FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,792
- 5,374
hakuna mkamilifu, ni kweli amekosea! amekiri na amejaribu kumtafuta bila mafanikio. ina maana unaweza kumuacha mtu unayempenda kwasababu ya kitu ambacho KINAWEZA KUSIKILIZIKA NA KUREKEBISHIKA?
Unconditional kwenye uongo (au kukaa na fact muhimu siku zote)?
Kitu kama kuwa na ndoa kabla, watoto nk ni mambo ya msingi na yanahitaji kuwekwa sawa mwanzoni mwa uhusiano.....
cacico mie nimebakia nashangaa kauli yake ya it is over kuanzia leo unisahau jamani ..mmhhakuna mkamilifu, ni kweli amekosea! amekiri na amejaribu kumtafuta bila mafanikio. ina maana unaweza kumuacha mtu unayempenda kwasababu ya kitu ambacho KINAWEZA KUSIKILIZIKA NA KUREKEBISHIKA?
Kiukweli alitakiwa aseme mapema na awakutanishe na huyo Mtoto huenda jamaa angempenda na huyo mtoto baada ya kumuona ,na ingesaidia kuzoeana mapema kwani wangekuja kuishi nyumba moja mwisho wa siku kama Baba wa kambo japo ni ngumu.
Pia ni bora ukasema mapema ukamkosa mtu kabla hamjazoeana sana na kupendana sana kuliko kumficha ukaja ukaumia baadaye.
Kongosho, saa ingine najiogopa kwa kuona akili yangu inakaribia kufanana na yako, uwiii!
Yaani on the first date na mtoto ataongelewa na kupigiwa simu,kha! Amemkosea sana huyu kaka. Tatizo ni moja, hii ameisema siku chache kabla ya engagement, mengine atayasema a day before harusi ama? Akaanze upya aisee, keshalikoroga. Otherwise ampe kaka wa watu space akijisikia atarudi mwenyewe!
Please nisaidie Dada! .ni kauli ya Meggy hiyo Kwangu.
Jamani mie namsaidiaje huyu rafiki ?
M & N Wamekuwa wapenzi for more than 5 years sasa long distance na wakikutana kila mmoja ana hamu na mwenzie.
Dada yuko 29 yrs old
Kabla ya hapo Bidada aliwahi kuzaa mtoto wake ana miaka tisa na alikuwa anajipanga ni lini amwambie mwenzie.
Jamaa amekuja kutoka huko ovasizi na ilikuwa next jmos wafanye engagement tayari kwa mambo mengine.
Meggy jmos ya tarehe 09 akamuomba mchumba wake watoke out kwa maongezi.
Jamaaa kwa Furaha akaitikia wito..wakiwa wametawaliwa na vicheko vya upendo ndipo Meggy kavunja ukimya kwa kumwambia Mchumba wake
Kuwa ana mtoto wa miaka 9 na alingoja tu wapate muda mzuri ili amwambie.
Jamaa alinyanyuka kwa hasira na kusema Kwa nini hukunambia mapema ?
it is over between us..naomba urudi nyumbani na unisahau milele.
Baada ya hapo Kaenda kwa mchumba nyumba imefungwa..
Toka hapo Meggy anapiga simu hapokei ..
anatuma message hazijibiwi ni week ya pili sasa
kabaki analia tu hata ukiongea nae ni machozi yanabubujika tu.
Jamani akina kaka/baba afanye nini huyu dada maana amekuwa mgonjwa ghafla
Kina mama/dada mpeni mawazo huyu binti namuona kila siku anazidi kuchanganyikiwa..
Nawasilisha....!
Huwa nalikaba kwapani, mtoto mgongoni
Yaani yashakuwa kwenye rapu rapu aisee, nikioga nakayamua kama kanga
cacico..unautesa moyo wangu wewe!!! that man u call 'husband' is truly blessed...hakumpenda kwa dhati! upendo wa kweli hauoni, husikii, haukwazi, hautafakari! nina mfano mdogo, cousin yangu alikuwa engaged, then jamaa akaenda masomoni south africa! waliendelea kuwasiliana baada ya mwaka jamaa karudi, aliporudi tu akamwambia cousin kuwa NIMEATHIRIKA NA HIV, if u ar ok tuendelee, if u ar not lets quit and i will understand u!
my cousin hakumuacha, waliendelea, walifunga ndoa, she is still negative sijui wanafanyaje? na watoto wawili wapo negative, and once ukikaa nao, utajua realy what luv is! shemeji akiumwa, mkewe hulala naye agakhan na kumhudumia UNCONDITIONALLY! Na tupo kumpa support! that is luv jamani! KAMA MTU ULIMPENDA UTAMUACHA SABABU YA MTOTO TU?? HAINIINGII AKILINI!
@Mnana ushauri wa sasa unaompa baada ya tukio hili ni upi
Kwa mfano ni dada ,mdogo wako au rafiki yako?
Kijana hawezi kurudi kamwe, Unajua inauma sana kuja kukutana na mme mwenzako ambaye amekutangulia kufanya kile ambacho wewe unakilingia kukifanya hivi karibuni na huyo mpenzi wako, hapa ni karahaa tupu. Kama mwanaume ni mwenye umri kidogo kama miaka 39, 40 au 45 na kuendelea huyo atarudisha mawazo nyuma lakini kama ni kijana wa umri wa miaka kuanzia 25, 30 mpaka 35 atajiuliza kwa nini achukue 'overused?'
hakuna mkamilifu, ni kweli amekosea! amekiri na amejaribu kumtafuta bila mafanikio. ina maana unaweza kumuacha mtu unayempenda kwasababu ya kitu ambacho KINAWEZA KUSIKILIZIKA NA KUREKEBISHIKA?
Hapa mapenzi wala hayahusiki mpendwa manake kama ni kuunga mdada ndie ambae kayaunga vibaya, inawezekanaje akae na jambo zito kama hilo mda wote huo? Mkaka wa watu kaogopa labda huko aliko anajiulza atakuwa kafichwa siri ngapi?Mapenzi ya siku hizi mbona ya kuunga unga na gundi?:A S confused: