Kwa wazazi na walezi: Mada maalum ya watoto

Kama mtoto akipaliwa unapaswa kufanya nini?
Wengi wetu hukimbilia kumpa maji au kumpiga piga mgongoni bila kujua hasa nguvu anayotumia hii ni hatari kwa afya ya mishipa na mifupa ya mtoto
Mtoto akipaliwa mpulize taratibu kwenye paji la uso na hata puani
Mie huwa nafanya hivyo na ina work. Ila mpk leo sijajua logic behind.

Au mtt akienda kwikwi unakata kiuzi cha nguo yake alovaa unakiviringisha unamuwekea juu ya paji lake baada ya muda kdg kwi kwi inakata.
 
Jamani loh atachekwa ukubwani subiri tafadhali hakuna madhara japo najua kuna wataalam watakuja na hoja za kupinga hili
Daktari alinambia hilo swala la kuwa kibamia sio kweli hasa hasa itamsaidia kupona haraka kuliko hadi awe mkubwa
 
Ooh kumbe hata asubuhi anaweza kuanza na msosi heavy mi huwa nadhani vema kuanza na vitu laini kama vile maziwa na yai, au supu au uji kumbe hata ndizi samaki anakula tu, ahsante kwa experience mupya
Maziwa ya ng'ombe hawanywi. Asubuhi chai au juice na vitafunwa vya kawaida vilivyozoeleka.
 
Back
Top Bottom