Kwa jinsi hali ya Ufisadi ilivyoshamiri tangu Raisi Kikwete aingie madarakani hastahili tena kuliongoza taifa hili. Kujiuzuru na kufukuzwa kwa watendaji peke yake haitoshi. Kama Bunge halina uwezo wa kujadili masuala yaliyopo mahakamani kwa nini wasitumie nguvu yao kisheria ya bunge kupiga kura ya no confidence kwa Raisi. Raisi anaonekana ameshindwa kuongoza nchi na ile kauli yake aliyosema kuwa amechoka italigharimu sana taifa kama tukisema tusubirie mpaka muda wake uishe.