Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,096
Nimetoka kutazama matangazo ya kampeni ya Tokomeza Zero iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo. Nikavutiwa nayo.
Hata hivyo, nimeshangaa kuona kampeni hii imeweka focus kwa wanafunzi wa kike pekee.. Hii imekaaje? Vipi kuhusu watoto wa kiume? Kwanini isiwe jumuishi?
Nampongeza sana DC Jokate kwa dhamira yake ya kutatua changamoto za elimu katika wilaya anayoiongoza.
Sote tunajua mikoa ya Pwani inakabiliwa na matatizo mengi na mara nyingi shule za huko zimekuwa zikishika mkia kwenye matokeo ya mitihani. Hivyo, uamuzi huu wa DC Mwegelo ni wa kuungwa mkono kwa nguvu zote.
Hivi karibuni kutakuwa na harambee ya uchangishaji fedha (fundraising) itakayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano ambapo kiingilio kitaanzia laki 1 kwa MTU mmoja na Milioni 1 kwa VIP.
Kama kuna ufafanuzi wa hili suala ningeomba nipatiwe maana imekuwa kawaida mtoto wa kiume kuwekwa kando kwa kisingizio cha kumuinua mtoto wa kike.
Hongera tena DC Jojo kwa initiative nzuri!
Hata hivyo, nimeshangaa kuona kampeni hii imeweka focus kwa wanafunzi wa kike pekee.. Hii imekaaje? Vipi kuhusu watoto wa kiume? Kwanini isiwe jumuishi?
Nampongeza sana DC Jokate kwa dhamira yake ya kutatua changamoto za elimu katika wilaya anayoiongoza.
Sote tunajua mikoa ya Pwani inakabiliwa na matatizo mengi na mara nyingi shule za huko zimekuwa zikishika mkia kwenye matokeo ya mitihani. Hivyo, uamuzi huu wa DC Mwegelo ni wa kuungwa mkono kwa nguvu zote.
Hivi karibuni kutakuwa na harambee ya uchangishaji fedha (fundraising) itakayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano ambapo kiingilio kitaanzia laki 1 kwa MTU mmoja na Milioni 1 kwa VIP.
Kama kuna ufafanuzi wa hili suala ningeomba nipatiwe maana imekuwa kawaida mtoto wa kiume kuwekwa kando kwa kisingizio cha kumuinua mtoto wa kike.
Hongera tena DC Jojo kwa initiative nzuri!