Hoja yako nambari 1 iko poa sana.Movie za Tanzania naona zinakosa yafuatayo
1. Uhalisia wa kimazingira.
Hiki ni kivutio kikubwa kama kweli tunataka kupanua soko letu lifikie duniani kote.
Afrika tunafahamika kwa utajiri wa maliasili (Mbuga na wanyamapori) hivi havionekani kwenye movie zetu.
Waafrika tuna ujenzi wetu wa asili (Nyumba za tembe etc) pia hivi havionekani tunaonesha maghorofa tu
Magari tunayotumia (Tunayoita ni ya kifahari) ni models za 2012 tukijitahidi sana, huko duniani wanaonesha za 2017 na zingine wanatabiri futurr
Mavazi waafrika tuna yetu ila daily tunajaribu kuonesha ya kwao ambayo ni provocative lkini sisi tunavaa kujishtukia, kama tumeamua tuende all the way kama wao au tubaki na yetu ya asili ambayo ni mazuri zaidi na kivutio duniani
2. Uhalisia wa kiugizaji
Tunajaribu kuigiza maigizo, msanii anaigiza kuwa anaigiza hawavai uhalisia
3. Maisha binafsi ya wasanii nje ya kamera ni hovyo hovyo tu. Postings zao za Social Media ni upupu ukiangalia maandishi katika Captions zao. Wako vizuri kwenye Ubuyu na kusutana. Wanajitahidi kwenye matusi zaidi
4. Masoko
5. Vifaa
Kweli mkuu umenifumbua macho,nilikuwa naona johari anahesabu sielewi ...kumbeeeeenasikia mkuu wa mkoa wa dar ameahidi kurudisha soko lao kwa kufungia uuzwaji wa movie za nje!!!
zimebaki siku ngapi sijui, wenyewe walikuwa wanahesabu huko insta!