Nyati ( mbogo) , Huyu wenyewe maofisa wanyama pori wanamuita FIELD FORCE, wanyama wengine wote , wakichachamaa na kuvamia maeneo ya WANANCHI kuwaswaga kuwarudisha porini ni rahisi tu.
Lkn miamba hii NYATI (MBOGO) msamiati wa kurudi nyuma wao HAWANA. ni mapambano kwenda mbele, jamaa alinisimulia kuwa waliwakamata MAJANGILI wakiwa wametega mtego na tayari NYATI kanasa!!.
Wale maofisa wa wanyamapori wakawapa MAJANGILI sharti la kuwaachia ni wao MAJANGILI waende wakautegue ule mtego ili NYATI anasuke.
MAJANGILI wakagoma katakata wakasema sharti hilo ni bora tu , wawapeleke kwenye mkono wa sheria. Lkn kwenda kumnasua NYATI akiwa HAI hawawezi kuthubutu.