Kwanini hakuna Zoo ya kufuga Nyati?

Kwanini hakuna Zoo ya kufuga Nyati?

Ukiona tu pua ilivyo na pembeni zake hutatamani kumfuga. Akikufukuza ujifanye unapanda kwenye mtu, mwamba anakojolea mkia wake na anakurushia mkojo ukiwa juu ya mtu. Mkojo unavyowasha utadondoka nae atakumaliza. Ni WA kufuga??
Usichanganye nyati na faru
 
Watu wamekariri simba simba simba.

Kipori pori simba ni paka mkubwa tu,kula yake ni ya shida na shuruba nyingi,tofauti na anvyoonekana ni mnyama asiyejiamini kabisa,ndio maana unaweza mkimbiza na akakimbia,usijefanya hii kwa chui ama nyati usijaribu kabisa wala kuwaza.

Ujasiri wa chui angekuwa na umbo kubwa kama la simba,hakuna mnyama angemsumbua.
Simba sio poa Mungu mwenyewe anajiita SIMBA WA YUDA sio Chui wala nyati wa yuda

Nyati mda wote wamekasirika tu, ushamuona simba mwenye hasira?
 
Nyati Wanaulinzi mkali sana katika kundi lao, wanavyeo pia, wapo makamanda hao wakiona kitu wanakuja Kwa kasi alafu wanasimama kucheki Hali ikoje. Alafu wanageuka kuashiria wenzao warudi nyuma. Baada ya kurudi nyuma wanatengeneza herufi C na wanakuja Kwa kundi kubwa wakati makamanda wao ndio waongoza mashambulizi makali. Ndio maana Simba huwa wanatega mtego wa kuvizia na kinipanga haswa ili mmoja wa makamanda ajipeleke pekeyake na wanapambanae kwelikweli huku mmoja wa Simba anamlenga mdomoni ili kuziba asitoe sauti. Maana akitoa sauti ikasikika Kwa wenzake wanakuja kumsaidia. Pia nyati yeye anahasira muda wote. Ndio maana kunamsemo ukiona mtu amechukia na kuwa makali sana tunasema jamaa amekuwa mbogo balaa. Huyu hafai kugugwa. Kunamatukio kadhaa Kwa watu wenye ranch kama Philips ilinga wanafuga hao ila aliwahi uwa mchungaji. Pia ASAS Iringa amecross nyati na ng'ombe, ukiona hizo specie iliyopatikana hapo hutamani kuona marambili Kama nimuoga, ila ni wapole sana wanachungwa kama ng'ombe tu maana makali yamepungua. Mwisho NYATI NI KIUMBE HATARI NA KATIRI SANA"
 
Watu wamekariri simba simba simba.

Kipori pori simba ni paka mkubwa tu,kula yake ni ya shida na shuruba nyingi,tofauti na anvyoonekana ni mnyama asiyejiamini kabisa,ndio maana unaweza mkimbiza na akakimbia,usijefanya hii kwa chui ama nyati usijaribu kabisa wala kuwaza.

Ujasiri wa chui angekuwa na umbo kubwa kama la simba,hakuna mnyama angemsumbua.
chui ni hatari, huyu sio wa kumfanyia masihara kabisa kabisa.. ukitaka kujua kwamba hanaga muda wa mazoea
1. hawaishi kwa makundi, labda mama akiwa analea watoto
2. mating yao ni for the purpose ( yaani jike na dume wanakutana kwa ajili ya uzalishaji tu) so kunamfanya awe ni kiumbe ambacho muda wote awe mawindoni
3. hali chini ( hula juu ya mti, anapanda na kitoweo juu ya mti), ni nadra sana kumkuta anakula chini
hana mazoea ya hovyo
 
Nyati ukimkuta kajitenga peke yake porini usimkaribie ni hatari zaidi ya hatari tofauti akiwa katika kundi pamoja na wenzake.

Wanayama wawili porini ambao muda wote wao wana hasira ni Kifaru (faru) na Nyati.

Hatari yao kubwa ni pembe zao zilizochongoka ila mbaya zaidi ni kifaru na wanakimbia balaa
uzuri wa faru ni kwamba hayupo vizuri kwenye ku sight (kuona) isipokuwa anafuata harufu, hivyo ni mzuri sana wa kujua na kufuata harufu na ndio maana sehemu yenye faru huwa watu wanaenda against na upepo... huyu nae dakika mbili tu anakupeleka ahera
 
Mwenye picha inayoonyesha mtu anacheza na Nyati kama huyu mtu anavyocheza na simba aweke hapa.
FB_IMG_1681378463737.jpg
FB_IMG_1681378463737.jpg
 

Attachments

  • FB_IMG_1681378459424.jpg
    FB_IMG_1681378459424.jpg
    80.9 KB · Views: 9
India Nyati wanafugwa kama ng'ombe tu na wafugaji wa kawaida tu vijijiji na huwatumia kulima mashambani na kukokota mikokoteni ya mizigo

Waweza pishana nao kibao wakichungwa na kijana mdogo tu kupelekwa malishoni

India hata tembo wanafugwa majumbani vijijini na hutumika kwa kazi mbalimbali za kilimo na kubeba mizigo na hata kuwatumia kama punda .mtu anapanda tembo anaenda aendako
Unachanganya Nyati na Ng'ombe maji sijui takataka gani! Ila Mzee wa Ngwasuma hafugiki! Ile ngoma acha tu, kidogo initoe roho Lake Manyara..hakuna mdudu mkorofi, jeuri kama yeye! Wewe usipomuona sio issue yake ye anakuwinda! Unaweza kukaa umetulia kumbe anakulia timing, mnyama mnduku sana huyo!

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani kutunza jamaa yako ni kazi kweli kweli kiasi cha kuweza kutumia kuliko anachoweza kuzalisha. Si huyo tu. Iko wapi zoo ya twiga, tembo au fisi?
Umelinganisha mambo pasipo ulinganifu. Tofauti na hao uliowataja nyati mahitaji yake hayatofautiani na ng'ombe.
 
Hapo predator kama simba ambao ndio adui wao mkuu,wakimkuta hivi wanakosa hata pa kuanzia na wakijifanya kulianzisha watakula kwanza tope hadi liishe hilo ,ndio vingine vifuate🙌
Screenshot_20230413-204448.jpg
 
Hapo predator kama simba ambao ndio adui wao mkuu,wakimkuta hivi wanakosa hata pa kuanzia na wakijifanya kulianzisha watakula kwanza tope hadi liishe hilo ,ndio vingine vifuateView attachment 2586814
Huyu mungu alijua kumkomesha hizo pembe zingikuwa zimechongeka kuangalia mbele yaani simba wangekuwa wanakufa sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom