Kwako Yatima Anna Zambi (16)

Kwako Yatima Anna Zambi (16)

Liverpool_Jr

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2019
Posts
1,220
Reaction score
1,417
Naitwa Mr. Liverpool A.K.A Kop mimi ni yatima kama wewe niliyepitia shida nyingi.

Kwanza kabisa nilizaliwa 1989 na wazazi Matajiri sana. Baba alikuwa mfanyabiashara mkubwa sana na mama alikuwa ni mama wa nyumbani.

Maisha nyumbani yalikuwa mazuri sana, yenye raha na ndugu walikuwa kibao kila mtu kuja kulia shida kwa baba.

Baba alipata stroke 1998 na kufariki ghafla, mama alikuwa mama wa nyumbani asiyejua kuendesha vitu vingi vya baba, maana alihakikishiwa maisha mazuri na mumewe, then alikaa tu nyumbani kuhudumiwa.

Mali nyingi za baba zilitapeliwa na rafiki pamoja na ndugu waliokuwa wakilia shida kwa mama na baba.

Ghafla maisha ya nyumbani yakaanza kuwa magumu. Shule nikahamishwa kutoka English medium mpaka kayumba (hela ziliisha zote mpaka za ada).

Kwa kuchanganyika, mama akaanza kuumwa sana. Nikawa namuombea sana na kila mara kuongea na Mungu asimchukue mama. Ghafla mama alizidiwa akafa.

Aisee kile kifo kiliniuma sana. Nikaanza kumlalalamikia sana Mungu: "Baba akiwa anaumwa nilikuomba sana apone ila ukamchukua, mama naye nimekulilia sana naye kafa, kweli wewe Mungu upo?"

Kujibu hili swali ziliruhusiwa shida hatari.
Kula kwa siku mara mbili. Ukienda kwa ndugu wanakuona unaenda kulia shida, "We kila siku unakuja kuomba hela kwetu, hakuna ndugu wengine?"

Nilikuwa nikienda kuomba hela za tuition na mitihani ya kujipima na mahitaji ya shule. 2001 nilijiapiza "sitomlilia ndugu yeyote shida, nakomaa nazo mpaka ziniue"

Nimekulia maisha ya shida ya kukondaa balaa. Ya kukosa hata 50 ya nauli ya kupanda daladala kwenda shule.

Nikiwa form one nilijiapiza "Elimu ndiyo mkombozi wangu, nitasoma sana"
Nilisoma balaa kwa njaa na ugonjwa (nilishawahi kwenda shule kichwa kinauma mpaka mzee mmoja njiani alishtukia!)

Nilijiepusha na bangi, unga, sigara, pombe na vyote (maana mitaa niliyokulia hivi vitu ni kawaida sana, vijana na watoto wengi waliharibika na miongoni mwao ni wenzangu).

Kwa msaada wa shangazi na wazazi wa rafiki zangu, maisha yakaenda, Form 4 ikaisha, mara Advance, mara chuo.

Kutoka tu chuo nikaajiriwa. Ashukuriwe Mungu sasa nimejiajiri.

Walewale ndugu kila mara wanapiga simu kuomba msaada. Huwa nasomaga SMS zao na kuzitupa kwenye dustbin.

Huwa nasaidia walionisaidia tu.

Kuna ndugu mmoja nikiwa form 2 nilishawahi kumwambia, "Ukinisaidia Mimi unakuwa unawekeza". Na kweli, amefariki na mimi ndio nasaidia familia yake aliyoiacha.

Kilekile kidogo alichonipa (kuninunulia vitabu form 2 tena viwili) basi narudisha kikubwa kwa familia yake.

Japo huwa najitahidi kuwasaidia walionifungia milango nilipoenda kuwaeleza shida zangu tena nikiwa mtoto, ila wengii nawafungia vioo (Mungu anisamehe kwa hili).

Baada ya vifo vya wazazi...

1.Nilimlalamikia sana Mungu.
2. Niliwaandikia sana barua wazazi wangu na kuziweka kwenye kabati la nguo zao (sijui kama walikuwa wanazisoma).
3. Nilishindwa kwenda kwa rafiki zangu, maana nikifika na kuwaona vile wanaishi kifamilia, niliishia kulia tu.

Nachotaka kukwambia:

1. Wale wale waliojifanya wapo karibu na familia yenu, watakukimbia.
2. Wale wale waliokua wakikupenda, ndio watakao kudhulumu.
3. Wale wale waliokua wakileta shida zao kwa Mzee Zambi, ndiyo watakao kimbia shida zako.

Jipe moyo mama. Pambana.

Mungu yupo na YUPO KWELI.

Japo ukiniuliza mpaka leo "Kwanini Mungu hakusikia maombi yangu asichukue wazazi wangu?" Jibu SINA.

Nachojua Mungu yupo na ananipenda na alinipigania sana.

Usikate tamaa Mungu yupo.

Maisha ya uyatima NYOKOO SANA..!!

#ASANTE
#YNWA
 
And do not come near the wealth of the orphan - unless intending to enhance it - until they attain maturity. Give full measure nd weigh with justice. We never require of any soul more than what it can afford. Whenever u speak, maintain justice - even regarding a close relative.."
From holly qur an
 
Aende kwa Zamaradi Mketema, yule dada tajiri; amejitolea kumtunza kama atakuwa tayari. Yule ataishi naye kwa dhati kwakuwa sio ndugu yake, hana maslahi naye, ndugu zake wanamjali sasa hivi watamchoka baadae. Pia, watawinda mabaki ya mali za marehemu: nyumba, gari, biashara n.k. Akiwa kwa Zamaradi atasaidiwa kuhusu mirathi bila longolongo.

Akiwa kwa Zamaradi atakuwa na ataendelea kupata elimu kwa mfumo wa shule ambazo wazazi wake waliuanzisha huo wa kusoma shule bora za private n.k

Kwa sasa kwa hali aliyonayo huyo mtoto hakuna neno lolote la faraja na ushauri litakalomfaa, moyo wake sio tu umevinjika, umesagika kabisa, inahitaji muda kurudi katika hali yake.

Nasisitiza, aende kwa Zamaradi, ndugu baadae watamchoka, watamuona wa kawaida, safari yake ya elimu ikawa ngumu.
 
Liverpool_Jr,
Mkuu pole sana kwa yote uliyoyapitia na pia hongera kwa mafanikio uliyonayo kwa sasa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkuu. Haijalishi hao waliokutupa pale ulipowalilia shida kipindi hicho ni kwa namna gani walikuumiza.

Mkuu ombi langu kwako usilipe baya kwa baya, hakika ukiwasamehe tegemea baraka za Mungu kukushukia jumla jumla.


KTBFFH [emoji108][emoji108][emoji108]
 
Pole kwa uliyopitia Mkuu. Kisa chako kinafanana sana cha rafiki yangu mmoja, Mungu aliwabarikiwa sana kwa miaka ile walikuwa matajiri sana katika mkoa X.

Baba yake alikuwa ni mtu mwenye kampuni kubwa sana, mbaya zaidi huyu rafiki yangu hakubahatika kumfahamu Mama yake mzazi maana alifariki na kumuacha akiwa mdogo sana.

Mzee wake alipata ugonjwa wa stroke pia aliugua kwa muda mrefu ila mwisho wa siku alifariki.

Kabla ya kufariki, huyo mzee hakuwa na mtu wa kumuamini tofouti na mdogo wake hivyo mali zote aliziacha chini ya uangalizi wa mdogo alipofariki tu yule mdogo mtu hata ushirikiano katika mazishi ya kaka mtu ulikuwa wa kusuasua.

Kufupisha story ni kwamba kaka mtu hakumjali tena yule kijana, na akawa akimuwinda ili ampoteze kabisa ili awe na amani na mali zile, kaka mtu alibadilisha umiliki wa kila kitu kikasoma jina lake hapa hata kumpeleka mahakamani inakuwa ngumu kidogo.

Kwa sasa kijana anapambana kivyake na Mungu kambariki na maisha yanamuendea vizuri tu.

Funzo kwetu wanaume, tujitahidi sana kuwashirikisha wake zetu katika biashara zetu hata ikitokea siku moja mmoja wetu akafariki basi mwanamke ataziedeleza biashara na watoto watakuwa salama.

Kuna wanawake wengi sana wamedhulumiwa mali za waume zao kwa kyshindwa kutambua mali halisi za mme wake hivyo kupelekea watu wengine ikiwemo ndugu na marafiki kufaidi jasho lao huku wao wakiwa na maisha ya mateso makubwa na dhiki.

Niwatakie Jumapili njema yenye baraka ndani yake.
 
"KILIO HAKIKA KILIO"
Nilipoteza baba nikiwa na umri wa mwaka 1 na miezi 6😢😢😢

Mama naye akamfuata mumewe nikiwa na umri wa miaka 12😥😥😥

Tegemeo likabaki kwa mama mkubwa. Naye akafuata baada ya miezi 2 tu tangu kufariki mama😢😢😢

Mungu aliniachia bibi pekee kama mlezi wangu. Mungu ampumzishe kwa amani bibi yangu kipenzi kwa kuwa alijitahidi sana kunilea. Amefariki nikiwa na miaka 21.

Mungu alivyo wa ajabu hadi mke wangu nae alipoteza wazazi wote wawili akiwa na umri wa miaka 7 tu.😢😢😢

"KILIO HAKIKA KILIO"
 
IMG_20191117_100448.jpeg
 
Back
Top Bottom