Kwa wenye swali lolote kuhusu water quality

Nmegundua kitu kimoja,wakat fulan elimu y darasan inaweza kuwa useless compared to reality,look!unasemaje et TDS haina uhusiano n pH did you what is TDS?,bila shaka ww huna knowledge ya neno minerals,n pia nna mashaka ata km umewahi ku work ktk field za maji,n km umewah kufanya basi haukuiva,listen bro!twende kwa facts chukua raw water pima TDS,then pima TDS ya treated water yaliyotoka kweny RO,kisha urudi hpa unipe technical reasons nini kimesababisha PH ya raw water kuwa kubwa compared to pH ya maji yaliyotoka ktk RO,nliposema filters umeelewa sivyo,look!ww umemaanisha "micron filter"y kweny RO ambayo umetaja n diameter yke ambayo imekuwa recommended ya 0.5micron,Mimi nlimaanisha "Filters ambazo zona n resins,ambazo kazi yke n kutrap ions kwa maana ya Anions na Cations ambazo n Calsium,Magnesium etc,visima vingi tu hpa Tanzania kwa watu wenye fedha zao wamefunga izo kupunguza minerals contents katika maji yao,!next time make sure unapinga kitu kwa facts siyo kupinga tu ilimradi!hope umenielewa,ucporidhika km upo dar ntafanya arrange nikukaribishe kweny ofcn tuongee ki practical zaid.
 
Mkuu swali lako liko very closed,nikiimanisha halijakuwa specific,unapozungumzia visima,c visima vyote vina maji yanayofanana kwa maana kiasi cha minerals contents,vpo visima ambavyo ukichimba ukionja maji yke utafikiri umelamba chumvi,sasa kisima km iko maji yke pia yatategemea unafanya irrigation y mazao gan,je!yanahitaji chumvichumvi?au la,lkn kwa kawaida mazao mengi yanahitaji chumvi kiasi kwa iyo baada y kupima sample y maji yko wataalam watakushauri kwa wakati huo kama maji yko yanafaa kwa irrigation ya mazao fulan fulan,kwa iyo kajibu swali lako mkuu jibu n kwamba ili ujue kisIrma chako kinafaa kwa umwagiliaji n vema ukapimiwa sampuli ya maji y icho kisima,then maji ndo yatasema ufanye nn,
 
Naomba kujua, unawezaje kufanya analysis ya maji ya kisima unayoyatumia nyumbani ili kujua composition yake? na je, kuna wakati underground water (kwa Dar Es Salaama) yamewahi kureportiwa kuwa yana elements/compounds ambazo ni dangerous? kama kuna maeneo ambapo maji yake si salama kwa kunywa na kupikia tunaweza kufahamu.
 
Maji ya maeneo karibu na Pwani ya bahari kama Bunju, Kunduchi na Kigamboni huwa na chumvi nyingi, je ni ile asili ya bahari aukuna sababu nyingine? nini kifanyike kuboresha quality ya maji husika? je kuna filters za kurekebisha hali hiyo? gharama zake zikoje?
 
Mkuu am not sure kwa swali lako,ila nafkiri Hardness determination n key parameter,kwa sababu determination iyo itakupa mwanga kujua Maji yko yana salt kiasi gani though kwa case ya salty unaweza fanya ata salinity determination,ndo maana salt water siyo reccomended kwa construction,n kwa iyo zege pia.
 
Mkuu,mbn umemjibu kirahisi sana usitake nihamini kama ww s water quality expert,wakat nakuamini we n miongoni mwetu,sababu unaweza kuta kisima chake kipo karibu n industrial area let say battery industry n wanadischarge waste water as final waste karibu n kisima chake unafikiri ayo maji yanafaa kwa umwagiliaji?icho kinachomwagiliwa c kitakauka,au kisima kina chumvi za kutosha tu je!kisima icho unahisi kitafaa tu kwa umwagiliaji?kwan c mazao yote yanahitaji salt nyingi.think twice!
 
Swal zuri mkuu,maeneo uliyotaja hpo yote yamemekuwa n maji y chumvi sababu kubwa ni ya ki-hydrology, kwamba mkondo wa maji chumvi umepita maeneo tajwa hpo juu,n usishangae pia maeneo ayoayo uliotaja hpo ukakuta ndan y ayo maeneo let say kigamboni utakuta c kigamboni yote una maji chumvi,ndo hpo tunasema sehemu unayokuta maji chumvi yameathiriwa kwa kiasi kikubwa n mkondo wa bahari wa maji Chumvi,kuhusu nn kifanyike kuiprove water quality kwa case y maji chumvi mkuu inahitaji investment kwa maana y technical personal,technology,capital,inawezekana kabisa kufanya salt water kuwa fresh water,ntakupa mfumo Dubai wanafanya kitu kinaitwa "Desalination"process kutoa maji chumvi kuwa fresh water wale jamaa maji Yao wanategemea bahari n TDS ya ni kubwa hakuna mfano,wamefunga RO za capacity kubwa mno n wamefanikiwa,unajua Tz hatujawa n water shortage kiasi icho adi ku impliment "Desalination process"km wenzetu,hpo Sudan tu ukifika ndo utajua shida y maji maana yke nn,wale hawapotez maji ata kidgo wanafnya kitu kinaitwa recyling yaan maji machafu wana ya treat again kuwa fresh water,kuhusu filters mkuu zinapatikana ila ili kujua inayokufaa mara nyingi wauzaji uhitaji report y kitaalam y maji yko baada y kupima yana minerals kiasi gani n hpo ndipo wanakushauri size ya filter inayokufaa!
 
Mkuu your smart,kujibu swali lako si rahisi kufanya analysis za maji mtu ambaye hana knowledge ya water quality,sababu ata ukiwa n vifaa vya kupima ayo maji utashindwa ku-interpret results ulizopata ili uchukue action stahiki,swali lako lapil iyo case uliyosema haikuwa dar nzima,n ilichangiwa n discharged za waster water from industry,msimu wa mvua tabia y kuzibua vyoo ovyo sasa mvua ilikusanya vyote ivyo direct kweny visima ambavyo avikuwa protected n mifuniko ndo ikasababisha izo hazard,n iyo n kwa surface water,ni ngumu underground water kuwa contaminated!
 
Pole sana mkuu,nataka nikuambie hii thread ni ya water quality,kwa iyo kuuliza kitu Yule anaejua jibu sahihi atakuja jibu,kwa iyo wakat fulani unaweza usipate unachouliza kulingana n reply za baadhi y watu,nmefuatilia conversion zenu n aliekuwa anakujibu kana kwamba hamkuelewana,but ucjal be comfortable kuuliza tena na tena utapata reply za kitaalam,your welcome!
 
Mkuu kama upo dar,kuna kampun kama HENKEL Chemicals,TATA chemicals unaweza pata unachohitaji!
 
Mkuu unaposema seasonal variation unamaanisha nn?na umegusia hali Ya hewa nayo npe maelezo yke kvp?na kvp soda Ash (Naco3)huondoa minerals contents?nifahamishe hpo km cjaelewa!Asante
Mkuu ninapozungumzia seasonal variation nina maanisha kipindi cha kiangazi na masika. Kama unavyofahamu kipindi cha masika mvua huwa zinanyesha sana na kima cha maji huwa kinaongezeka kutokana maji kupenya ardhini (infiltration), Sasa kama maji ya mvua yataongezeka na huenda haya maji yakawa ni acidic rain (sulphuric acid-H2SO4 au Nitric acid-HNo3). Kwa faida ya wengine acidic rain inasababishwa na deposition of chemicals (kama sulphate-So4, carbondioxide-Co2, Nitrogen gas etc) kwenye anga (atmosphere). Hizi gesi/chemicals angani linasababishwa na shughuli zetu za kila siku kama moshi wa magari, kuchoma misitu, moshi wa viwandani n.k na matukio ya asilia kama volcano.

Sasa hizi chemicals/gesi zinapokuwa angani zina-react/zinaungana na maji wakati mvua inanyesha na kusababisha acidic rain. mfano So4 + H2O = H2So4 (acidic rain). Katika kipindi cha masika maji ya mvua (acidic rain) yanapopenya ardhini yanaenda moja kwa moja kwenye mkondo wa maji na kufanya yaungane na hayo maji, sasa kama unatumia kisima kama chanzo cha maji (underground water) na kisima kinategemea maji kutoka kwenye mikondo ya maji (water table). Haya maji ya acidic rain yanapoingia kwenye kisima chako kutoka kwenye mkondo wa maji ni lazima yabadili minerals content maana yanakuja na baadhi ya chemicals/gesi ambazo zimezitaja hapo, obvious lazima pH ya maji ibadilike ndio maana nilisema seasonal variation. Hali ya hewa pia inaingia hapo hapo kwenye seasonal variation pamoja discharges of gaseous molecules to atmosphere.

Kuhusu NaCo3 (sodium carbonate) kwenye maji ya kunywa (drinking water) inatumika kama pH regulator kuligana na raw water mineral contents. Mara nyingi underground water (maji ya kisima) yanakuwa na pH chini ya 6 (acidic-pH), Kwa hiyo ilikuongeza pH anghalau kufikia 7 tunaweka base (mfano. Na2Co3). Jambo la msingi katika kutumia Sodium carbonate kama pH regulator mpaka ujue mineral contents za raw water ili isije ikasababisha reaction nyingine.

Ahsante.
 
Sasa umejibu vizuri mkuu,sikuwa nmekuelewa ile mwanzo uliposema sodium carbonate inaremove minerals,ndo maana nikaomba ufafanuzi,na ulichokieleza hpo ndo kazi kubwa ya soda Ash,lakin pia umesema raw water ina pH below 6?hpo sikuungi mkono,n afikiri ni treated water kwa maana y maji yaliyotoka katika RO ndo huwa n pH around 6,na ndio maana ata iyo soda Ash uwekwa after treated water n siyo before kwa maana kwenye raw water!
 
Naendelea kupata elimu japo kuna mdahalo mkubwa huku.... Kwenye coz zangu nimesoma waste water treatment and disposal, water resource engineering (this semester) ila naona vitu vingi hum bado vipya so mdahalo wenu unanipa somo sana na kunifungua akili.
 
Wazo zuri lakini kuna mambo ya msingi ambayo unapaswa kuyazingatia na kuyafahamu kabla ya kuanza.

Kwanza kabisa unatakiwa kuchagua eneo ambalo unataka kuanzisha hiyo firm yako.

Ukishapata pata eneo kabla ujaanza shughuli yoyote shauriana na wataalam mchague chanzo cha maji kulingana na ukubwa wa kiwanda.

Mkishakubaliana kama ni kisima, tafuta wataalam wa geology ili waweze kupima eneo husika kujua kama maji yanapatikana ktk eneo husika. Kama yanapatikana kwa kiasi kinachofaa unaweza kuanza kuchimba kisima halafu na kuchukua sample ya maji ili kupima mineral content zilizomo (hii itakusaidia kujua mfumo wa kutibu maji kulingana na quality of raw water yako).

Baada ya hapo Pima discharge rate uangalie kisima kinaweza kutoa maji lita ngapi kwa siku na uangalie uwezekano wa maji kukauka au kupungua hasa kipindi cha kiangazi ili usije kuanza halafu baada ya muda kisima kikakauka.

Baada ya hatua zote izo unaweza kujenga jenga kama godown ambalo utaligawa sehemu muhimu: sehemu ya kutibu maji, sehemu ya packaging, sehemu ya kutengenezea chupa, store na sehemu ya ofisi.

Katika Chumba cha kutibu maji tuweka raw water storage tank, filters (sand &'carbon), NF, RO, ozone machine, pure water storage tank... Kwenye hiki Chumba utafungiwa mfumo ambao ni computerised (self operating) kwa hiyo hiki Chumba kitahitaji mtu mmoja au wawili kwa kazi ya operation, data reading na kuadd chemicals kama Antiscalant & pH regulator.

Chumba cha packaging utafunga pia machine zote muhimu kwa ajili ya bottle cleaning, water filling & caping, bottle printing (priniting machine especially expire date), na machine kwa ajili ya kupack chupa za maji pamoja kama dazani 1.

Chumba kwa ajili ya kutengeneza chupa na cap kitakuwa na machine zake na umbo na size ya chupa unazotaka.

Uwe na store pamoja na ofisi na gari aina ya canter kwa ajili ya kusambazia maji.

CHANGAMOTO
Changamoto kubwa katika kiwanda ni kuharibika kwa baadhi ya part ktk machine. Mara nyingi machine za chumba cha packaging ndio zinasumbua Mara kwa Mara mfano printing machine ikihalibika tu hamwezi kupack maji maana yenyewe ndio ina print expire date kwenye chupa za maji (uwezo kuuza maji bila ya kuwa na expire date).. Mara nyingi hii machine hua inasumbua.

Kwa hiyo utapokuwa una nunua machine nunua na spare parts za muhimu in case tatizo likitokea unafunga mwenyewe badala ya kuagiza. Kuna baadhi ya spare parts unakuta kuna duka 1 tu ndio linauza (kariakoo), na bei zao ziko juu yaani kifaa ambacho ukikiagiza mpaka kinafika inaweza kukugharimu laki 9 lakini wao wanauza milion 7. Kwaiyo ni vizuri kuwa na baadhi ya spare parts.

Kuhusu kufunga machine, watakao kuuzia machine ndio waje wakufungie ili kuepuka shida yoyote itakayojitokeza wakati wa ufungaji. Lakini pia unapaswa kuwa na mtaalamu ambaye atapata maelekezo kutoka kwa hao waliokuuzia ili kufahamu jinsi ya kufanya maintenance na kutatua common problems.

Bei ya vifaa inategemeana na campun utakayonunua ila wachina wako cheap sana kuliko makampun mengine.

NB:hakikisha unapata vibali vyote muhimu kwanza kabla ya kuanza kujenga

ÑaombA kuwasilisha... Kwa msaada wowote usisite kuniuliza
Mheshimiwa asante sana kwa ushauri wako. Naona kuna vitu unavijua pasipo shaka sasa pls nimashine zipi ambazo ni nzuri especially zisizosumbua.
 
Sasa umejibu vizuri mkuu,sikuwa nmekuelewa ile mwanzo uliposema sodium carbonate inaremove minerals,ndo maana nikaomba ufafanuzi,na ulichokieleza hpo ndo kazi kubwa ya soda Ash,lakin pia umesema raw water ina pH below 6?hpo sikuungi mkono,n afikiri ni treated water kwa maana y maji yaliyotoka katika RO ndo huwa n pH around 6,na ndio maana ata iyo soda Ash uwekwa after treated water n siyo before kwa maana kwenye raw water!
Mkuu nimesema MARA NYINGI MAJI YA KISIMA (UNDERGROUND WATER) YANAKUWA NA PH BELOW 6. Nimesema hivi kwa sababu ukichukua sample ya maji ya kisima (underground water) kabla haijapita kwenye treatment yoyote Mara nyingi pH yake inakua acidic in nature (below 7), lakini haina maana ya kwamba maji yote ya kisima lazima pH iwe acidic.

Ndio maana kwny treatment plant nyingi tunatumia sana base kama pH regulator compared to acid.

Nini maana ya kutumia sana base kama pH regulator kuliko acid? Maana yake pH ya maji iko chini ya desirable standards. Lakini pia nakubaliana na wewe kwa upande mwingne
 
Back
Top Bottom