Kwa waliozoea vya kunyonga, kwa Maxence Melo wamegusa nyaya!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
14731382_10209187595079724_4073162889581117901_n.jpg

Maxence Melo: Wamiliki wa JamiiForums (JF) ni Watanzania wanaoitumia.

Naam, wanaoimiliki na kuitumia JamiiForums ni Watanzania wanaoisimamia katika mfumo wa uendeshaji wa jumla...JF haiendeshwi na mtu moja. Maxence Melo si mwanzilishi pekee wala mmiliki pekee wa Jf na ndiyo sababu, pamoja na yeye kushikiliwa na Jeshi la Polisi, tupo tunaendeleza mapambano.

JF ni jukwaa la habari, jukwaa la mijadala na jukwaa la elimu, zote kwa pamoja, na kwa sababu hiyo inawagusa Watanzania wote kwa namna moja ama nyingine. JF ni jukwaa huru na mtu yeyote mwenye umri usiopungua miaka 18 yuko huru kujiunga bila usumbufu na kufyonza elimu itolewayo.

JF ni jukwaa ambapo koleo huitwa kwa jina lake na nyani ngeledi hukomwa bila kumtizama uso wake. Vita iliyotangazwa dhidi ya JF ni vita dhidi yetu Watanzania. Watawala wa nchi hii wameamua kutuziba midomo tusihoji tulikotoka, tuliko na tunakoelekea. Uhuru wa maoni uko hatarini kutoweka.

Hapana, hatukubali. Tukisalimu amri kwa vitendo vya hawa walevi wa madaraka, tumekwisha na hatutakuwa na nchi. Uhuru wa kujieleza ni haki na wajibu wa kila mwananchi ndani ya taifa hili. JamiiForums kimekuwa chombo pekee mbadala pale vyombo vingine vya habari vilipokubali kutumika kuficha ukweli.

[HASHTAG]#freemanxencemelo[/HASHTAG] now!

Herbert Hoover: Every dictator has climbed to power on the ladder of free speech. Immediately on attaining power each dictator has suppressed all free speech except his own.

Kila dikteta alipanda madarakani kupitia ngazi ya uhuru wa kujieleza. Mara baada ya kutwaa madaraka kila dikteta amekandamiza uhuru wa watu kujieleza isipokuwa wake mwenyewe.
 
JF imesaidia sana kukuza demokrasia na uhuru wa kujieleza Tanzania

JF imesaidia kufufua ufisadi kwenye wizara/mashirika mbalimbali ya serikali

Hatuwezi kukaa kimya kuona mchango wa JF unapuuzwa,hatuwezi kukaa kimya kuona uhuru huu unazimwa


[HASHTAG]#FreeMexenceMelo[/HASHTAG]
 
Kupambana na serikali ni ngumu Sana Fuateni tu Sheria zinavyosema tuendelee kuijenga nchi yetu...

Long live our Country.
Nani anaye pambana na serikali? Acha mawazo mgando. Tunapigania Katiba kuheshimiwa kwa manufaa yetu na ya watoto wetu. Serikali na watawala wake watapita nchi itabaki. Hatuwez tukaacha wapita njia wa tufanye yuhame kwenye misingi inayoongoza nchi. Wenzetu wana pakukimbilia. Amani ikitoweka tutakimbilia wapi? Waluoingia kwenye machafuko walishayafanya haya tunayofanyowa now wakaona hata wakitulia watauawa so bora wauwawe wakiwa wana tafuta haki. This is terrible!
 
Kupambana na serikali ni ngumu Sana Fuateni tu Sheria zinavyosema tuendelee kuijenga nchi yetu...

Long live our Country.

Na kinyume chake (serikali kupambana na uma ) ni sawa na kuzuia mkondo wa bahari iliochafuka. Serikali kama serikali itimize wajibu wake wa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria bila ya kuminya uhuru au kujaribu kutumia mkono wa chuma. Watanzania wengi tunajua wajibu wetu kwa taifa letu lakini pia tunazijua haki zetu kama raia. Huu si wakati tena wa mtu au kikundi kujiamulia kufanya wanavyotaka na wala si wakati wa kutisha au kutishika kisa mtu/watu fulani wanalazimisha kutawala kwa mkono wa chuma! Hizi ndio zama za utandawazi na tunawahakikishia watawala wa jinsi hii kama watashindwa tu.
 
JF imesaidia sana kukuza demokrasia na uhuru wa kujieleza Tanzania

JF imesaidia kufufua ufisadi kwenye wizara/mashirika mbalimbali ya serikali

Hatuwezi kukaa kimya kuona mchango wa JF unapuuzwa,hatuwezi kukaa kimya kuona uhuru huu unazimwa


[HASHTAG]#FreeMexenceMelo[/HASHTAG]
Kosa wanalofanya hawa viongozi wetu ni kwamba hawafanyi tafakuri ya kutaka kujua kwa nini kihistoria imekuwa rahisi sana kuitawala hii nchi. Kwa miaka nenda rudi wananchi wamevumilia kila aina vituko kutoka kwa viongozi ambao ama hawasomi alama za nyakati au hawana dira kabisa ya wapi tunakoelekea.

JF imefanya kazi kubwa ya kuwakumbusha viongozi wajibu wao kwa wananchi wao na hapo hapo kuwazindua wananchi kuhusu haki zao. Utawala huu utakuwa unafanya makosa makubwa sana kama utaendelea kuziba macho na masikio na hivyo kutoweza kuona uvumilivu wa wananchi unaokaribia kufikia mwisho.

Vyombo vyetu vya ulinzi kwa sasa ni kama vimesahau jukumu lao kuu ambalo ni kuwalinda wananchi na mali zao na kwamba ili wafanikiwe lazima wawatendee haki. Kila siku daraja linajengeka kati ya vyombo vyetu vya usalama na wananchi kiasi kwamba jukumu kuu sasa ni kuwalinda viongozi dhidi ya wananchi.

JF forum imefanya kazi kubwa kuvishtua si hivyo vyombo tu bali na tabaka linalowatuma kuwanyanyasa raia kwa visingizio kama hiki kilichotumika kumkamata Maxense Melo. Wamekuwa wakiwakamata wananchi na kuwatesa bila sababu za msingi wakisahau kuwa wenye nguvu hasa ni hao hao wananchi.

[HASHTAG]#FreeMexenceMelo[/HASHTAG] now!

Kila dikteta alipanda madarakani kwa ngazi ya uhuru wa kujieleza. Mara baada ya kutwaa madaraka kila dikteta amekandamiza uhuru wa watu kujieleza isipokuwa wake mwenyewe.
 
Agenda kubwa ilikuwa katiba mpya, tukahamia uchaguzi, tukaendanda kwenye mjadala wa mikutano ya kisiasa, tukaingia kwenye UKUTA, tukandelea na Sakata la mpambanaji Lema (Nabii), kwa mbaaali ikatangazwa operation kata funua, tukajikuta kwenye sakata la kupotea Ndugu Ben Saanane, maiti za watu zikaonekana ruvu, mara tukaingia kwenye sakata la ndugu Maxence Melo. Dah! Tusimamie lipi sasa?
 
Back
Top Bottom