuru Waingereza walitazama Kenya kisheria kuwa na sehemu mbili:
a) Protectorate of Kenya, yaani kanda la kilomita 16 (=maili 10) kwenye pwani la bahari, pamoja na visiwa vyote. Hili lilikuwa kanda ambalo waliwahi kukodi kutoka Sultani, wakiendelea kulipa kwenye makisio ya Zanzibar. Kisheria walitawala hapa kwa niaba ya Sultani.

b) Kenya colony, yaani maeneo yote mengine ya Kenya.

Hali halisi walitawala yote kama sehemu moja. Wakati wa uhuru wanasiasa wa Kenya bara hawakuwa tayari kutambua hali za Sultani, hivyo Waingereza walinyamaza tu na kukabidhi yote kwa serikali ya Nairobi. Hata hivyo, wenyeji wengine walipinga. Katika historia hii uko pia msingi wa mahakama za kadhi (mahakama za Kiislamu) zilizopo katika Kenya, maana Waingereza walitunza utaratibu waliokuta.
 
Hili ndio swali ambalo wengi hasa Watanzani huliliza mara kwa mara na ni swali ambalo popote ukijitambulisha kama mwenyeji wa Mafia basi aghalabu kwa mtu aliewahi kukifahamu kisiwa hiki kwa kusikia atakuuliza swali la msisitizo zaidi, Mafia si ya huko Zanzibar?

Wengi hawafahamu kua Kisiwa cha Mafia kinachopatikana bahari ya Hindi kusini mashariki mwa Jiji la Dar es Salaam ni sehemu ya Tanzania bara na ni moja ya Wilaya za Mkoa wa Pwani baada ya Wilaya ya Kibaha, Kibiti, Kisarawe, Rufiji, Mkuranga, Bagamoyo na Chalinze.

Kuifungamanisha Mafia na Zanzibar kunatokana na ukweli kua kijografia Mafia huwekwa pamoja na visiwa vya Zanzibar yaani Unguja na Pemba ukijumuisha visiwa vingine vidogo kuzunguuka unguja na pemba na hutambulika kama Funguvisiwa Zanzibar au kwa kimombo hufahamika kama Zanzibar Archipelago.

Hivyo basi, makala hii inajaribu kueleza kwa kina ni kwa namna gani Kisiwa cha Mafia ambacho wakati fulani kilikua chini ya dola ya Zanzibar kilihama (ama kuhamishwa) na kua sehemu ya Jamuhuri ya Tanganyika iliyojipatia uhuru wake mwaka 1961.

Historia fupi ya kisiwa cha Mafia

Japo inafahamika kua watu wa mwanzo kuweka makazi ya kudumu katika kisiwa cha Mafia walikua ni Wamwera waliotoka Songo Songo Kilwa lakini Profesa Felix Chami aligundua kua watu walianza kuishi katika Mafia labda tangu nyuma ya Karne ya Pili. Ushahidi wa mabaki ya vyungu na vikagae vyenye asili ya bara Asia vilivyopatikana kwa kufukuliwa katika maeneo ya Mlongo, Ng'ombeni, Juani na Chole kisiwani Mafia yanadhihirisha urefu wa historia ya Mafia na mahusiano yake na wageni nyuma ya karne kumi.

Kati ya karne ya 11 na 13 Mafia ilianza kutawaliwa na Washirazi, ambao in Waarabu toka Persia walikua watawala wa Kilwa. Wakiongozwa na Bashati walianzisha makazi yao kusini magharibi ya kisiwa kikuu cha Mafia katika eneo la Rasi Kisimani Mafia na eneo la Kua linalopatikana Kusini Magharibi mwa Kisiwa kidogo cha Juani kilicho Mashariki mwa Kisiwa Kikuu cha Mafia.

Kisimani na Kua kila moja iliwahi kua Mji Mkuu wa Mafia, Magofu yaliyopo sasa maeneo hayo yanayovuta wageni kuyatembelea ni kielelezo cha umaarufu wa maeneo haya nyakati hizo.

Wasakalava kabila toka Madagascar wanatajwa kama sababu ya kufa kwa Mji wa Kua ambapo mwaka 1829 Wasakalava (wanatajwa kama kabila la wala watu) wakiwa katika Majahazi zaidi ya 80 waliuvamia Mji wa Kua na kuwaua na kuwala nyama wenyeji mithili ya Simba alapo swala na inatajwa baadhi ya wenyeji wa Kua waliokamatwa na walichukuliwa kama watumwa na wengine walikimbilia Chole na huu ulikua ndio mwisho wa Mji wa Kua na mpaka leo hii kua haikuwahi kukaliwa tena na binaadamu ulihamwa jumla yamebaki magofu makubwa yaliyo porini bila uangalizi wowote. Kwa upande wa Mji wa Rasi Kisimani wenyewe ulisambaratishwa kimbunga kizito katikati ya mwaka 1872 na kupelekea anguko lake.

Uvamizi wa Mji wa Kua uliusukuma utawala wa Zanzibar chini ya Sultani kutuma sehemu ya jeshi lake ambao ni Wabaluchi (waarabu hivi) kuja kupambana na Wasakalava na kufanikiwa kuwafurumusha na kuawaua wote katika Bahari ya Mtwara wakati wakiwa mbioni kuondoka kurudi Kwao Madagascar.

Baadhi ya watu hao Wasultani ambao ni Wabeluchi waliamua kubaki Mafia na kuanzisha makazi yao eneo la Kitoni. Watu wa asili hiyo wameendelea kuwepo mpaka leo hii kisiwani Mafia na hutambulika kama Waburushi waliotapakaa Katika maeneo ya Usewe, Kitoni na Chem Chem (Mfano wa watu hawa no watu maarufu kisiwani humo kama Mzee Seif Sultan, Dadi Karimu na Shaha aliwahi kua Mbunge wa Mafia kuanzia 2000 mpaka 2015)

Kuanguka kwa Miji ya Kua na Kisimani kulepelekea kuibuka kwa Kisiwa cha Chole kama mji mkuu wa Mafia na eneo muhimu kibiashara.

KISIWA CHA MAFIA CHAUZWA

Hili ndio jambo ambalo wengi hawalijui na laiti kama isingetokea leo basi Mafia ingekua sehemu ya Jamhuri ya Zanzibar sambamba na Unguja na Pemba. Je ni nani aliiuza Mafia? Na je mnunuzi alikua nani? Na ilipelekeaje Mafia kuhama toka Zanzibar na kua Tanganyika?

Yafaa tukumbuke kua baada ya utawala wa wareno Afrika ya Mashariki kuangushwa na Waarabu wa Oman mnamo mwaka 1698, eneo lote la Visiwa vya Unguja, Pemba na kisiwa cha Mafia pamoja ukanda wote wa Pwani ya Afrika ya Mashariki kuanzia rasi ya Delgado (Sasa Msumbiji) mpaka eneo la Kipini Kenya mpaka Mogadishu likawa chini ya Utawala wa Sultani wa Oman.

Hata baada ya mkutano was Berlin ambao uliligawa Bara la Africa kwa Mataifa mbalimbali ya Ulaya bado Kisiwa cha Mafia pamoja upana wa maili 10 mwambao wa Pwani katika ukanda wa nchi za maziwa makuu bado ziliachwa chini ya utawala wa Zanzibar. Choko choko za Ujerumani chini ya Mbabe Karl Peters dhidi ya maslahi ya Uingeleza na dola ya Zanzibar zilipelekea kufanyika kwa mkataba kati ya serikali ya Uingereza na Ujerumani ambapo mbali na mambo mengine walikubaliana kwamba Ujerumani sharti auheshimu utawala wa Zanzibar pamoja na eneo lote la pwani linalomilikiwa na Zanzibar.

Licha ya makubaliano hayo ya mwaka 1890, kati ya mwaka 1886 na mwaka 1896 utawala Zanzibar iliamua kuyakodisha ama kuyauza maeneo yake yote ya ukanda Pwani na baadhi ya Visiwa nae kubakia Visiwa vya Zanzibar pekee. Kwa mfano eneo la Pwani ya Kenya na Kisiwa cha Lamu yalikodishwa kwa Waingereza, Pwani ya Mogadishu ilikodishwa na kisha kuuzwa kwa Serikali ya Italia
Ujerumani iliilipa Serikali ya Zanzibar chini ya Sultan Sayyed Ali Bin Said kiasi cha milioni nne fedha za Oman kama gharama za kukinunua kisiwa cha Mafia na ukanda wa Pwani ya Tanganyika.

Kwa mara ya kwanza mwaka 1892 Ujerumani ikamleta mwakilishi wake Mafia kuja kusimika utawala wao ambao mwanzoni walichagua kisiwa kidogo cha Chole kilicho upande wa Mashariki wa kisiwa kikuu cha Mafia kama Mji Mkuu na Makao Makuu ya utawala wao. Kabla ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia kuanza, Ujerumani alishahamisha makao yake makuu kisiwani Mafia toka kisiwa cha Chole kuja Kilindoni mahala ambapo sasa ndio Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya Mafia au Bomani kama livyofahamika sasa.

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ambayo Mafia ilipiganiwa eneo la Ng'ombeni Mlongo (mpaka leo eneo hili kuna mti wa muembe unaoitwa Muembe Vita) na Uingereza kuibuka mshindi, Kisiwa cha Mafia pamoja Tanganyika ukiwemo ukanda wa Pwani kwa pamoja ukawa chini ya Uingereza na baada ya uhuru tarehe tisa mwezi wa kumi na mbili mwaka alfu tisaa mia na sitini na moja sehemu ya Tanganyika huru na Hayati mwalimu Nyerere akawa Waziri Mkuu wake wa kwanza.

HITIMISHO

Kama tulivyoona kwenye makala hii hapo juu kua Mafia ilikua sehemu ya Zanzibar mpaka mwaka 1890 ambapo Sultan wa Zanzibar Sayyed Ali bin Saad aliamua kuwauzia Ujerumani. Kwa maamuzi haya Kisiwa cha Mafia kikatengwa na Dada zake Unguja na Pemba na kikasukumizwa bila kupenda kwa Dada wa kufikia Tanganyika almaarufu Tanzania bara.

Swali la nje ya chaki: Hali ya kisiwa cha Mafia kiuchumi, Kisiasa na Kijamii. Je, ingekua bora kama ingekua sehemu moja na Dada yake Zanzibar ama ingekua 'dhoofu-lhali' zaidi ya sasa ilivyo kwa 'Dada wa kufikia'Tanganyika?

Karibu kwa maoni na ushauri
Umesimulia historia vizuri sana.
Niongeza mawili tu:
1) Ni kweli wenyeji wa Mafia husimulia hao Wasakalava wa Madagaska walivamia Kua kwenye kisiwa cha Juani (kisiwa cha pili cha Mafia) na kula watu wote. Ila tu hii ya kula watu tusichukue kama habari ya kihistoria. Wasakalava wako hadi leo pala Madagaska, hakuna uthibitisho kwamba walikula watu. Katika karne ya 18 walihofiwa kama watu waliovinda watumwa hadi Ngazija (Komoro) na kuwauza kwa Wafaransa na Waarabu. Kuna taarifa nyingi kuhusu shughuli hizi. Linganisha hapa Sakalava people - Wikipedia

2. Kuhusu Mafia na Zanzibar - unaongea kama wangepaswa kuchagua baina Tanganyika na Zanzibar. Hapa unataja Tangansika kama "Tanzania bara". Ila tu hii ni historia ya juzijuzi tu, si ya karne ya 19. Jina Tanganyika lilichaguliwa na Waingereza walipotafuta jina baada ya kutwaa koloni ya Wajerumani, mnamo 1920 hivi waliamua watumia "Tanganyika". Hadi kuja kwa Wajerumani kulikuwa na maeneo ya pwani (bila tofauti ya visiwa au "bara") yaliyokuwa chini ya Sultani na maeneo mengine ya ndani ambako Sultani hakuwa na athira; kisehemu nchi na maeneo ya kujitegemea (kama Usangu, Uhehe, nchi nyingi za Wachagga...) au sehemu bila serikali kuu ambako kila kijiji kilijitawala.

Ukiuliza je Mafia ingefaa kuwa pamoja na Zanzibar - basi swali hili ungeuliza pia kuhusu Tanga, Pangani, Saadani, Bagamoyo, Dar es Salaam, Kilwa, Mikindani, LIndi . . . . maana sehemu hizo zilikjuwa sawa na Mafia hata kama si kisiwa.
 
HIVI HAKUNA NAMNA TUNAWEZA KUWA NA TANZANIA AMBAYO ZANZIBAR NI MIKOA KAMA BARA. IWE SERKALI MOJA, RAISI MMOJA! IKIBIDI ZANZIBAR IPEWE SPECIAL TREATMENT KATIKA HUDUMA KI MAISHA NA MIUNDOMBINU ILI WARIDHIKE. ITASAIDIA KUPUNGUZA GHARAMA ZA UENDESHAJI WA TANZANIA MAMA.
 
Nasema hivyo sababu mm ni mshirazi kutoka kisiwa cha mafia hila rafiki zangu wengi uniita mm mpemba na sina namna inabidi nikubaliane na hali

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Ni wachache sana kilwa waliochanganya...ila ni kweli historia..kwa mbali inawaweka karibu...lakini asilimia kubwa watu wa kilwa wanafanana sana na wa Tanganyika.. ...
 
HIVI HAKUNA NAMNA TUNAWEZA KUWA NA TANZANIA AMBAYO ZANZIBAR NI MIKOA KAMA BARA. IWE SERKALI MOJA, RAISI MMOJA! IKIBIDI ZANZIBAR IPEWE SPECIAL TREATMENT KATIKA HUDUMA KI MAISHA NA MIUNDOMBINU ILI WARIDHIKE. ITASAIDIA KUPUNGUZA GHARAMA ZA UENDESHAJI WA TANZANIA MAMA.
huo utakuwa ni upumbavu kwa upande wa zanzibar, maana ni haki ya zanzibar kuwa nchi, wao ni sehemu ya muungano kwa hiyari. ila wao kama wao ni nchi kamili kabisa, ingekuwa muungano haukutokea, zanzibar ingebaki kuwapo na ingekuwa nchi jirani. na kwa vyovyote vile hawayokubali serikali yao ya kitaifa kufutwa na kiongozi wao hawatokubali aache kuitwa na kupambanuliwa kwa cheo na wadhifa wa urais
 
mbona tanganyika ilimezwa na zanzibar na hakuna anayepaparika? nionyeshe nchi ya Tanganyika! Ni kwa sabab watanganyika wanaelewa kuwa mipaka iliwekwa na binadam tena kwa maslahi yake ila undugu wetu uko pale pale. na hakuna asiyejua umoja ni nguvu. tukifuta mipaka manake tunarudi kwenye uhasilia na uhalisia wetu. hata mzanzibar anakuwa na nafasi kuwa rais wa Tanzania nzima kama anavyotokea wa geita au musoma au unguja. Nchi itaendeshwa kwa gharama nafuu. ubinafsi tu ndo watusumbua. mbona hushangai USA!
 
HIVI HAKUNA NAMNA TUNAWEZA KUWA NA TANZANIA AMBAYO ZANZIBAR NI MIKOA KAMA BARA. IWE SERKALI MOJA, RAISI MMOJA! IKIBIDI ZANZIBAR IPEWE SPECIAL TREATMENT KATIKA HUDUMA KI MAISHA NA MIUNDOMBINU ILI WARIDHIKE. ITASAIDIA KUPUNGUZA GHARAMA ZA UENDESHAJI WA TANZANIA MAMA.
Umenena sana mkuu japo kimasikhara

Mambo kama sisi ni/sio taifa hayana mantiki sana ni kujitaabisha tu kidunia

Mimi naona hii iliyopo inaleta sana "Sisi/Wao"

Vunja Tanganyika, vunja Zanzibar mazima weka kitu kimoja

Mbona Mafia ni kisiwa lakini iko Bara

Zanzibar pia inaweza kuwa Bara

Lakini sasa utaratibu ukishafanyika hata hiyo bara haitakuwepo, itakuwa nchi mpja tu
 
Naam naam
mbona tanganyika ilimezwa na zanzibar na hakuna anayepaparika? nionyeshe nchi ya Tanganyika! Ni kwa sabab watanganyika wanaelewa kuwa mipaka iliwekwa na binadam tena kwa maslahi yake ila undugu wetu uko pale pale. na hakuna asiyejua umoja ni nguvu. tukifuta mipaka manake tunarudi kwenye uhasilia na uhalisia wetu. hata mzanzibar anakuwa na nafasi kuwa rais wa Tanzania nzima kama anavyotokea wa geita au musoma au unguja. Nchi itaendeshwa kwa gharama nafuu. ubinafsi tu ndo watusumbua. mbona hushangai USA!
 
Nakubaliana na mwandishi juu ya historia ya kisiwa cha Mafia, na kwamba Sultan alikuja kukiuza kwa Wajerumani, na kwamba kwenye Berlin Conference, Tanganyika iliangukia mikononi mwa mjerumani. Ila napata wasiwasi juu ya ulivojaribu kukitoa kisiwa hicho mikononi mwa mjerumani na kuja kwa Waingereza, na hasa unapohusisha mapigano ya Vita ya Kwanza ya Dunia

Kwa ufahamu wangu, baada ya kumalizika kwa WWI kulifanyika mkutano uliokuja na kitu kinaitwa Versailles' Treaty, ambao pamoja na mambo mengine, iliafikiwa kuwa mjerumani anyang'anywe makoloni mengi Africa, ikiwemo Tanganyika, na Tanganyika ikawekwa chini ya uangalizi wa Uingereza.

Na kwasababu tayari Mafia ilikuwa chini ya mjerumani, ambaye koloni lake la Tanganyika (ikihusisha Kisiwa cha Mafia) na kupewa mwingereza, ndivyo ambavyo kisiwa hicho kilivohama kutoka kwa mjerumani na kuja kuwa sehemu ya Tanganyika chini ya uangalizi wa mwingereza
 
Hili ndio swali ambalo wengi hasa Watanzani huliliza mara kwa mara na ni swali ambalo popote ukijitambulisha kama mwenyeji wa Mafia basi aghalabu kwa mtu aliewahi kukifahamu kisiwa hiki kwa kusikia atakuuliza swali la msisitizo zaidi, Mafia si ya huko Zanzibar?

Wengi hawafahamu kua Kisiwa cha Mafia kinachopatikana bahari ya Hindi kusini mashariki mwa Jiji la Dar es Salaam ni sehemu ya Tanzania bara na ni moja ya Wilaya za Mkoa wa Pwani baada ya Wilaya ya Kibaha, Kibiti, Kisarawe, Rufiji, Mkuranga, Bagamoyo na Chalinze.

Kuifungamanisha Mafia na Zanzibar kunatokana na ukweli kua kijografia Mafia huwekwa pamoja na visiwa vya Zanzibar yaani Unguja na Pemba ukijumuisha visiwa vingine vidogo kuzunguuka unguja na pemba na hutambulika kama Funguvisiwa Zanzibar au kwa kimombo hufahamika kama Zanzibar Archipelago.

Hivyo basi, makala hii inajaribu kueleza kwa kina ni kwa namna gani Kisiwa cha Mafia ambacho wakati fulani kilikua chini ya dola ya Zanzibar kilihama (ama kuhamishwa) na kua sehemu ya Jamuhuri ya Tanganyika iliyojipatia uhuru wake mwaka 1961.

Historia fupi ya kisiwa cha Mafia

Japo inafahamika kua watu wa mwanzo kuweka makazi ya kudumu katika kisiwa cha Mafia walikua ni Wamwera waliotoka Songo Songo Kilwa lakini Profesa Felix Chami aligundua kua watu walianza kuishi katika Mafia labda tangu nyuma ya Karne ya Pili. Ushahidi wa mabaki ya vyungu na vikagae vyenye asili ya bara Asia vilivyopatikana kwa kufukuliwa katika maeneo ya Mlongo, Ng'ombeni, Juani na Chole kisiwani Mafia yanadhihirisha urefu wa historia ya Mafia na mahusiano yake na wageni nyuma ya karne kumi.

Kati ya karne ya 11 na 13 Mafia ilianza kutawaliwa na Washirazi, ambao in Waarabu toka Persia walikua watawala wa Kilwa. Wakiongozwa na Bashati walianzisha makazi yao kusini magharibi ya kisiwa kikuu cha Mafia katika eneo la Rasi Kisimani Mafia na eneo la Kua linalopatikana Kusini Magharibi mwa Kisiwa kidogo cha Juani kilicho Mashariki mwa Kisiwa Kikuu cha Mafia.

Kisimani na Kua kila moja iliwahi kua Mji Mkuu wa Mafia, Magofu yaliyopo sasa maeneo hayo yanayovuta wageni kuyatembelea ni kielelezo cha umaarufu wa maeneo haya nyakati hizo.

Wasakalava kabila toka Madagascar wanatajwa kama sababu ya kufa kwa Mji wa Kua ambapo mwaka 1829 Wasakalava (wanatajwa kama kabila la wala watu) wakiwa katika Majahazi zaidi ya 80 waliuvamia Mji wa Kua na kuwaua na kuwala nyama wenyeji mithili ya Simba alapo swala na inatajwa baadhi ya wenyeji wa Kua waliokamatwa na walichukuliwa kama watumwa na wengine walikimbilia Chole na huu ulikua ndio mwisho wa Mji wa Kua na mpaka leo hii kua haikuwahi kukaliwa tena na binaadamu ulihamwa jumla yamebaki magofu makubwa yaliyo porini bila uangalizi wowote. Kwa upande wa Mji wa Rasi Kisimani wenyewe ulisambaratishwa kimbunga kizito katikati ya mwaka 1872 na kupelekea anguko lake.

Uvamizi wa Mji wa Kua uliusukuma utawala wa Zanzibar chini ya Sultani kutuma sehemu ya jeshi lake ambao ni Wabaluchi (waarabu hivi) kuja kupambana na Wasakalava na kufanikiwa kuwafurumusha na kuawaua wote katika Bahari ya Mtwara wakati wakiwa mbioni kuondoka kurudi Kwao Madagascar.

Baadhi ya watu hao Wasultani ambao ni Wabeluchi waliamua kubaki Mafia na kuanzisha makazi yao eneo la Kitoni. Watu wa asili hiyo wameendelea kuwepo mpaka leo hii kisiwani Mafia na hutambulika kama Waburushi waliotapakaa Katika maeneo ya Usewe, Kitoni na Chem Chem (Mfano wa watu hawa no watu maarufu kisiwani humo kama Mzee Seif Sultan, Dadi Karimu na Shaha aliwahi kua Mbunge wa Mafia kuanzia 2000 mpaka 2015)

Kuanguka kwa Miji ya Kua na Kisimani kulepelekea kuibuka kwa Kisiwa cha Chole kama mji mkuu wa Mafia na eneo muhimu kibiashara.

KISIWA CHA MAFIA CHAUZWA

Hili ndio jambo ambalo wengi hawalijui na laiti kama isingetokea leo basi Mafia ingekua sehemu ya Jamhuri ya Zanzibar sambamba na Unguja na Pemba. Je ni nani aliiuza Mafia? Na je mnunuzi alikua nani? Na ilipelekeaje Mafia kuhama toka Zanzibar na kua Tanganyika?

Yafaa tukumbuke kua baada ya utawala wa wareno Afrika ya Mashariki kuangushwa na Waarabu wa Oman mnamo mwaka 1698, eneo lote la Visiwa vya Unguja, Pemba na kisiwa cha Mafia pamoja ukanda wote wa Pwani ya Afrika ya Mashariki kuanzia rasi ya Delgado (Sasa Msumbiji) mpaka eneo la Kipini Kenya mpaka Mogadishu likawa chini ya Utawala wa Sultani wa Oman.

Hata baada ya mkutano was Berlin ambao uliligawa Bara la Africa kwa Mataifa mbalimbali ya Ulaya bado Kisiwa cha Mafia pamoja upana wa maili 10 mwambao wa Pwani katika ukanda wa nchi za maziwa makuu bado ziliachwa chini ya utawala wa Zanzibar. Choko choko za Ujerumani chini ya Mbabe Karl Peters dhidi ya maslahi ya Uingeleza na dola ya Zanzibar zilipelekea kufanyika kwa mkataba kati ya serikali ya Uingereza na Ujerumani ambapo mbali na mambo mengine walikubaliana kwamba Ujerumani sharti auheshimu utawala wa Zanzibar pamoja na eneo lote la pwani linalomilikiwa na Zanzibar.

Licha ya makubaliano hayo ya mwaka 1890, kati ya mwaka 1886 na mwaka 1896 utawala Zanzibar iliamua kuyakodisha ama kuyauza maeneo yake yote ya ukanda Pwani na baadhi ya Visiwa nae kubakia Visiwa vya Zanzibar pekee. Kwa mfano eneo la Pwani ya Kenya na Kisiwa cha Lamu yalikodishwa kwa Waingereza, Pwani ya Mogadishu ilikodishwa na kisha kuuzwa kwa Serikali ya Italia
Ujerumani iliilipa Serikali ya Zanzibar chini ya Sultan Sayyed Ali Bin Said kiasi cha milioni nne fedha za Oman kama gharama za kukinunua kisiwa cha Mafia na ukanda wa Pwani ya Tanganyika.

Kwa mara ya kwanza mwaka 1892 Ujerumani ikamleta mwakilishi wake Mafia kuja kusimika utawala wao ambao mwanzoni walichagua kisiwa kidogo cha Chole kilicho upande wa Mashariki wa kisiwa kikuu cha Mafia kama Mji Mkuu na Makao Makuu ya utawala wao. Kabla ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia kuanza, Ujerumani alishahamisha makao yake makuu kisiwani Mafia toka kisiwa cha Chole kuja Kilindoni mahala ambapo sasa ndio Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya Mafia au Bomani kama livyofahamika sasa.

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ambayo Mafia ilipiganiwa eneo la Ng'ombeni Mlongo (mpaka leo eneo hili kuna mti wa muembe unaoitwa Muembe Vita) na Uingereza kuibuka mshindi, Kisiwa cha Mafia pamoja Tanganyika ukiwemo ukanda wa Pwani kwa pamoja ukawa chini ya Uingereza na baada ya uhuru tarehe tisa mwezi wa kumi na mbili mwaka alfu tisaa mia na sitini na moja sehemu ya Tanganyika huru na Hayati mwalimu Nyerere akawa Waziri Mkuu wake wa kwanza.

HITIMISHO

Kama tulivyoona kwenye makala hii hapo juu kua Mafia ilikua sehemu ya Zanzibar mpaka mwaka 1890 ambapo Sultan wa Zanzibar Sayyed Ali bin Saad aliamua kuwauzia Ujerumani. Kwa maamuzi haya Kisiwa cha Mafia kikatengwa na Dada zake Unguja na Pemba na kikasukumizwa bila kupenda kwa Dada wa kufikia Tanganyika almaarufu Tanzania bara.

Swali la nje ya chaki: Hali ya kisiwa cha Mafia kiuchumi, Kisiasa na Kijamii. Je, ingekua bora kama ingekua sehemu moja na Dada yake Zanzibar ama ingekua 'dhoofu-lhali' zaidi ya sasa ilivyo kwa 'Dada wa kufikia'Tanganyika?

Karibu kwa maoni na ushauri
Nini mafia? Hata unguja na pemba ni sehemu ya tanganyika isipokuwa kuna hulka imejijenga miongoni mwa watu wa visiwani kuwa wao ni waoman na washirazi kiasili ndio wenye nia ovu ya kutaka utaifa wao kando na tanganyika lkn ukweli usiopingika ardhi yote ya visiwani mali ya tanganyika. Kama hao machotara wanataka waende huko wanapojnasibu oman na iran lkn ardhi ni mali ya tanganyika hata kijiografia oman na iran wapi na wapi? Lkn tanganyika na visiwa vyote ni pua na mdomo ardhi yetu ya tanganyika haitaporwa kirahisi hivo mungu ibariki tanganyika
 
Mafia kweli ni kisiwa lakini si visiwa vyote viwe sehemu ya Zanzibar. Mafia iko karibu sana na Wilaya ya Kibiti kwa sasa, na kuna visiwa vingine kama Mbwera nk. Na usafiri wa kwenda Mafia ni rahisi sana kutokea Nyamisati ambayo ipi wilaya ya Kibiti (zamani ilikuwa wilaya ya Rufiji)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom