Kwa utapeli huu tuwe makini katika kutuma pesa

Kwa utapeli huu tuwe makini katika kutuma pesa

Okinawan

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2018
Posts
254
Reaction score
261
Habari,wanajamii jana kuna suala ambalo limenigusa sana na si mara moja kutokea bali ni mara ya pili juzi kuna ndugu yangu alitumiwa pesa kwenye mtandao fulani wa simu alipoipokea ile pesa haukupita muda alitumiwa meseji nyingine iliyomtaka arudishe pesa kwa wakala maana ilitumwa kimakosa,yeye hakuirudisha ile hela ila ilipofika jioni alianza kupigia simu watu wake wote ambao alikuwa na ahadi nao ya kulipana hela ndipo kuna mmoja akamwambia nilikutumia kiasi fulani asubuhi.

Hapo ndipo jamaa aliposhtuka kama ule ulikuwa ni utapeli Jana mimi nilitumiwa pesa kwenye mtando uleule kama anaotumia ndugu yangu ambapo baada ya kutumiwa pesa nikapokea meseji nyingine inayonitaka nirudishe pesa kwa wakala haraka maana namba ilikosewa kwasababu nilifahamu huu ni utapeli nilipiga namba ya huduma kwa wateja na keeleza yaliyonisibu kwakifupi waliniambia pole sana na siku nyingine niwemakini.

Swali nililojiuliza je,kama ningetapeliwa kweli fedha zangu zingerudi na kama wangenitapeli hawa watu ni untouchable na si rahisi kuwapata? Namba zinazoonekana kwenye hiyo picha ni namba za hao matapeli na hiyo meseji walionitumia msaada kwa wataalamu wa mambo
Screenshot_20180419-201542.jpg
 
Cha kujiuliza.
1. Wakala anajulikana kwa namba ya uwakala, na si yenye mpangilio kama wa namba yako wako.
2. Utaambiwaje utume pesa kwa "wakala" usiyemjua? Kwanini asikuambie uende kwa wakata ufanye kama unatoa hela?
3. Umetumiwa hela, OBVIOUS ni kwamba ulikuwa na ahadi na mtu au kuna mtu unamdai utaanzaje kutuma hela kwenda namba usiyoijua? Kama kuna mtu akatuma kimakosa,
Mtandao husika ndo huwa unatoa hela kwenye akaunti yako na kuiwekwa kwa aliyekosea.


Tuwe makini
 
Utaratibu unaelekeza usirudishe hela iliyotumwa kwako ki makosa hata kama imekosewa kweli. Utaratibu unaeleza mtu aliekosea kutuma Pesa ndo areport huduma kwa Wateja kwaajili ya kuomba kurudishiwa. unaweza ukafanya uungwana kuirudisha wakati huo huo kumbe na aliekosea alishawasiliana na huduma kwa Wateja, Kama kuna salio lako lengine watai reversal tena kama kawa.
 
Utaratibu unaelekeza usirudishe hela iliyotumwa kwako ki makosa hata kama imekosewa kweli. Utaratibu unaeleza mtu aliekosea kutuma Pesa ndo areport huduma kwa Wateja kwaajili ya kuomba kurudishiwa. unaweza ukafanya uungwana kuirudisha wakati huo huo kumbe na aliekosea alishawasiliana na huduma kwa Wateja, Kama kuna salio lako lengine watai reversal tena kama kawa.
Point
 
Habari,wanajamii.Jana kuna suala ambalo limenigusa sana na si mara moja kutokea bali ni mara ya pili.Juzi kuna ndugu yangu alitumiwa pesa kwenye mtandao fulani wa simu alipoipokea ile pesa haukupita muda alitumiwa meseji nyingine iliyomtaka arudishe pesa kwa wakala maana ilitumwa kimakosa,yeye hakuirudisha ile hela ila ilipofika jioni alianza kupigia simu watu wake wote ambao alikuwa na ahadi nao ya kulipana hela.Ndipo kuna mmoja akamwambia nilikutumia kiasi fulani asubuhi.Hapo ndipo jamaa aliposhtuka kama ule ulikuwa ni utapeli.Jana mimi nilitumiwa pesa kwenye mtando uleule kama anaotumia ndugu yangu ambapo baada ya kutumiwa pesa nikapokea meseji nyingine inayonitaka nirudishe pesa kwa wakala haraka maana namba ilikosewa.Kwasababu nilifahamu huu ni utapeli nilipiga namba ya huduma kwa wateja na keeleza yaliyonisibu kwakifupi waliniambia pole sana na siku nyingine niwemakini.swali nililojiuliza je,kama ningetapeliwa kweli fedha zangu zingerudi? Na kama wangenitapeli hawa watu ni untouchable na si rahisi kuwapata? Namba zinazoonekana kwenye hiyo picha ni namba za hao matapeli na hiyo meseji walionitumia.Msaada kwa wataalamu wa mamb😵verView attachment 750502
Hiyo massage nimeipata sana Last week kwenye simu zangu zote halafu unahitaji nini kujua hiyo text ni ya kiyapeli? mbona iko wazi sana ni utapeli?
 
Hahahahahaaaa.

Nimeiona Babu, Ahsante pia na muhusika wa hiyo post pia
Na kwakuongezea tu... kuna mijamaa mitaalam ya kutuma msg za kuonesha umetumiwa pesa... then wanakutumia ujumbe au kukupigia simu kuwa umetumiwa kimakosa na kukusihi urudishe.. ukweli ni kwamba inayokuja ni msg tu! .... kama we ni msamaria mwema unataka urudishe.... angalia salio kwanza!!!!

Rudisha salio kama aliyekutumia mnafahamiana
. Kama hamfahamiani we mwambie kiungwana tu kuwa awasiliane na huduma kwa wateja wamrudishie mkwanja wake....!
 
Habari,wanajamii jana kuna suala ambalo limenigusa sana na si mara moja kutokea bali ni mara ya pili juzi kuna ndugu yangu alitumiwa pesa kwenye mtandao fulani wa simu alipoipokea ile pesa haukupita muda alitumiwa meseji nyingine iliyomtaka arudishe pesa kwa wakala maana ilitumwa kimakosa,yeye hakuirudisha ile hela ila ilipofika jioni alianza kupigia simu watu wake wote ambao alikuwa na ahadi nao ya kulipana hela ndipo kuna mmoja akamwambia nilikutumia kiasi fulani asubuhi.

Hapo ndipo jamaa aliposhtuka kama ule ulikuwa ni utapeli Jana mimi nilitumiwa pesa kwenye mtando uleule kama anaotumia ndugu yangu ambapo baada ya kutumiwa pesa nikapokea meseji nyingine inayonitaka nirudishe pesa kwa wakala haraka maana namba ilikosewa kwasababu nilifahamu huu ni utapeli nilipiga namba ya huduma kwa wateja na keeleza yaliyonisibu kwakifupi waliniambia pole sana na siku nyingine niwemakini.

Swali nililojiuliza je,kama ningetapeliwa kweli fedha zangu zingerudi na kama wangenitapeli hawa watu ni untouchable na si rahisi kuwapata? Namba zinazoonekana kwenye hiyo picha ni namba za hao matapeli na hiyo meseji walionitumia msaada kwa wataalamu wa mambo View attachment 750502
Kwanza je ni kweli hela iliingia ktk cm yko ? Tuanzie hpo ili nijujibu kitaalam
 
Na kwakuongezea tu... kuna mijamaa mitaalam ya kutuma msg za kuonesha umetumiwa pesa... then wanakutumia ujumbe au kukupigia simu kuwa umetumiwa kimakosa na kukusihi urudishe.. ukweli ni kwamba inayokuja ni msg tu! .... kama we ni msamaria mwema unataka urudishe.... angalia salio kwanza!!!!

Rudisha salio kama aliyekutumia mnafahamiana
. Kama hamfahamiani we mwambie kiungwana tu kuwa awasiliane na huduma kwa wateja wamrudishie mkwanja wake....!
Nimekuelewa Babu.
Be blessed.

Ngoja nimuite na Hajar aje apate haya madini kutoka kwa Babu
 
Hapo huyo aliyekosea ndio anatakiwa awapigie mtandao wa simu wairudishe hiyo pesa.
 
Khaaaa.
Niliona post unamwambia aende PM kwako without kumbe alighairi mfungulie bana.

Kwani sasa hadithi utahadithiwa na mjukuu yupi kama Hajar umemu Ban
Alikuja kavaa Jeans... sasa huo si ukosefu wa adabu? Kibaya zaidi alikaidi agizo langu la kunisaidia kushika mkongojo wangu...
 
Back
Top Bottom