Kwanini Hayati Magufuli hapoi?

Kwanini Hayati Magufuli hapoi?

music mimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2013
Posts
500
Reaction score
888
Wataalam wa siasa mnisaidie kunielewesha. Kwanini kila kona ya nchi mtu anayeongelewa sana kwenye mijadala ni Magufuli?

Mwanzoni nilijua ni ishu temporary kutokana amekufa akiwa madarakani, ila kila kukicha ni kama moto unaotambaa kwenye nyasi kavu zilizotandazwa.

Of course kuna upande unamsifu sana na kuna upande unamsema vibaya sana.

Swali langu kwa nini yeye na kuna wastaafu wengi tu na walifanya mambo mengi (mabaya na mazuri)?

Maana nnaona dalili ya kizazi cha sasa awa waliozaliwa kuanzia 1997 hapo kuendelea wanaanza kumtumia kama reference as tulivyofanya sisi watu wazima kwa Nyerere.
 
Tafakari jambo hili; ibada inaweza kuanza hadi kumalizika bila mtakatifu au malaika kutajwa. Ila yule haachi kutajwa hata kama ni ibada ya dakika tano! Ukilielewa hili hutahoji tena vitu vilivyo wazi.
 
Utendaji mbovu sana wa aliyepokea kijiti ndio sababu ya kutajwa kwake sana.

Chama chake kimekuwa cha hovyo zaidi hasa kwa upande wa uchumi na utawala bora kiasi cha viongozi wake wanaweza kukosa majibu ya maana kwenye dhiki za raia na kuwajibu waende Burundi na hakiwakemei. Ni kama vile chama kimejaa MAZOBA

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
FB_IMG_1656522799766.jpg
 
Ukiwatoa Nyerere, Mkapa na Magufuli waliobaki walikuwa wanafilisi nchi. Sasa wakumbukwe kwa lipi?
Kwa ndani kabisa, haya mambo ya Ukatoliki na Uislam tunashindwa kuwa na common say towards viongozi wetu. Wametugawa nasi tukawezekana. #UdiniUkristoVsUislam. Viongozi wote have got both strengths and weaknesses
 
Wataalam wa siasa mnisaidie kunielewesha. Kwa nini kila kona ya nchi mtu anayeongelewa sana kwenye mijadala ni Magufuli?

Mwanzoni nilijua ni ishu temporary kutokana amekufa akiwa madarakani, ila kila kukicha ni kama moto unaotambaa kwenye nyasi kavu zilizotandazwa.

Of course kuna upande unamsifu sana na kuna upande unamsema vibaya sana.

Swali langu kwa nini yeye na kuna wastaafu wengi tu na walifanya mambo mengi (mabaya na mazuri)?

Maana nnaona dalili ya kizazi cha sasa awa waliozaliwa kuanzia 1997 hapo kuendelea wanaanza kumtumia kama reference as tulivyofanya sisi watu wazima kwa Nyerere.
kwasababu aliua na kutesa wapinzani wake.
alipora korosho za wakulima huko kusini akitumia JWTZ
Alijenga uwanja wa ndege kijijini kwao bila kufuata sheria za manunuzi wala kupitishwa na bunge (kinyume kabisa na katiba na sheria)
Alinunua ndege bila kufuata hayo nliyosema hapo juu
aLIKAA Ikulu miaka 5 bila kupandisha madaraja wala mishahara kwa watumishi wa umma
Yupo wapi ben sanane? Anzory Gwanda na Alphonso mawazo? waliwafanya nini watu hawa?
Nani alimminia TUNDU LISU Marisasi yale pale Dodoma mchana ule wa jua kali ? upo wapi upelelezi wa sjauri lile la kinyama kabisa?
 
Back
Top Bottom