Kwani ukiwa na degree lazima upewe ajira? Acheni ujinga ninyi wasomi, ajira za kupewa hakuna duniani kote. Nendeni mashambani mkajiajiri kwa kulima.
Lengo kuu la serikali kuwasomesha/kuwapa elimu wanainchi wake ni kuhakikisha kwamba kupitia wanainchi hao walioelimika tunapata taifa imara wakitumia taaluma zao ipasavyo katika nyanja mbali mbali.
Na katika kutimiza hilo serikali ndio inayotoa muongozo kwa kuunda sera mbali mbali ambazo zinatekelezwa kwa mtindo wa mgawanyo wa kimajukumu. Na wakufanya majukumu hayo ni hao hao wanainchi, hivyo basi kumbe serikali inatengeneza wasomi hili ije iwaajiri hapo baadae.
Sasa labda nikuulize wewe, unaposema kwamba ajira za kupewa hakuna na hizo ajenda/sera/majukumu zinatekelezwaje na wanazitekeleza wakina nani?
Huko mashambani unapokusema ndio watu wanaenda tu hivi hivi hata kama hawana A wala B kama starting point ya kujiajiri? na kwanza kuna haja gani ya mtu kusoma sheria kwa miaka 18 halafu leo hii aende akajiajiri shambani ambako hakuna uhusiano wowote na taaluma yake ya sheria?
Nina binadamu zangu wawili mmoja ana shahada ya political science na mwingine ya Public administration, hawa wote hawana ajira. Sasa je, na wao wakajiajiri huko mashambani unakosema wakitumia hizo taaluma zao?
Kwanza sehemu zingine za huko duniani unafahamu kwamba wana sera nzuri za kiuchumi kuliko sisi na zinafanya kazi ipasavyo lakini bado serikali inalaumiwa kwa wanainchi kukosa kazi na inakubali lawama? yaani mpaka wameamua kuja na program mbadala wa kutatua tatizo la ajira, unafahamu kitu kinachoitwa working claims?
Serikali haiweze kukuepuka hili suala la unemployment linalokuwa kwa kasi, wao ndio wahusika namba moja wa kubeba lawama.
Imeshindwa kuandaa mazingira/sera nzuri za kukabiliana na tatizo hili. Halafu kuna wapuuzi kama wewe mnakuja na kauli nyepesi za kutetea hovyo ineptness ya serikali yenu eboo!!
Binafsi nafikiri wewe ndio uachage ujinga kabisa! shwaini