joram azimio
Member
- Feb 27, 2012
- 5
- 3
Maelezo yako na ushauri wako nakubaliana nao kwa kiasi kikubwa.
Isipokuwa nilitaka nikufahamishe jambo moja kwamba wakazi wa serengeti kwa asili shughuli zao kubwa ni ufugaji, kilimo na uwindaji, wamekuwa wakifanya uwindaji huo miaka na miaka lakini bado hawakuvuruga ecosystem kama ambavyo tumekuwa tukilazimishwa kuamini. Wananchi wa serengeti hawajawahi kutegemea uwindaji kama njia kuu ya kujipatia kipato ama maendeleo bali kilimo na ufugaji.
Suala la vijana kukaa kijiweni lilikuwepo na bado lipo kutoakana na kutokuwa na mwamko wa elimu, ingawa sasa mambo ni tofauti sana, vijana wengi sana sasa wanasoma na hao ndio mategemeo makubwa kwa ajili ya maendeleo ya wilaya yetu.
Nikizungumzia ajira za Mahotelini sio kweli sana kama unavyodai, tunao vijana ambao si wengi waliokuwa wamesomea kozi za hoteli na utalii lakini bado hawakupata ajira katika mahoteli yaliyoanzishwa, hii ilisababishwa na mameneja waajiri wengi kuajiri watu wao ama watu kutoka huko kwao, kiujumla kulikuwa na upendeleo mkubwa sana. Mimi binafsi mdogo wangu alikuwa amemaliza certificate ya hotel management lakini alifanya intervie mara tatu na kuachwa, alipokuja dar akafanikiwa kupata kazi hotel moja hapa jijini. Baada ya wananchi kulalamika kwamba watoto wao hawaajiriwi na badala yake wanaajiriwa watu wengine hasa kutoka Arusha, Kilimanjaro, Mwanza na Kenya ndipo baadhi ya waliokuwa na sifa wakapata nafsi ya kuajiriwa na mdogo wangu wakamuita na kwakuwa walimpa maslahi mazuri comapred na huku alikokuwa nikamshauri aende.
Lakini pamoja na hayo yote niliyosema bado tunawajibika kupigana zaidi ili kufikia malengo kama mikoa na wilaya nyingine.
Mkuu kwa jinsi watu wa wilaya ya serengeti na tarime walivyo wachapa kazi wakiamka kielimu naamin watafika mbali sana japo kuna vikwazo vya kimfumo kama vile makao makuu makuu ya hifdhi kuwekwa Arusha bila sababu za msingi.Tuweke mkakati wa pamoja ili vijna wasomi + wengine wa maeneo hayo wakumbuke kuwekeza huko kwani tuko ambao sio wa huko kiasili lakin tunapenda mkoa huo kwa jinsi tunvyoujua tofauti na watu wengine ambao huwa wanakimbilia tu kukosoa mkoa huo kw maneno bila kufanya critical analysis ili kujua undani wa masuala yalivyo.Lets work up,wakisikia kuna fursa watakuja mbio tu.