Kwa wateule hawa, bora Pascal Mayalla asiteuliwe maana itakuwa kumdhalilisha tu

Kwa wateule hawa, bora Pascal Mayalla asiteuliwe maana itakuwa kumdhalilisha tu

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
7,170
Reaction score
8,622
Haiwezekani kichwa kilichojaa nondo na busara kama Pascal Mayalla kiwe kwenye teuzi na kundi moja la wanasiasa kama hawa.

Ukiangalia majina yalivyotoka ni wazi kuwa majina anapelekewa mwenye mamlaka ya kuteua bila kuangalia nani anafaa na ananondo za nguvu kiasi gani.

Ushauri tu kwa kada wa CCM ndugu Mayalla awe mshauri tu wa serikali maana kuteuliwa sio ishu. Kama wasio na nondo na wapiga kelele wanateuliwa kuna nini cha maana kupata teuzi?
 
Siku Pascal mayalla akiteuliwa cheo chochote akija kukutana na Pascal Mayalla wa Jamii forum watapigana sana, hizi Akili zipo tu kabla ya vyeo ila baada ya teuzi hutaamini tena kama ndio yeye.
Nasema watapiganaaa.

Mama Samia na mie u-DAS please
 
Paskali naona anafaa kwenye ukurugenzi wa mji/jiji.
 
Shida ya Pascal Mayalla kajificha humu JF tu na haonekani kwenye MAINSTREAM MEDIA sa mama atamuonea wapi? Hivi Mayala wa kumfananisha na G. Zakaria, au Nikki II au Nyangasa?? Hell No!!

Nahisi a little effort has to be done to promote him.

Hivi tukiamua kwa nguvu moja regardless ya tofauti zetu kum-publish Mayala mnadhani hatatoka???

Tujaribuni tuwe na mwakili wetu.
 
SSH ameanza kupwaya sana sana.

Naona amewapa shavu wale waliofika bei na wasanii wasio na tija kabisa
 
Back
Top Bottom