Ulishawahi kujiuliza matapeli wa "Pesa itume kwenye namba hii" huwa wanasajili laini kwa vitambulisho gani?

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
10,206
12,747
Nafungua code TCRA na jeshi la Polisi Tanzania lifanyieni Kazi haraka ili kukomesha tabia ya wizi/utapeli kupitia simu.

Asalam alaykum Jammiya, Bwana Yesu asifiwe watumishi wa mungu hakika Kristo ni Tumaini letu sote Mimi na mwenzangu Cute Wife ni wazima wa afya.

Ni hivi mitandao ya simu Tanzania, Ina vibarua wanaopita mitaani wanaojulikana Kama mawakala (freelancers) Hawa hulipwa kwa commission kulingana na idadi ya sim card (laini za simu) watakazo sajili kwa mwezi na malipo yao hulipwa mwezi Hadi mwezi.

Hii shughuli ni mtu yoyote mwenye kujua na kusoma anaweza kufanya kazi na ajira zao hazina mkataba Wala hakuna Barua kutoka serikali za mitaa Hawa freelancers huwa Wana simamiwa na kiongozi wao (team leader) lengo ni kusimamia vifaa kazi /vya kutendea kazi lakini malipo ya mshahara wao hulipwa na system ya mtandao husika.

Twende kwenye point Kama kichwa habari kinavyojieleza.

Kumekua na meseji za "ile pesa tuma kwenye namba hii" /waganga kutoka sumbawanga/mtu kupiga simu nakuanza kujifanya katuma pesa kwenye namba yako.

Kwa kweli ukifikiria sana unagundua kabisa kuwa matapeli Wana Uhuru mwingi sana na wanajiachia sana.

Sasa swali linakuja je Hawa matapeli wanasajili laini kw kutumia vitambulisho vya Nani???

Kwa hali halisi hawawezi kutumia vitambulisho vyao maana wanahofia kukamatwa endapo Yale majina yatafatiliwa.

Matapeli hununua laini kwa Hawa freelancers (mawakala) wanaopita mtaani kusajili laini /wanaweza kujifanya hawana kitambulisho lakini wanahitaji sana laini husika kwa kuwa wakala anataka hela hufanya juu chini na kumpa tapeli laini bila ya kujua kuwa aliyempa laini ni MTU wa namna gani.

Kinachofanywa na mawakala (freelancers) ili kupata laini, wanapokua wanamsajilia mtu mwenye kitambulisho halisi humsajilia Mara ya kwanza na kukamilisha laini Kisha anamdanganya mteja kuwa ile namba ya kwanza mtandao umegoma kwa hiyo atamuomba mteja Tena kuchagua namba nyingine ili amsajilie Tena.

Mteja atakapo chagua Tena nakusajiliwa anakuwa amesajiliwa sim card mbili bila yeye kujua hapo atapewa moja na nyingine wakala anaondoka nayo kwenda huko anapokutana na mtu ndiyo hao matapeli anaiuza Kisha tapeli anaendelea kufanya kazi yake.

Huu mchezo unachezwa sana na hawa freelancers (mawakala) vitambulisho za mama zetu/bibi zetu/ wajomba zetu wanasajiliwa Mara mbili mbili sana na Kisha majina yao yanakwenda kutumika huko kutapelia watu.

Tcra mkishirikiana na Jeshi la Polisi NALIA NGWENA kupitia jamii forum nimeona nifungue mbinu ovu inaayotumiwa na freelancers (mawakala) wanaozunguka huko mitaani.
 
Kutokana na hilo nafikiri mitandao ya simu ikaweka utaratibu wa kuhakiki namba ya simu mara baada ya kufanya usajili. Kupitia zoezi Hilo yule aliyesajiliwa namba ya simu kimagendo ama kinyemela ufungiwa huduma na kubaki kwa mmiliki halali wa kitambulisho cha taifa.
 
Kwa kuanzia, serikali ingepiga marufuku makampuni ya simu kuruhusu watu wasio na sifa, kusajili hovyo wateja wanao hitaji hizo laini za simu.

Badala yake, hilo zoezi lingefanywa na mawakala wa huduma za kifedha, ambao wana leseni za biashara na Tin number. Kupitia njia hii, hawa wapuuzi wangepungua sana, kama siyo kuisha kabisa.
 
Kutokana na hilo nafikiri mitandao ya simu ikaweka utaratibu wa kuhakiki namba ya simu mara baada ya kufanya usajili. Kupitia zoezi Hilo yule aliyesajiliwa namba ya simu kimagendo ama kinyemela ufungiwa huduma na kubaki kwa mmiliki halali wa kitambulisho cha taifa.
Kwa wewe mtoto wa mjini utafanya hivyo je wale wa kijijini

Wazee wetu wasiojua A au B huo muda hawana yaani Kuna watu akishasajili laini hayo Mambo yakusajili Tena au kuhakiki usajili huo muda hawana

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwa kuanzia, serikali ingepiga marufuku makampuni ya simu kusajili wateja hovyo. Na badala yake, hilo zoezi kingefanywa na mawakala wa huduma za kifedha, ambao wana leseni za biashara na Tin number.
Wazo zuri mkuu hapa naunga mkono lakini siyo Hawa mawakala wa mtaani wengi wao ni wezi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwa wewe mtoto wa mjini utafanya hivyo je wale wa kijijini

Wazee wetu wasiojua A au B huo muda hawana yaani Kuna watu akishasajili laini hayo Mambo yakusajili Tena au kuhakiki usajili huo muda hawana

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mitandao ya simu wanalo jukumu la kutoa elimu kwa wateja wao juu ya uhakiki wa namba zao za simu mara baada ya kusajili, pili mifumo yao inabidi kutambua namba ya NIDA iliyosajili namba zaidi ya moja kwa mtandao mmoja na kuomba uthibitisho wa mmiliki dhidi ya namba hizo.
 
Kuna ile namba ya kuangalia jina lako lime sajili idadi ngapi za line ya simu kwa mtandao husika, mf: tigo jina lako linasoma una line ngapi za tigo, airtel, voda na halotel ni hivyo hivyo pia inakupa option ya kufunga namba za simu ambazo either huzifahamu au huzitumii tena

Namba nimeisahau ila kama kuna anaeikumbuka aiainishe hapa! Nakumbuka kwa tigo mimi ilisoma nina line 6 nikapunguza nikaacha mbili ambazo ni active ila hizo nyingine nilizo futa kuna baadhi sizijui na wala sikuwahi ziona, kwa aitel nilikuta mbili nikaipiga chini moja nikabaki na moja na Voda nilikuta moja
 
Mitandao ya simu wanalo jukumu la kutoa elimu kwa wateja wao juu ya uhakiki wa namba zao za simu mara baada ya kusajili, pili mifumo yao inabidi kutambua namba ya NIDA iliyosajili namba zaidi ya moja kwa mtandao mmoja na kuomba uthibitisho wa mmiliki dhidi ya namba hizo.
Kweli kabisa mkuu NAKAZIA

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Nafungua code TCRA na jeshi la Polisi Tanzania lifanyieni Kazi haraka ili kukomesha tabia ya wizi/utapeli kupitia simu.

Asalam alaykum Jammiya, Bwana Yesu asifiwe watumishi wa mungu hakika Kristo ni Tumaini letu sote Mimi na mwenzangu Cute Wife ni wazima wa afya...
Hio ni moja lakini usha jiuliza kwa nini kuwa track ni ngumu sana? Akili zao zipo kwenye TCRA na Police kushindwa kuwa track na kuna sababu nahisi nisha wahi iweka humu niliambiwa na Jamaa angu askari
 
Hapana hii mbona rahisi kustuka coz Kuna *106#kujua kama nida yako imesajili namba ngapi?

Hilo pia ni kulifanya dk 0 pia usubiri tcra na police wakufanyie?

Hapana watanzania tuna ujinga mwingi na kupuuza mambo.

Hao matapeli Wana namna zao za kupata hizo laini na pia huko wanapo pata laini ndio wanatoa hizo namba za watu wanao watumia hizo sms

Zoezi la kurasimisha namba tu ilikuwa ni shughuli kwa Watanzania

Mtu anarasimisha siku ya mwisho na wengine hawajarasimisha kabisa Hadi namba zimefingiwa

Hapo pia utawakaumu tcra?
 
Technology yetu ipo chini mbona hizi mambo SA hakuna ukifanya hicho kitu wanakudaka kabla hujatoa Line kwenye mambo wako kwanza line zote zinasoma zilizopo zikiwa kwenye kifaa chochote hawa wahuni wanatumia Line moja siku nzima na muda mwingine wanawatumia hadi wakamataji harafu hakuna madhara yeyote hapo utamlaumu nani?
 
Back
Top Bottom