VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Tangu lianze vuguvugu la kuhama chamani-kutoka CCM kwenda kwingineko,wahamaji wamekuwa wakihamia CHADEMA. Kuanzia Simiyu hadi Monduli;Shinyanga hadi Muleba mambo ni hayo hayo.
Wamehama madiwani wa kutosha (wa mwisho ni wa jana wa kule Kamachumu Muleba). Wabunge wawili nao wameshagoma kuchukua fomu za CCM: Lembeli na Bulaya.
Pamoja na kwamba hawajataja vyama watakavyoibukia, I bet, wataibukia CHADEMA. Watakapoamua kugombea nje ya CCM. Labda wasigombee kabisa. Vuguvugu hili,kwetu wachambuzi wa kisiasa,lilitarajiwa. Majeraha ya Dodoma yatapuuzwa lakini chama kitaumizwa. Hilo lipo wazi kama nazi. Tutaficha kucha lakini upele utatuumbua.
Kuhama chama hakunishtui. Hakunioneshi tukio la kustaajabisha kisiasa. Wapo wazito kabisa chamani,kama Wasira,Tambwe na Makongoro,waliohama wakimwaga lawama lakini wakarejea wakifurahia. Na hata kuponda walipopapenda wakati wanakwenda.
Swali langu,hasa wakati huu wa uchaguzi,ni kwanini iwe CHADEMA tu? Kwanini kila mhamaji anahamia CHADEMA tu na si kwingineko? Tanzania haina vyama viwili. Waende na kwingine.
Kutakuwa na tatizo au tuzo ima wanakotoka au wanakowenda. Si bure! Viongozi wa CCM na CHADEMA wamulike vyema kabla ya kufungwa kwa dirisha hili la usajili ambao kwasasa halihitaji akili. Kutakuwa na jambo,na kuna mkono mtu nawaambia!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.
Wamehama madiwani wa kutosha (wa mwisho ni wa jana wa kule Kamachumu Muleba). Wabunge wawili nao wameshagoma kuchukua fomu za CCM: Lembeli na Bulaya.
Pamoja na kwamba hawajataja vyama watakavyoibukia, I bet, wataibukia CHADEMA. Watakapoamua kugombea nje ya CCM. Labda wasigombee kabisa. Vuguvugu hili,kwetu wachambuzi wa kisiasa,lilitarajiwa. Majeraha ya Dodoma yatapuuzwa lakini chama kitaumizwa. Hilo lipo wazi kama nazi. Tutaficha kucha lakini upele utatuumbua.
Kuhama chama hakunishtui. Hakunioneshi tukio la kustaajabisha kisiasa. Wapo wazito kabisa chamani,kama Wasira,Tambwe na Makongoro,waliohama wakimwaga lawama lakini wakarejea wakifurahia. Na hata kuponda walipopapenda wakati wanakwenda.
Swali langu,hasa wakati huu wa uchaguzi,ni kwanini iwe CHADEMA tu? Kwanini kila mhamaji anahamia CHADEMA tu na si kwingineko? Tanzania haina vyama viwili. Waende na kwingine.
Kutakuwa na tatizo au tuzo ima wanakotoka au wanakowenda. Si bure! Viongozi wa CCM na CHADEMA wamulike vyema kabla ya kufungwa kwa dirisha hili la usajili ambao kwasasa halihitaji akili. Kutakuwa na jambo,na kuna mkono mtu nawaambia!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.