Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,034
- 144,388
Mbinafsi na msaliti mkubwa wee!Maendeleo ni mabadiliko. Kujenga miundombinu ya kila aina ni sehemu ya maendeleo. Kujenga viwanja vya ndege nchini kunaongeza miundombinu ya usafiri wa anga. get up with positive thinking guys.
Uwanja wa ndege wa Chato siyo mali ninafsi ya JPM, ni mali ya umma kama ilivyo kwa viwanja vya ndege vingine. Tafsiri ya maendeleo ya kujenga airport ya Chato ni kuongeza idadi ya airports tulizonazo nchini.
Ni kutoangalia mbele ku-personalize ujenzi wa Chato Airport na maslahi binafsi, na hata ku-launch personal attack dhidi ya JPM. In the next nine years JPM will have gone out of state house but the airport will remain. Mara zote huwa kuna mtu maarufu na sababu mahsusi kuwezasha miji na miundombinu yake kujengwa. Kinachotakiwa kufahamika ni kuwa Tanzania is not static. Kuna decent enterprising people, and possibly later, kutakuwa na class or community of enterprising practices itakayokuja kutumia fursa za infrastructure zilizokwisha jengwa kufanya maamuzi ya uwekezaji mkubwa (mega investments).
Miaka 150 iliyopita Nairobi haikuwa kama ilivyo leo. Miaka 150 iliyopita Dar es salaam ilipojengwa na Sayyid Majid haikuwa kama hii ya leo. Wala miaka miaka 126 Emini Pasha alivyoanzisha miji ya Bukoba na Mwanza hakuna aliyejua michango ya miji hiyo katika uchumi wa taifa kama tunavyoshuhudia leo. Maendeleo ni mnyororo huanza na pingili ya kwanza nyingine huongezeka.
Ninawashauri wenye mawazo binafsi kuyaondoa vichwani mwao na badala yake wafikiri faida za mandeleo yatakayotoka na taifa kuwa na viwanja vya ndege vingi vya kutosha, takriban kila wilaya - ma vivyo hivyo usafiri wa anga wa kumwaga. Hali iko hivyo katika nchi zilizoendelea. Wacha Chato airport ijengwa, na pengine ijengwe bandari kwenye ufukwe wa ziwa Nyanza pia, kuwepo na mahoteli makubwa, biashara ya dhahabu ifanyike hapo badala ya kusafirisha madini hayo kwenda Sydney, Brussels, London au Cape Town. What is wrong kukiwa na Chato City? Hi! think development, think positive guys.