Inawezekana
chinchilla coat maana hakuna sababu ya msingi ya kufanya kesi hizo zisiwe na dhamana zaidi ya kukomoana. South Africa mpaka kesi za mauaji zina dhamana
Kuna yule jamaa ndugu yake Rostam Aziz alikua na kesi ya utakatishaji pesa kwa kukutwa na Dollar 9000 tu kwenye akaunti yake! Huyo ni mtu ambaye hua anafanya biashara za mabilioni! Kama asingejiongeza na kukiri kosa hivyo kuhukumiwa kulipa faini ya shilingi milioni mia mbili angeweza kukaa mahabusu hata miaka mitano wakati kesi yake ikiendelea!
Na utaona siku wakija kurejesha dhamana kwenye kesi hizi za utakatishaji basi mashtaka mengi watakayokua wanafunguliwa watu yatakua hayahusishi hili shtaka maana watu hua wanabambikiwa makusudi ili tu wakae ndani!