ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Enyi wanawake mliobahatika kuhudhuria hapo Diamond, Mwanamke mwenzenu huyu, ameshindwa kuwa nanyi katika hiyo kitu mnaiita " KITCHEN PARTY GALA'. Yeye yupo Matombo Morogoro, alisikia kwenye matangazo tu kuhusu hiyo kitu, alivutiwa na alipenda kujua huwa mnafundishwaga nini huko kwenye "Gala" lakini ameshindwa kuwa nanyi.
Nauli kutoka alipo kwenda na kurudi ni zaidi ya kiingilio na kwa muda wakumaliza mafundishio hayo (Saa Nne Usiku) ingemlazimu achukue gesti , ila amesikia ticket zilikuwa zinauzwa shear illusion mlimani city; 8020fashions sinza Mori,Shekinah garden mbezi makonde,Tsn supermarket mikocheni,born 2 shine MwengeTra,Jackz cosmetics kinondoni na bei ya Ticket ni tsh 30,000 .
Katika hilo alisikia pia kuna wengine ambao wanaruhusiwa kununua meza. Ameona hii inawahusu zaidi wanawake wenye nazo, waishio Dar Es salama tu, wasomi na ambao pengine ndoa zao zinahitaji msasa.
Labda kwa wenzako mlioenda mwaweza kusaidia kumpa yale yaliyojili huko,wanauwafunda kwenye nini??
Nauli kutoka alipo kwenda na kurudi ni zaidi ya kiingilio na kwa muda wakumaliza mafundishio hayo (Saa Nne Usiku) ingemlazimu achukue gesti , ila amesikia ticket zilikuwa zinauzwa shear illusion mlimani city; 8020fashions sinza Mori,Shekinah garden mbezi makonde,Tsn supermarket mikocheni,born 2 shine MwengeTra,Jackz cosmetics kinondoni na bei ya Ticket ni tsh 30,000 .
Katika hilo alisikia pia kuna wengine ambao wanaruhusiwa kununua meza. Ameona hii inawahusu zaidi wanawake wenye nazo, waishio Dar Es salama tu, wasomi na ambao pengine ndoa zao zinahitaji msasa.
Labda kwa wenzako mlioenda mwaweza kusaidia kumpa yale yaliyojili huko,wanauwafunda kwenye nini??