Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,446
WAKATI Siku ya Wapendanao — February 14 mwaka huu — inakaribia, staa wa filamu, Elizabeth Michael Lulu, amekuja na jambo jipya; anauza nguo zake na viatu ambapo pesa atakayoipata itakwenda kusaidia wenye uhitaji katika jamii.
Lulu amethibitisha hayo katika akaunti yake ya Instagram ambapo amekuja na kitu hicho alichokipa jina la “Save My Valentine”.
“Wakati Wengine Tumepata Fursa Ya Kuwa Na Furaha Kwa Vile Tulivyonavyo Kuna Baadhi Ya Wenzetu Wamekosa Nafasi Hiyo….. Na HUU NI MPANGO WA MUNGU, Kuelekea Siku Ya Wapendanao Februari 14,Nimeamua Kuuza Sehemu Ya Nguo Zangu Ambazo Yawezekana Umeshawahi Kuziona au Haujaziona.
Na Pesa Yote Itakayopatikana Kupitia Mauzo Haya Itaenda Kusaidia Vitu/Watu Wenye Uhitaji Katika Jamii.
Please Join me to Save My Valentine.
#Savemyvalentine”Ameandika Lulu
Post mbili za stori alizoweka kwenye mtandao wake wa instagram: