Kwa ujenzi huu wa Uwanja wa ndege Chato, Rais Magufuli anatukatisha tamaa "watu wake"

bad,bad ever ...!,kwa nini asingeuimarisha UWANJA wa mwanza kwa 100%,au kabisa kuufanya wa kimataifa...ukaudumia na Serengeti.../ madege makubwa ya kitalii yakaweza kutua mwanza.
Kwa akili zangu ndogo sana
atakapomaliza mda wake na
ndio utakuwa mwisho wa
uhai UWANJA huo,
•HIVI HAKUNA WASHAURI
WA MAMBO YA AINA HII./
ILI KUTUOKOA NA HASARA
ZISIZO ZA LAZIMA?
Inauma sana
 
Aiseee mkuu nimesoma huwezi amini kila paragraph moja inanitia simanzi
Kweli charity begins at home,ule usemi wa nabii hakubaliki kwao this time jamaa anaubadili utakuwa nabii anakubalika kwao.
Sio kila kitu ukifanya kwenu utaheshimika.Mimi nadhani watu wa chato wana mahitaji mengi ya muhimu kama Huduma bora za afya na elimu.Hicho kiwanja anachojenga chato hata wanachato hakitawasaidia.
 
Maendeleo ni mabadiliko. Kujenga miundombinu ya kila aina ni sehemu ya maendeleo. Kujenga viwanja vya ndege nchini kunaongeza miundombinu ya usafiri wa anga. get up with positive thinking guys.

Uwanja wa ndege wa Chato siyo mali ninafsi ya JPM, ni mali ya umma kama ilivyo kwa viwanja vya ndege vingine. Tafsiri ya maendeleo ya kujenga airport ya Chato ni kuongeza idadi ya airports tulizonazo nchini.

Ni kutoangalia mbele ku-personalize ujenzi wa Chato Airport na maslahi binafsi, na hata ku-launch personal attack dhidi ya JPM. In the next nine years JPM will have gone out of state house but the airport will remain. Mara zote huwa kuna mtu maarufu na sababu mahsusi kuwezasha miji na miundombinu yake kujengwa. Kinachotakiwa kufahamika ni kuwa Tanzania is not static. Kuna decent enterprising people, and possibly later, kutakuwa na class or community of enterprising practices itakayokuja kutumia fursa za infrastructure zilizokwisha jengwa kufanya maamuzi ya uwekezaji mkubwa (mega investments).

Miaka 150 iliyopita Nairobi haikuwa kama ilivyo leo. Miaka 150 iliyopita Dar es salaam ilipojengwa na Sayyid Majid haikuwa kama hii ya leo. Wala miaka miaka 126 Emini Pasha alivyoanzisha miji ya Bukoba na Mwanza hakuna aliyejua michango ya miji hiyo katika uchumi wa taifa kama tunavyoshuhudia leo. Maendeleo ni mnyororo huanza na pingili ya kwanza nyingine huongezeka.

Ninawashauri wenye mawazo binafsi kuyaondoa vichwani mwao na badala yake wafikiri faida za mandeleo yatakayotoka na taifa kuwa na viwanja vya ndege vingi vya kutosha, takriban kila wilaya - ma vivyo hivyo usafiri wa anga wa kumwaga. Hali iko hivyo katika nchi zilizoendelea. Wacha Chato airport ijengwa, na pengine ijengwe bandari kwenye ufukwe wa ziwa Nyanza pia, kuwepo na mahoteli makubwa, biashara ya dhahabu ifanyike hapo badala ya kusafirisha madini hayo kwenda Sydney, Brussels, London au Cape Town. What is wrong kukiwa na Chato City? Hi! think development, think positive guys.
 
Hoja nzuri ila siasa nyingi.Maswali haya mazuri yaalipaswa pia kuulizwa kipindi kilichopita, akili ipi ilitumika kujenga uwanja wa Arusha ilihali KIA ipo,busara ipi ilitumika kupeleka lami Rombo wakati kuna mikoa lami walikuwa wanaisikia wanaisikia redioni.

Kwa nini kipindi hicho ilikuwa busara kupunguza kasi ya ujenzi wa uwanja wa Songwe na kuimarisha uwanja wa Arusha.

Kama kuna kaundi kadogo kanaona ni busara kwao kupeleka kila kitu kwao kwa fedha za nchi na wengine huyafanya hayohayo.Kama ni vibaya kufanya na JPM tuwaseme na wengine waliofanya kama haya.

Ni jambo lisilozingatia vipaumbele ila nami ningekuwa na nafasi kama ya JPM ningefanya hivyo hovyo.Nani kati yetu angetawanya nguvu na akili zake kwa watu wanaoamini kuwa wao ni daraja la kwanza hawastahili kuongozwa na yeyote asiyetoka kwao.

Tunatakiwa kuwa na viongozi aina ya Nyerere nchi kwanza wewe na ya kwenu baadaye ila hatutakiwi kuwa wanafiki.Uchaguzi unapokuja lazima uwe na majibu kwa waliokubeba na kuwaonyesha madhara ya kung'ang'ania ukanda au ukabila kama kipimo cha uongozi.Nani kati yetu angependa kukataliwa hata na wa kwao? Ukitumia nguvu ya fedha za matajiri tusiojua wamezipataje fedha zao kwanini wengine wasitumie njia tofauti kufuta mbinu zako.Tuache kulea ukanda tujenge Tanzania.

Nimetoa mifano hiyo kwa makusudi maana mada inaonyesha kasoro zinazofanana na hizo zisizo gusa kanda moja.
Unaujua uwanja wa Arusha au unaandika tu bila kuelewa?
 
Mwanzoni niliposikia ujenzi wa Uwanja wa ndege Chato,basi nilidhani wameamua kumtengenezea mzee walau "Airstrip" tu ili iwe rahisi kwake kufika mpaka kijijini kwake kwa njia ya anga,kuepusha safari ndefu ya Dsm-Chato au Mwanza-Chato.Na kwa sasa uwanja huo unaendelea kujengwa kwa kasi kubwa.

Lakini kumbe si "Airstrip" tena,bali ni "Airport",maana huwezi kuwa na Airstrip yenye runway 3000M(urefu) na 45M (Upana)..huu ni uwanja kabisa,na ndio maana hata tangazo la Tender limesema "New Airport"....So this is another coming Airport in lake Zone.

Kuwa na Runway ya urefu wa mita 3000 si kitoto,maanake hii ni eneo la mruko lenye urefu wa km3,na upana wa mita 45.....Waoooooh!!!another "International Airport" to come.

Uwanja wa ndege wa Dsm una runway mbili moja kubwa nafikiri ni km 3 (3000M) kwa urefu plus mita kadhaa za threshold na upana ni mita 46,wakati ile ya hapo Dsm ndogo inayotumika mchana tu na kwa ndege ndogo ni km 1 (1000M) urefu na upana wa mita 30...

Sasa utaona Runway ya Chato kwa urefu inalingana na hii ya uwanja wa Dar na upana wa Dsm umezidi kwa mita moja ule wa Chato.

Hapo inapaswa tujuwe "Pavement Identification number",tufahamu "strength of runway" ya Chato itakuwa na uwezo wa kuchukuwa ndege za uzito gani,lakini kwa urefu huu tu,maanake sasa Chato inaenda kupokea ndege zenye ukubwa wa Boeing738,B733,B737 na Airbus 320 na A319 ambazo toka Uhuru hazijawahi kutuwa Iringa,Songea,Kigoma,Tabora,Musoma na Tanga;ambayo ndio miji mikubwa ktk nchi yetu

Niliwahi kutuwa kwenye Uwanja wa Geita pale Mchauru(?),huu una hata Location Indicator ya ICAO na unafahamika kama HTRU,hawa wana hata "Control Tower",kutoka Geita pale Mgodini hadi Chato ni kama km 100 na ushee.Sijajuwa kwanini wanapeleka uwanja mkubwa hivi Chato,sidhani baada ya mkuu JPM kutoka madarakani uwanja huu utatumika kibiashara.

Hili lilitokea kwa Mizengo Pinda,alijenga Mpanda uwanja mzuri sana na wenye Tarmac nzuri sana...Lkn baada ya kutoka yeye umebaki malisho ya ng'ombe na mbuzi wa Mpanda.Na kwa sasa una hadhi ya "Airstrip" sababu hauna hata Control Tower,hakuna ndege za kibiashara zinazokwenda huko.Kampuni ya Auric Air ilikuwa na safari zake Mpanda,lakini sasa wamesitisha karibu mwaka na ushee.Ulijengwa kwa bilions of money.This was one of the "White Elephant" projects of our time.

Ukiutazama uwanja ule wa Mpanda,unajisemea tu kuwa viwanja hivi vingekuwa vinabebeka,basi ule kwa uzuri wa Runway yake na Apron,na aina ile ya lami,basi tungeubeba na kuupeleka eneo lenye movements nyingi ya ndege za kibiashara na kuutoa kule palipodorora.

Bagamoyo alitengeneza "HELIPORT" na akawa anaitumia kila mwisho wa week akienda nyumbani kupumzika,aliitengeneza pale Msoga kijijini kwake.Naona kila mtu anatazama nyumbani kila akipata madaraka.Wanasema "Charity begins at home"....Mkapa aliwapa Daraja,JK kawapelekea EPZ,bandari na heliport.Pinda aliwapelekea uwanja wa ndege ambao hautumiki.Kwa hiyo si ajabu kwa JPM kupeleka uwanja nyumbani.

Kabla ya JK kulikuwa hakuna "HELIPORT" Msoga....Lkn yeye amepeleka na hata siku anaaga Ikulu,alipelekwa Kijijini Msoga na chopa ya kukodishwa ya kampuni ya Everrest ya Kenya inayofanya kazi Tanzania.Mtu kwao,mkataa kwao mtumwa...

Naogopa pia uwanja wa Chato usijekuwa malisho ya mbuzi,ingetosha huko Mkuu tungemtengenezea tu HELIPORT ili awe anapelekwa na Chopa,maana jeshi letu lina chopa mpya,Uwanja unajengwa CHATO unakuwa na Runway (3000m to 45m)....Hii sawa na KIA na Julius Nyerere International Airport.Huku ni kujipendekeza au nini???

Ni ukweli Rais anahitaji usafiri wa anga aendapo likizo au mapumziko nyumbani,lkn si kwa kujenga Airport Chato.Hivi kweli Chato unajenga Runway yenye "Bitumen Standards".

Kuna viwanja tunapaswa kuviboresha maana vina movements nyingi za ndege,Uwanja kama Songea umechakaa na kila siku kuna ndege moja ya abiria inakwenda,Uwanja wa Iringa huu ni km2.1 na una movements karibu mbili kwa siku,uwanja wa Kigoma ambao hata ndege za wakimbizi na UN hutuwa,japo wao kwa kusaidiana na UNHCR wamejenga uwanja Kasuru.

Safari ya kwanza ya Mandela kuja Tanzania kuonana na Mwalimu alitua uwanja wa ndege wa Mbeya.Mbeya ilikuwa katika Ramani kubwa kwa ajili ya kusaidia harakati za Kusini mwa Afrika na ilitumika pia wakati wa vita ya kwanza na ya pili ya dunia.Siku CEO wa Air Zimbabwe anazindua route mpya ya -Harare-Dsm-Harare,alisikika akisema kwa mara ya kwanza Air Zimbabwe kuja Tanganyika ilikuwa mwaka 1946(Wakati huo wa Southern Rhodesia),viwanja ilivyokuwa inatuwa ni Mbeya na Tabora.

Hivyo uwanja kama wa Mbeya(Songwe) ndege hazitui usiku eti hauna taa za sehemu ya kutua na kurukia ndege, uwanja huo ulitakiwa kujengwa miaka mingi,ulitakiwa kutumika kama "Refueling Point" kwa ndege zinazosafiri toka Kaskazini kwenda Kusini mwa Afrika/dunia au kinyume chake.Siasa za Tanzania na vipaumbele vinavyobadilikabadilika ndio vikatufikisha hapa.

Hii ya Airport ya Chato,inaweza kuwa na "watetezi" wake,lakini haiondoi haki ya wengine kuhoji umuhimu wa kiwanja kikubwa kiasi hiki kwenye eneo ambalo baada ya mtu kutoka madarakani,haiwezi kuwa na "umuhimu" wa matumizi kama ilivyo sasa.Hii inawapa "wakosoaji" wakati mzuri na "watetezi" wa Rais wakati mgumu.Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Kuhoji kwetu,si hujuma na shutuma kwa aliye na mamlaka,bali ni tabia ya binadamu kuuliza kile anachoona kinampa utata.
Are you questioning the authority?
 
barafu mkuu, nilifuatilia sana kampeni za mheshimiwa bwana rais daktari lakini sikuwahi kusikia hata siku moja akiweka ujenzi wa kiwanja cha ndege Chato kwenye manifesto zake. Huu ni uamuzi wa ule mhimili uliojikita Zaidi ya mihimili mingine.
Huu ni mwanzo tu, kitakachofuata atajimegea mabilioni na kwenda kuwekeza na kuficha nje ya nchi kama walivyofanya akina Mobutu au Ghadafi na hakuna mtu atatia neno kwa vile kila atakayeropoka ni jela.

Historia ya dunia iko wazi kabisa hakuna kiongozi aliyenyamazisha watu kwa Kuminya uhuru wa habari ambaye hakufanya ufisadi, fuatilieni kuanzia Rwanda kwa Kagame ana mabilioni kibao kajimegea.

Sasa hivi tunalialia uwanja wa Chato makubwa na ya kuudhi zaidi yanakuja, sio ndani ya chama chake, upinzani au serikalini hakuna wa kumkosoa au kumzuia
 
LUSOMYA
Inaonekana hujaelewa kitu hapa.
Kwanini Uwanja ujengwe kijijini Chato na sio Geita mjini? Chato kuna ni nini?
Kuna haja gani kuwa na uwanja mkubwa, wakisasa na wa gharama hivyo katika kijiji cha Chato?
Upi uhusiano wa Dhahabu na uwanja mkubwa wa ndege?

Mererani kuna Tanzanite, Mwadui kuna Almasi, Nzega kuna Dhahabu, Bulyakuru kuna Dhahabu, Singida Vijijini kuna dhahabu nk. Kote huko hakuna viwanja vya ndege vilivyojengwa na Serikali.
Mkuu hawa vijana huwa haelewi. Unaweza toa mifano harisia lakin bado asilewe kitu as if yeye ameapa kukutetea uovu wa mtu wake
 
Mwanzoni niliposikia ujenzi wa Uwanja wa ndege Chato,basi nilidhani wameamua kumtengenezea mzee walau "Airstrip" tu ili iwe rahisi kwake kufika mpaka kijijini kwake kwa njia ya anga,kuepusha safari ndefu ya Dsm-Chato au Mwanza-Chato.Na kwa sasa uwanja huo unaendelea kujengwa kwa kasi kubwa.

Lakini kumbe si "Airstrip" tena,bali ni "Airport",maana huwezi kuwa na Airstrip yenye runway 3000M(urefu) na 45M (Upana)..huu ni uwanja kabisa,na ndio maana hata tangazo la Tender limesema "New Airport"....So this is another coming Airport in lake Zone.

Kuwa na Runway ya urefu wa mita 3000 si kitoto,maanake hii ni eneo la mruko lenye urefu wa km3,na upana wa mita 45.....Waoooooh!!!another "International Airport" to come.

Uwanja wa ndege wa Dsm una runway mbili moja kubwa nafikiri ni km 3 (3000M) kwa urefu plus mita kadhaa za threshold na upana ni mita 46,wakati ile ya hapo Dsm ndogo inayotumika mchana tu na kwa ndege ndogo ni km 1 (1000M) urefu na upana wa mita 30...

Sasa utaona Runway ya Chato kwa urefu inalingana na hii ya uwanja wa Dar na upana wa Dsm umezidi kwa mita moja ule wa Chato.

Hapo inapaswa tujuwe "Pavement Identification number",tufahamu "strength of runway" ya Chato itakuwa na uwezo wa kuchukuwa ndege za uzito gani,lakini kwa urefu huu tu,maanake sasa Chato inaenda kupokea ndege zenye ukubwa wa Boeing738,B733,B737 na Airbus 320 na A319 ambazo toka Uhuru hazijawahi kutuwa Iringa,Songea,Kigoma,Tabora,Musoma na Tanga;ambayo ndio miji mikubwa ktk nchi yetu

Niliwahi kutuwa kwenye Uwanja wa Geita pale Mchauru(?),huu una hata Location Indicator ya ICAO na unafahamika kama HTRU,hawa wana hata "Control Tower",kutoka Geita pale Mgodini hadi Chato ni kama km 100 na ushee.Sijajuwa kwanini wanapeleka uwanja mkubwa hivi Chato,sidhani baada ya mkuu JPM kutoka madarakani uwanja huu utatumika kibiashara.

Hili lilitokea kwa Mizengo Pinda,alijenga Mpanda uwanja mzuri sana na wenye Tarmac nzuri sana...Lkn baada ya kutoka yeye umebaki malisho ya ng'ombe na mbuzi wa Mpanda.Na kwa sasa una hadhi ya "Airstrip" sababu hauna hata Control Tower,hakuna ndege za kibiashara zinazokwenda huko.Kampuni ya Auric Air ilikuwa na safari zake Mpanda,lakini sasa wamesitisha karibu mwaka na ushee.Ulijengwa kwa bilions of money.This was one of the "White Elephant" projects of our time.

Ukiutazama uwanja ule wa Mpanda,unajisemea tu kuwa viwanja hivi vingekuwa vinabebeka,basi ule kwa uzuri wa Runway yake na Apron,na aina ile ya lami,basi tungeubeba na kuupeleka eneo lenye movements nyingi ya ndege za kibiashara na kuutoa kule palipodorora.

Bagamoyo alitengeneza "HELIPORT" na akawa anaitumia kila mwisho wa week akienda nyumbani kupumzika,aliitengeneza pale Msoga kijijini kwake.Naona kila mtu anatazama nyumbani kila akipata madaraka.Wanasema "Charity begins at home"....Mkapa aliwapa Daraja,JK kawapelekea EPZ,bandari na heliport.Pinda aliwapelekea uwanja wa ndege ambao hautumiki.Kwa hiyo si ajabu kwa JPM kupeleka uwanja nyumbani.

Kabla ya JK kulikuwa hakuna "HELIPORT" Msoga....Lkn yeye amepeleka na hata siku anaaga Ikulu,alipelekwa Kijijini Msoga na chopa ya kukodishwa ya kampuni ya Everrest ya Kenya inayofanya kazi Tanzania.Mtu kwao,mkataa kwao mtumwa...

Naogopa pia uwanja wa Chato usijekuwa malisho ya mbuzi,ingetosha huko Mkuu tungemtengenezea tu HELIPORT ili awe anapelekwa na Chopa,maana jeshi letu lina chopa mpya,Uwanja unajengwa CHATO unakuwa na Runway (3000m to 45m)....Hii sawa na KIA na Julius Nyerere International Airport.Huku ni kujipendekeza au nini???

Ni ukweli Rais anahitaji usafiri wa anga aendapo likizo au mapumziko nyumbani,lkn si kwa kujenga Airport Chato.Hivi kweli Chato unajenga Runway yenye "Bitumen Standards".

Kuna viwanja tunapaswa kuviboresha maana vina movements nyingi za ndege,Uwanja kama Songea umechakaa na kila siku kuna ndege moja ya abiria inakwenda,Uwanja wa Iringa huu ni km2.1 na una movements karibu mbili kwa siku,uwanja wa Kigoma ambao hata ndege za wakimbizi na UN hutuwa,japo wao kwa kusaidiana na UNHCR wamejenga uwanja Kasuru.

Safari ya kwanza ya Mandela kuja Tanzania kuonana na Mwalimu alitua uwanja wa ndege wa Mbeya.Mbeya ilikuwa katika Ramani kubwa kwa ajili ya kusaidia harakati za Kusini mwa Afrika na ilitumika pia wakati wa vita ya kwanza na ya pili ya dunia.Siku CEO wa Air Zimbabwe anazindua route mpya ya -Harare-Dsm-Harare,alisikika akisema kwa mara ya kwanza Air Zimbabwe kuja Tanganyika ilikuwa mwaka 1946(Wakati huo wa Southern Rhodesia),viwanja ilivyokuwa inatuwa ni Mbeya na Tabora.

Hivyo uwanja kama wa Mbeya(Songwe) ndege hazitui usiku eti hauna taa za sehemu ya kutua na kurukia ndege, uwanja huo ulitakiwa kujengwa miaka mingi,ulitakiwa kutumika kama "Refueling Point" kwa ndege zinazosafiri toka Kaskazini kwenda Kusini mwa Afrika/dunia au kinyume chake.Siasa za Tanzania na vipaumbele vinavyobadilikabadilika ndio vikatufikisha hapa.

Hii ya Airport ya Chato,inaweza kuwa na "watetezi" wake,lakini haiondoi haki ya wengine kuhoji umuhimu wa kiwanja kikubwa kiasi hiki kwenye eneo ambalo baada ya mtu kutoka madarakani,haiwezi kuwa na "umuhimu" wa matumizi kama ilivyo sasa.Hii inawapa "wakosoaji" wakati mzuri na "watetezi" wa Rais wakati mgumu.Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Kuhoji kwetu,si hujuma na shutuma kwa aliye na mamlaka,bali ni tabia ya binadamu kuuliza kile anachoona kinampa utata.
Alitanguliza traffic lights pale chato, hapo huitaji maelezo mengi kumjua ni mtu wa aina gani
 
Rasilimali za kanda ya ziwa hazikuinufaisha kanda hii. Kila kitu kilipelekwa kaskazini. Sasa huu ni wakati wa kanda ya ziwa kunufaika .
Kama wew ni wakanda ya ziwa na unahoji hivi pole..
Bado kuna watu wamekusaidia jinsi ya kuhoji ili hoja zako ziendane kikanda kama unavyotaka lakini bado empty.
 
Baada ya miaka 23 ya utawala, Mwalimu alijengewa nyumba Butiama kwa heshima aliyopewa na wananchi, huu mwaka mmoja wa utawala Chato inakimbiza Geneva.
Mwl Nyerere alipokuwa anakabidhiwa hiyo nyumba, aliishangaa nyumba ilivyo kubwa, mpaka akawauliza humu ndani ataishi tembo maana aliishangaa kuona anajengewa nyumba kubwa hivyo
 
Hoja nzuri ila siasa nyingi.Maswali haya mazuri yaalipaswa pia kuulizwa kipindi kilichopita, akili ipi ilitumika kujenga uwanja wa Arusha ilihali KIA ipo,busara ipi ilitumika kupeleka lami Rombo wakati kuna mikoa lami walikuwa wanaisikia wanaisikia redioni.

Kwa nini kipindi hicho ilikuwa busara kupunguza kasi ya ujenzi wa uwanja wa Songwe na kuimarisha uwanja wa Arusha.

Kama kuna kaundi kadogo kanaona ni busara kwao kupeleka kila kitu kwao kwa fedha za nchi na wengine huyafanya hayohayo.Kama ni vibaya kufanya na JPM tuwaseme na wengine waliofanya kama haya.

Ni jambo lisilozingatia vipaumbele ila nami ningekuwa na nafasi kama ya JPM ningefanya hivyo hovyo.Nani kati yetu angetawanya nguvu na akili zake kwa watu wanaoamini kuwa wao ni daraja la kwanza hawastahili kuongozwa na yeyote asiyetoka kwao.

Tunatakiwa kuwa na viongozi aina ya Nyerere nchi kwanza wewe na ya kwenu baadaye ila hatutakiwi kuwa wanafiki.Uchaguzi unapokuja lazima uwe na majibu kwa waliokubeba na kuwaonyesha madhara ya kung'ang'ania ukanda au ukabila kama kipimo cha uongozi.Nani kati yetu angependa kukataliwa hata na wa kwao? Ukitumia nguvu ya fedha za matajiri tusiojua wamezipataje fedha zao kwanini wengine wasitumie njia tofauti kufuta mbinu zako.Tuache kulea ukanda tujenge Tanzania.

Nimetoa mifano hiyo kwa makusudi maana mada inaonyesha kasoro zinazofanana na hizo zisizo gusa kanda moja.
Shule za kata zimeua kabisa vipaji vya watanzania, wewe ni tunda la elimu ya kata na sidhani kama umewahi kupanda ndege maishani kwako.

Ngoja nikupe elimu bure we mbulumundu mkosa uelewa:

Ukiacha Dar, uwanja unaofuatia kwa kuwa na ndege nyingi binafsi ni uwanja wa Arusha, kwa vile wewe maskini huwezi kuhakiki hilo hauna nauli. Uwanja wa ndege wa Arusha at any time kuna ndege binafsi 30 zimepaki, ni wa pili kutoka uwanja wa Dar. Hakuna uwanja mwingine Tanzania wenye ndege nyingi kati ya hivyo viwili.

Kule Chato tajiri ni Magufuli peke yake na ndio atakuwa mtanzania wa kwanza kutoka mkoa huo kumiliki ndege binafsi. Arusha walipelekewa uwanja kwa kuwa ndege wanazo, uwanja wa ndege sio sawa na uwanja wa mpira kila mwenye miguu anacheza, unahitaji kuwa na ndege na Arusha wanazo za kwao binafsi ndio maana walipelekewa uwanja.

Mapimbi kama nyie mnaoona uwanja wa ndege ni anasa na bahati mbaya mmepewa nafasi za upendeleo serikalini ndio mnafanya nchi hii kuwa maskini hadi mwisho wa dunia
 
Back
Top Bottom