hannibali
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 468
- 427
Habari za muda huu!
Juzi nimehudhuria harusi kuna watu waliamua kufunga ndoa na ilikuwa ndoa ya Kiislam.
Sasa pale ukumbini ilipigwa sala kabisa na mashekhe walipiga visomo kadhaa, mashekhe muda wote walikuwa wanapiga marufuku na kulaani unywaji wowote wa kilevi, cha ajabu baada ya dua, watu wakaingia na mapombe yao toka nje! Acha watu wagambike sasa! Mavurugu kama yote.
Sasa nilijiuliza hotuba yote ile ya mashekhe wale lakini watu walishindwa kuacha lipite wakagambika kisawasawa, matokeo yake wale mashekhe waliondoka bila kuaga na kupelekea lawama mzito kwa wahusika.
Jamani eeeh ndoa ni tendo takatifu, sio vizuri kuichanganya na ulevi ambapo shetani ndio leader hasahasa mkiwa mmekatazwa matokeo yake munaharibu ndoa za watu.
Juzi nimehudhuria harusi kuna watu waliamua kufunga ndoa na ilikuwa ndoa ya Kiislam.
Sasa pale ukumbini ilipigwa sala kabisa na mashekhe walipiga visomo kadhaa, mashekhe muda wote walikuwa wanapiga marufuku na kulaani unywaji wowote wa kilevi, cha ajabu baada ya dua, watu wakaingia na mapombe yao toka nje! Acha watu wagambike sasa! Mavurugu kama yote.
Sasa nilijiuliza hotuba yote ile ya mashekhe wale lakini watu walishindwa kuacha lipite wakagambika kisawasawa, matokeo yake wale mashekhe waliondoka bila kuaga na kupelekea lawama mzito kwa wahusika.
Jamani eeeh ndoa ni tendo takatifu, sio vizuri kuichanganya na ulevi ambapo shetani ndio leader hasahasa mkiwa mmekatazwa matokeo yake munaharibu ndoa za watu.