Kwanini Adam.......?

Kwanini Adam.......?

hakuwa nyoka wa kawaida, alikuwa kiumbe mwenye akili kubwa, uwezo wa kuongea, na kwa hakika alikuwa na miguu ya kutembea wima kabla ya kulaaniwa
Ni fiction story tu ndio maana hadi wengine wanaamini hata alikuwa tunda bali Hawa na Nyoka walifanya mapenzi (sex)
 
ulikuwa mpango wa M-ngu mwanadamu atende dhambi na aje amuokoe maana yeye anajua yote mpaka yajayo
Ni mpango wa mungu pia watu wateseke? Watu wazima na Watoto wateseke na wapate cancers, wafe kwa vita, ajali na njaa, wabakwe, walawitiwe n.k??
 
Ni mpango wa mungu pia watu wateseke? Watu wazima na Watoto wateseke na wapate cancers, wafe kwa vita, ajali na njaa, wabakwe, walawitiwe n.k??
watu kuteseka ni kwasababu ya dhambi zao, mazingira na ujinga wao, kufa kwa watu sababu ya njaa na n.k nikufanya watu wamtumaini yeye BINADAMU ANAPOKAMILIKA ANAJISAHAU
 
Kwanini Hawa, alipodanganywa na kula tunda la mti wa katikati.
hakugunduwa kuwa yuko uchi? mpaka alipokula na Adam...?
Je... nini kingetokea kama Adam asingekula¡
Hawa lile hakuwa kwenye agano na Mungu, aliyekuwa amepewa dhamana alikuwa ni Adam, Adam alikuwa na jukumu la kumkanya na kumuongoza mkewe kwa hiyo yeye alikuwa kwenye hatia zaidi

Rejea 1samwel 3:1........... Utaona Elly anakutana na adhabu kwa sababu ya uovu wa watoto wake, maana hakusimama na kuwakanya juu ya tabia zao mbaya
 
Za kuambiwa changanya na za kwako... Hakuna tunda lolote la mti wa kati walilokula...
Walifikia balehe, waka.to.mb.ana wakaujua utamu basi...


Cc: Mahondaw
 
Mungu mwenye Agano na Adam, Kwa nini aruhusu Adamu adanganywe na Hawa?

Au ilikuwa plan ya huyo Mungu kwamba Adam adanganyike?
Binadamu ni kiumbe aliyependelewa na Mungu kuliko hata Malaika, ni Binadamu tu ndiyo Mungu hutuita Watoto wake, Malaika akiwaita Messengers.

Na kama Kuna Zawadi ya Thamani ambayo Mungu alitupa Binadamu na hakumpa kiumbe mwingine yoyote basi ni (Free will), ni Will ambayo imebebwa na Soul, ambapo pia Kuna Emotion na Mind, Malaika hawako na Soul ila wako na Spirit tu, means hawana Hisia, Hawawezi kupenda wala kuchukua, Hawawezi kuwa huru kwenda wanapotaka ama kufanya wanachotaka, ila Binadamu yupo huru.

Sasa Mungu hakutaka kumfanya Binadamu kuwa kama Malaika Kwa kumnyima Uhuru, alimpa Uhuru kuchagua jema na baya, alimpa Uhuru Binadamu aamue kumpenda Mungu ana kutompenda,

Mungu hakuruhusu Shetani amdaganye Hawa, Wala hakuruhusu Hawa amshawishi Adam, ila aliwapa Binadamu Uhuru wa kuchagua, nao wakachagua kumuasi.....! Kama Adam na Hawa wasingeasi, Yesu asingekuja, Mungu asingekua na haja ya kuanzisha Taifa la Israel kupitia Ibrahim.

Baada ya Adam kuasi ikamgharimu Mungu Tena kuja na Mpango kupitia Ibrahim, Mungu angekua Binadamu asingekubari mpango wake uharibike, ila mpaka Leo MUNGU HUWATAKA WALE WATAOMWABUDU KWA ROHO NA KWELI KWA HIYARI YAO,...! so wewe ndiyo utachagua, umfate Mungu ama Shetani, ukimfata Shetani yeye Hana Shida, ndiye Muumba wako na Bado anakupenda.
 
ndy wapo ila hawaishi duniani kuishi milele hapa hapa dunian hakuna maana utapoteza uwapendao wote unabaki peke yako unapata raha gan?
Kuna Uzima wa Milele baada ya kufa, Kwa maana ya Ufufuo na Watakatifu kuishi Milele.

Pia Kuna Uzima wa Milele wa kutokuonja Mauti Kwa baadhi ya Watu.

1 Wakorintho 15:51-54

51. Sikilizeni, nawaambia siri: sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa 52. ghafla, kufumba na kufumbua, tarumbeta ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa tarumbeta italia, wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa. 53. Kwa maana hali hii ya kuharibika lazima ivae kutokuharibika, na hali hii ya kufa lazima ivae hali ya kutokufa. 54. Kwa hiyo, wakati kuharibika kutakapovaa kutokuharibika, na mwili wa kufa utakapovaa hali ya kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia, “Kifo kimemezwa na ushindi .”

Ukiangalia kwenye Biblia hapo, Mtume Paul anazungumza kitachotokea, anasema Sote hatutalala, means sio wote watakufa, anasema itakua ni kitendo Cha kufumba na kufumbua, Watu watafufuliwa na Miili isiyoharibika NASI TUTABADIRISHWA (Wa kina nani) wale wataokuwa Hai Watabadirishwa, anasema Miili hii ya kuharibika itavaa kutoharibika, na itavaa kutokufa.

Hivyo Kwa Wale wataopata nafasi ya kuwepo hai Wakati Tarumbeta ya 7 ikipigwa, itabidi Miili Yao ibadirishwe, hawata kufa, ila Miili Yao itabadirishwa, na Biblia inasema itakua kitendo Cha haraka sawa na kufumba na kufumbua....!

Biblia inaeleza wazi kuwa sio wote watakufa, Wapo wataishi Milele bila kufa, Wataungana na Watakatifu wengine wataofufuliwa.

Kuna Uzima wa Milele wa kwanza na Kuna Uzima wa Milele wa pili, ni sawa na Kuna Ufufuo wa kwanza na Ufufuo wa pili.
 
Back
Top Bottom