Ncha Kali
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 14,501
- 27,001
Heshima yako Mzee wetu.
Sina shaka na busara zako, umelitumikia vema Taifa letu, na hata sasa umekuwa ukitumika kama mshauri.
Kitendo cha kutamani kugawa ‘nyongeza’ ya mhula wa utawala, kama zawadi kwa mtu fulani kisa ‘amekurejesha’ ikulu, ni ulevi wa madaraka kama sio kuchanganyikiwa.
Taifa linawategemea wazee kama nyie, kwa heshima kama washauri, hebu ona sasa mnavyoonesha ubinafsi hadharani!
Nchi sio mali yenu binafsi, ingawa mmekuwa mkijimilikisha siku zote. Yamekuwa yakisemwa mengi kuhusu ‘kugawa’ rasilimali za Taifa kwa maslahi binafsi, hili ni moja ya kuthibitisha ukweli wa yaliyosemwa.
Kwa heshima nawajibika kukukumbusha hili, usitoe ahadi ukiwa mwenye furaha sana. Bila shaka kwa sasa unajutia kauli yako iliyopingwa hadharani, kamzawadie kwa namna nyingine kakutendeeni makubwa sishangai.
Miaka mitano ya zawadi, kwa sababu hiyo tu.? Nchi ni yetu sote, nasi zamu yetu ifike.
Wasalaam,
Ncha Kali.
Sina shaka na busara zako, umelitumikia vema Taifa letu, na hata sasa umekuwa ukitumika kama mshauri.
Kitendo cha kutamani kugawa ‘nyongeza’ ya mhula wa utawala, kama zawadi kwa mtu fulani kisa ‘amekurejesha’ ikulu, ni ulevi wa madaraka kama sio kuchanganyikiwa.
Taifa linawategemea wazee kama nyie, kwa heshima kama washauri, hebu ona sasa mnavyoonesha ubinafsi hadharani!
Nchi sio mali yenu binafsi, ingawa mmekuwa mkijimilikisha siku zote. Yamekuwa yakisemwa mengi kuhusu ‘kugawa’ rasilimali za Taifa kwa maslahi binafsi, hili ni moja ya kuthibitisha ukweli wa yaliyosemwa.
Kwa heshima nawajibika kukukumbusha hili, usitoe ahadi ukiwa mwenye furaha sana. Bila shaka kwa sasa unajutia kauli yako iliyopingwa hadharani, kamzawadie kwa namna nyingine kakutendeeni makubwa sishangai.
Miaka mitano ya zawadi, kwa sababu hiyo tu.? Nchi ni yetu sote, nasi zamu yetu ifike.
Wasalaam,
Ncha Kali.