Hawa kuku ni wakubwa na wanaafya lakini hawatagi. Naombeni msaada wakuu.
hahahahahaha dah JF is never boring. Dah mkuu umenichekesha sana, ila ujue huyu jamaa ana shida kweli halafu wewe unazingua !!!Mkuu pengine lishe unayowapa haikidhi ushawishi wa wao kutaga!
Jitahidi uwachanganyie na lishe ya vifaranga ili waridhike kwamba hata wakitaga uhakika wa msosi wa vifaranga upo!
Kuku kuto kutaga kunasababiswa na mambo mengi sana.
1. Kulishwa chakula hafifu, hapa ni kama kuku wanafungiwa ndani muda wote,
2. Kupewa chakula kingi sana kupita kiasi- Hapa kuku hunenepa na kushindwa kutaga au chakula chenye kiwango kikubwa sana cha protein.
3. Aina ya breeds kuna breeds huchukua hadi miezi 7 ndo zianze kutaga.
4. Wakati- Unaweza kuta kuku wako wamefikia kipindi cha kutaga wakati wa baridi hivyo wanaweza wasitage hadi kipindi cha joto.
5. Vitu kama utitiri, viroboto na vitu kama wanyama vinaweza watia hofu wakachelewa kutaga.
6. Kama unawafuga nje unaweza kuta walisha anza kutaga bila wewe kujua na wanatagia kwenye machaka kuna kuku wanaweza taga hadi wakaatamia na kutotoa bila wewe kujua.
Mkuu nimekupata vizuri. Kwanza hawa kuku ni chotara muda mwingi wapo ndani mara chache sana wamekua wakitoka nje. Pili nipo machame huku kuna baridi kali hasa.
Jogoo wamekuwa wakubwa hadi hiyo ngozi ya juu inafunika jicho la upande mmoja.
Hawa kuku ni wakubwa na wanaafya lakini hawatagi. Naombeni msaada wakuu.
Ishu ya chakula na magonjwa ikoje katika banda lako?
Madawa nawapati. Banda ni zuri na hawajawah kuumwa mkuu.
Huyu Jogoo mbona hana sifa za Jogoo Bora?? jogoo bora huo upanga hautakiwi kulala..unatakiwa uwe wima, na pia umbo la jogoo wako ni dogo sana japo anaonekana amekomaa jogoo Bora anatakiwa kuwa kuwa na umbile kubwa!!....tafuta mbegu nzuri ya JogooMkuu nimekupata vizuri. Kwanza hawa kuku ni chotara muda mwingi wapo ndani mara chache sana wamekua wakitoka nje. Pili nipo machame huku kuna baridi kali hasa.
Jogoo wamekuwa wakubwa hadi hiyo ngozi ya juu inafunika jicho la upande mmoja.