Kwaheri upinzani Tanzania

Kwaheri upinzani Tanzania

Upinzani ndio uliofanya ccm iwe makini sana katika kuchagua mgombea urais

Mkuu ongezea pia kuwa hata huyo Magufuli mwenyewe anajituma kwelikweli akijua kuwa kuna ufuatiliaji makini wa wapinzani. Hana wasiwasi kabisa na jamaa zake ambao huko bungeni kazi yao ni kuunga mkono hoja za serikali yake moja kwa moja bila mikwaruzo. Sanasana wanaishia kubembeleza majimbo yao yaonewe huruma na kukumbukwa walau kwa "vichache".
 
Ccm haina wabunge hata mawazir ni shida,upinzan utaendelea kuwepo.Mtu ni mmoja tu,wengine wanasubir order.Jpm anatumia psychology kulead nchi,anachukua maumivu ya watz yaliyodumu kwa miaka mingi chin ya utawala wa ccm,yeye mwenyewe anakir amekuta vitu vya ajabu sana kuanzia ikulu mpaka uraian,mtu mmoja hawez kuyamaliza.Jpm anajaribu kuwapambanisha raia na watumishi wa umma kana kwamba utumishi wa umma walikuwa maadui wa raia,kumbe mfumo wa serikali ya ccm ndio uliowafikisha hapo walipo.Bado maisha ya watanzania wengi ni duni mno.
 
BYE BYE UPINZANI TANZANIA.


NAANZA kuona KIFO Kibaya kwa UPINZANI wa TANZANIA masikini ambao uliweza kuishi kwa kutegemea makosa na U DHAIFU wa SERIKALI,

SASA hivi RAIS akitoa HOTUBA inaungwa mkono na WATANZANIA wote na wanaijadili kwa muda mrefu huku kila HOTUBA ANAYOTOA ikileta MATOKEO ya moja kwa moja kwa WANANCHI mfano aliposema kuhusu ufinyu wa BAJETI wa MAHAKAMA baada ya siku amewakabidhi BILIONI 22, Amezungunza na wazee wa DSM kuhusu JENGO la WAZAZI MUHIMBILI tayari JANA MAOFISA wa WIZARA WAMEHAMA na leo kazi ya kuweka VITANDA inaendelea ili WAJAWAZITO walale humo nauonea HURUMA sana.

UPINZANI ndio maana kila SIKU unazungumzia suala la ZANZIBAR kama AGENDA kuu Sasa sijui baada ya MARCH 20 UCHAGUZI utakapokwisha sijui WATAONGEA nini MASIKINI,
WA JIANDAE tu turudisha VITI VYA UBUNGE mwaka 2020 kwa CCM WALIOVIAZIMA MWAKA JANA

ITAKUWA ni HUZUNI kubwa kwa UPINZANI wa Tanzania kila UKIHANGAIKA WANANCHI hawana muda nao WANASIKILIZA kasi ya RAIS tu katika FALSAFA yake katika KUPAMBANA na UFISADI aliyoipa jina la KUTUMBUA la MAJIPU .

bYE BYE UPINZANI TANZANIA.
Kina Tyson mko wengi
 
mimi si mpinzani lkn upinzani hauwezi kufa.hayo yote yanayo fanywa na makufuli ndio yalikuwa yakisemwa na upinzani.ukumbuke upinzani ulisha tengeneza kizazi chake.


Mimi huwa nachukia sana mtu akikosea jina...hivi hiyo 'makufuli' umeandika sarcastically au umekosea tu kwa bahati mbaya...Jina la Rais wetu ni John Pombe MAGUFULI.
 
Ww unaesema kwa heri upinzani inaonekana una jipu la mgongoni watawala wasipoliona ,UKAWA watalianika.
 
Strictly speaking,
Upinzani utakufa hadi kufikia 2020
Maana wapinzan hawajui kazi zao.
Wapinzan wanafanya kaz moja tu nayo n kuipinga serikali iwe inafanya kazi nzuri wao wanapinga tu.

Kwa style hio ya kusubiri kupinga kila
Had kufikia 2020
Watakosa vya kupinga
maana kila JPM anachoongea kinakuwa n amri ya serikali na kinatekelezwa mara moja
Hio imewashtua wapinzan wengi
Wamebak kutoka nje ya bunge na kuzomea tu.
Wewe unajua kazi yako??
 
Nyie ni wale mnaosukumwa na mihemko na wepesi kidanganyika.
Sasa aseme leo vitanda vipelekwe asubuhi ukute tayari vipo..huo mchanganuo na taratibu zilifanyika saa ngapi??
Hiyo ni sawa na maigizo alakini ana watu wake kama nyie mnamuelewa
 
Ukitamani upinzani kufa inamaanisha ubongo wako umegoma kusoma vitu vipya itabidi uoteshewe ubongo mpya
 
Kama serikali haina madhaifu ni kwanini serikali imehujumu bunge kurushwa live?
 
Kifo cha ccm kitakuwa kibaya kuliko aina zote za vifo zinazojulikana ulimwenguni....
 
JPM ni mwanadamu, anafanya makosa na atafanya makosa mengi mbeleni. Kitu kizuri ambacho anahitaji kukitunza ni ile tabia ya kumzungumzia mnyonge, kumfikiria yule ambaye hana wa kumtetea. Wanasiasa wengi wa Afrika hushindwa uongozi kwa sababu unafika wakati wanashindwa kuoanisha urais wao na maisha ya mnyonge ambaye hana wa kumsemea.

Anaposema kuwa watu wamuombee, inabidi wale wanaomuombea wakumbuke kuweka kwenye sala zao, lile ombi la kumuepusha rais na zile roho za kuwasahau wanyonge. Umaarufu wake utafifia kama sio kupotea kabisa, siku atakayoanza kuondoa ule muunganiko wa urais wake na maisha ya mnyonge asiyekuwa na mtetezi.
Noted sir.
Nice and fair comment
 
Sera za Magufuli zote ameiba upinzani.

Ataendelea kusubiri kusikia wapinzani wanasema nini ili na yeye aseme.
 
Hayo majipu yaliyotumbuliwa yamemsaidia nini mlalahoi je sukari,unga,mchele,mafuta na au vyakula vimeshuka bei??
 
Naweza kukuhakikishia kuwa wapinzani hawatakosa la kuzungumza hata kwenye serikali zilizoendelea kama Uingereza na Marekani au Canada, Australia, Sweden, etc upinzani una mambo tele na ajenda mpya kila siku sembuse hapa kwetu ambapo hata wajinga wana mambo tele ya kuikosoa serikali yao.
Upinzani lengo lao si kuikosoa serikali na hili ndio kosa kubwa ambalo labda mleta mada anazungumzia!
Lengo kuu la vyama vya siasa ni kuoffer mbinu mbadala ambazo zitasaidia ustawi wa jamii! Shida kubwa ni consistency ktk itikadi za vyama vyetu, kimantiki hakuna tofauti yeyote ya msingi ktk vyama vyote karibu 20 vilivyopo nchini!
Wote wanaabudu ktk itikadi za Nyerere, wote wanafikiri nchi hii kazi yake ni kutengeneza mazingira ya kumsaidia mnyonge, wote hawajui ni mfumo upi hasa wa kutoka nao! Lkn wanafanana zaidi wote wanaishi kibepari na kuhubiri ujamaa wa kumkomboa mnyonge!
Kwa kutojitambua huku, huwezi shangaa kuona kuwa msingi Mkuu wa siasa zetu ni majungu, sababu chadema, cuf etc hawana alternative plans kwa shida alizonazo Mtanzania na badala yake wana capitalise ktk majungu ambapo watahangaika kumuonesha mwananchi kuwa hawa jamaa wanapiga!
 
Back
Top Bottom