Kwani haya mapenzi ni lazima??????

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,110
115,886
MPENZI WAKO ANA WIVU??KUZIDI HUYU??




Alikuja dada mmoja jana hapa ofisini kuongea kuhusu adha anayoipata katika maisha ya ndoa,akiwa na malalamiko kibao kuhusu WIVU wa mumewe?akasema amechoka jamani WIVU huu umezidi...Tulijua namna ya kumsaidia lakini leo alisikika kwenye hekaheka na Gea kama ushuhuda wake kwa jamii


HAYA NDIO BAADHI YA MAMBO YA WIVU ANAYOTENDEWA NA MUMEWE
1.Mwanaume akiondoka asubuhi anamuingiza vidole sehemu za siri ana mwambia hapa nimeacha hivi ole wako jioni nikirudi niikute tofauti.

2.Mwanaume ananusa chupi zake,anasema huwa ana kawaida ya kuloweka chupi zake siku hiyo akamkuta mwanaume bafuni ananusa chupi zake huku anasema mwanamke kazidi umalaya huyu.

3.Mgeni mwanaume akija nyumbani tena mgeni wa mume,bwana anafanya kuwaangalia machoni kama kuna dalili zozote za kukonyezana.

4.Kuna siku mwanaume anaaga anatoka baadae anarudi kwa kujificha halafu anajificha chini ya uvungu aone kama mkewe ataingiza mwanaume ndani.Baadae mwanamke anashangaa mwanaume anaibukia chini ya uvungu.

5.Haruhusiwi kuwa na marafiki wala kukaa kuongea na majirani.

6.Akitoka akirudi mume anamnusa mwili mzima kama anaharufu ya tofauti.

7.Anapigwa mpaka basi.

Hapa ndipo namkumbuka Aunty Sadaka aliwahi kusema kuna wakati tunachukulia poa mambo wanayoyafanya wapenzi wetu dhidi yetu na kuishia kusema "mpenzi wangu ana wivu" kumbe ana ku abuse kupita kiasi.Na inapofika point hii kunakuwa hakuna mapenzi tena ni hatua mbaya ambayo wote wawili kama bado mnapendana mnahitaji msaada kubwa wa kisaikolojia.Na kama mmoja kachoka hakuna la zaidi zaidi ya kutengana.
 
Kha! this is too much, huu si wivu bali ni unyanyasaji, anaingizwa vidole na si kwa mapenzi bali kupimwa anaona sawa? anapigwa anaona sawa?

Nimekosa ushauri huenda hata binti anamatatizo
 
Huyu mwanamme ana matatizo ya akili..kuna mmoja huwa anafagia uwanja wakati anatoka na kuondoa alama za miguu akirudi jioni na kukuta kuna miguu imepita itabidi wife atoe maelezo
 
Huyu mwanamme ana matatizo ya akili..kuna mmoja huwa anafagia uwanja wakati anatoka na kuondoa alama za miguu akirudi jioni na kukuta kuna miguu imepita itabidi wife atoe maelezo

Hee kweli FL? duniani kuna mambo so ina maana hakuna mtu kuja kwako? je nikifagia upya? kupenda kazi kweli
 
Lol hii imepitiliza sana tena sana sitamani kupata mume wa aina hii kama mambo yenyewe ndo hayo
 
Huo sio wivu ni unyanyasaji! Huwezi kluita wivu wakati mwenzake anateseka, wivu wa kweli ni ule wenye mapendo ndani yake.
 
Mh! Hapana. Kwani huyo mwanamke hana wazazi?
Si ajabu anaendelea kuvumilia hayo mateso kwa sababu za kiuchumi zaidi.
 
Kama maelezo haya yanaeleza tabia ya kweli mtu kuwa nayo kumfanyia mke wake basi huyu bwana ana matatizo ya akili. Hata mke anayeweza kuvumilia hali hii naye pia ana matatizo ya akili kuendelea kuvumilia maana ni dhahiri huyu bwana anaweza kukatiza maisha yake muda wowote. The boss chukua hatua ya kumshauri huyo mama aachane na huyu bwana kichaa.
 
Huu ni unyanyasaji wa hali ya juu... Kwani yeye mwanaume akiondoka anaweka kipimo gani? na akirudi anatumia kipimo gani kucheki kama ametumika au la? This is not acceptable...

Ila huyo dada naye ana walakini.... hata kama ni mapenzi, ikifikia hatua hii sio mapenzi tena ni matezi
 
4.Kuna siku mwanaume anaaga anatoka baadae anarudi kwa kujificha halafu anajificha chini ya uvungu aone kama mkewe ataingiza mwanaume ndani.Baadae mwanamke anashangaa mwanaume anaibukia chini ya uvungu.
Dah! Hii kali sana, lakini tujiulize kwanini huyu mwanaume anafanya haya? Ameanza tu from nowhere? au kuna sababu?
 
1.Mwanaume akiondoka asubuhi anamuingiza vidole sehemu za siri ana mwambia hapa nimeacha hivi ole wako jioni nikirudi niikute tofauti.
Sasa hapa anafanyaje jamani, anaingiza vidole gani? Na yeye anaamini hiki ni kipimo sahihi? Huyu mwanaume chizi kweli

6.Akitoka akirudi mume anamnusa mwili mzima kama anaharufu ya tofauti.
Kwa maana hiyo huyu mwanamke haogi mpaka mumewe harudi na huyu mwanamke hafanyi kazi ambayo inabadilisha harufu ya mwili wake kwa mfano kumpa joto? Mambo mengine tufikirie kama ni taarifa sahihi au ni kudanganyana tu hapa

7.Anapigwa mpaka basi.
hii kupigwa mpaka basi nayo imekaaje wajameni, inaingia kichwani? Manake huyu hana ndugu, wasimamizi wa harusi, wazazi, majirani? Manake kupigwa sana si jambo linalojificha

Nway haya mateso yapo lakini tuangalie ushahihi wake na uelewa wa yule anayefanyiwa, sasa huyu mwanamke yeye hasikii hii 50/50 TGNP na wenzake wanayolilia kila siku?

Asante mtoa mada na pole msababisha mada
 
wanajuana wenyewe, pengine alishaibiwa hadi akachoka, au anamjua mwanamke wake kuwa ana udhaifu wa kudanganyika kirahisi, analegeza macho kwa kila mtu etc...wanajuana weneyewe, tusijaji bila kuangalia upande mwengine wa shilingi....wivu wa aina hiyo generally si mzuri, ila hatujui ni kwanini jamaa anafanya hivyo, labda kuna sababu...hatuwezi jua....kama hamna sababu, basi mwanaume anahitaji kueleweshwa tu au labda ana pepo uyo...
 
Huyu jamaa hamuamini mwenzake, kwa hiyo hamna ndoa hapo ni ubabaishaji tu, huwezi pima uaminifu wa mwenzako namna hiyo, acha kabisa!!!!!!
 
Sasa huu si wivu wala mapenzi, kama vile haitoshi jamaa kamgeuza ngoma ya Segere kwa ngumi na mateke. Kinachofanyika hapo ni ubabe na unyanyasaji.

Upande wa pili wa shilingi, huwenda huyo bwn ameshamfuma mkewe na skendali za ngono, japo si sababu tosha ya kufanya hayo anayoyafanya. Kama ndo hivyo, mwanamke naye abadilike.

Hapo hakuna ndoa, imezidi ndoano. Namshauri aachane na huyo bwn, agange kivyake, akibahatika kupata mwanaume mwenye staha aolewe, iwapo tatizo ni mume au abadilike mwenyewe kama ndo chanzo cha zogo.
 
Dah! Hii kali sana, lakini tujiulize kwanini huyu mwanaume anafanya haya? Ameanza tu from nowhere? au kuna sababu?

ni jambo muhimu hili ; Unaweza kukuta alitendwa kupitiliza na matokeo yake yakawa ndio haya!

Jamani nadhani apatikane huyo mume ajieleze; hii ni kutokana na na ukweli kuwa si tabia yake tangu amezaliwa; kila mtu ni kichaa na huwa kuna vitu vinavyotriger huu ukichaa!

Lazima kuna sababu!
 
Imenikumbusha leo nimlipokuwa nakuja kazini nikamuona mwanamke (around 50 yrs old) kasimama anasuburi taxi, it was around 8:00 AM the tempreture was almost 45c... I stopped the car and I told her I am heading to so and so place if she is going that direction I could just take her there... she agreed...

Alivyo kaa vizuri akaniuliza (Mama B is a typical Arab woman with a very strong Omani/arabic Accent )

MAMA B: wazee wako hawajambo?
NONAME: watakuwa hawajambo ( smile) mie nimeolewa siishi na wazee wangu
MAMA B: ooow samahani binti mie sikudhani kama umeolowa, huoneshi kama umeolewa, unaonesha bado mdogo...
NONAME: No problems (laughing)
MAMA B: unajuwa hata mie nikikaa na mdogo wangu watu wanadhani yeye mkubwa mie mdogo....
NONAME: Aha labda wewe unaraha zaidi ya mdogo wako (smiling)
MAMA B: Raha gani binti yangu... mme wangu anakula roho yangu...matusi anayonitukana kila siku hamna mtu aliwahi kutukanwa hivyo... nikitoka kidogo nikarudi ana anza kunitukana.... eti ulikuwa wapi? ulikuwa na nani?
NONAME: offfffff anawivu eeh
MAMA B: Mie kwenye umri huu nataka nini? kwani nikitoka ntaenda wapi? lakini kwa maneno na matusi yake mie sikuhizi na mwambia MIE NTATOKA na ntaenda kulala na mwanaume yoyote ili nikukomeshe...samahani Binti lakini huyu mwanaume kanichosha Duh!
NONAME: hahhhahha u will do that?


Anyway tukawa tumefika, akanishukuru na mie nikaondoka... But u know I was already in love with that old lady lolllll I liked her spirit... I wouldnt think that kind of woman will even dare to think that way>


wivu mwengine ni Maradhi....
 
Dah! Hii kali sana, lakini tujiulize kwanini huyu mwanaume anafanya haya? Ameanza tu from nowhere? au kuna sababu?

Kuna sababu inayoweza kujustify ukatili wa kiasi hiki?with or without sababu,bado hatua anazochukua hazifai na ni unyanyasaji mkubwa.
 
Jamani nadhani apatikane huyo mume ajieleze;
Na mimi naamini ndio njia pekee ya kuwasaidia wanawake wanaonyanyaswa na waume zao ni kwa kutambua tabia za waume zao na kutafuta mbinu za kuzirekebishaa lakini kushutumu na kutanga divorce it wont help
 
Kuna sababu inayoweza kujustify ukatili wa kiasi hiki?
Ni kweli hakuna lakini tukiishia kushutumu na kulaani tutamsaidia huyu mwanamama? Basi tutafute source kwa mtoa mada ambaye alishamshauri huyo mwanamama hapo kabla kwenda kuongea na huyo mwanamume kwani i hope mtoa mada atakuwa mwanasaikolojia/mwanadini/mwanaustawi wa jamii na ndiyo maana huyo mwanamama akaenda hapo kutafuta usaidizi
 
Back
Top Bottom