Kwa Ujenzi huu, Jiji la Dodoma litachoka mapema sana

Mnyamahodzo

JF-Expert Member
May 23, 2008
1,932
985
Ujenzi wa majiji ya Dar es salaam, Tanga na Mwanza unahistoria ndefu sana. Yalijengwa polepole mwaka kwa mwaka. Lakini lililo la muhimu zaidi ni ubora wa vifaa vya ujenzi vilivyotumika.

Majengo ya zamani kabisa katika Majiji ya Tanga na D'salaam yalijengwa kwa mawe na matumbawe na mengine kwa tofali za kuchoma huku nguzo na migamba ikiwa ni ya mikoko na mivinje iliyokomaa hasa.

Ulipokuja ujenzi wa kutumia tofali za simenti (blocks), tofali zake zilikuwa ni imara sana kutokana na aina ya sementi, kiasi cha mchanganyo wa sementi na mchanga na pia idadi ya siku tofali lilizolazwa katika maji. Majengo ya maghorofa yalijengwa kwa tofali bora pamoja na yale ya kawaida (ofisi na nyumba za viongozi).

Watu binafsi nao walipenda kuwa na tofali bora kama za MECCO au TACONA. Baada ya kipindi kigumu cha kiuchumi ndipo wananchi wakaanza kuchakachua vipimo vya sementi: mchanga na utiaji wa maji.

Ukiingia Tanga, Mwanza na Dar utaona majengo ya toka 1950 hadi 2000 yaliyo katika ubora wake.

Ninachokiona kwasasa Jiji Dodoma majengo mengi kujengwa kwa pupa. Tofali zinazotumika ni za ubora wa chini..hakuna kampuni rasmi yenye kuzalisha tofali bora. Nyingi ya tofali ukinyanyua usawa wa kiuno na kudondosha zinavunjika; ukisugua kwa kijiti zinapukutika upesi. Ni tofali zenye mchanganyiko mmbovu wa mchanga na sementi. Ni tofali zisizokunywa maji ya kutosha.

Majemgo mengi misingi yake ni mifupi bila kuzingatia kuwa mwamba wa maji (water table) wa Dodoma hauko chino sana. Matokeo yake, mwaka mmoja toka jengo lisimame utaona msingi unaanza kumong'ong'onyoka na sakafuyingi kutoa sauti tofauti tofauti unapokanyaga juu yake.

Kama TBA na Halmashauri ya Jiji la Dodoma hawatachukua njia za makusudi katika kudhibiti uzaloshajina utumiaji wa vifaa vya ujenzi vyenye ubora wa chini, iko hatari hatari hata maghorofa yanayojengwa sasa baada ya miaka miwili kuwa na nyufa na mengine kutakiwa kuvunjwa baada ya miaka 10 hivi.

Nawasilisha.

Kwa kuandika hivi haimaanishi katika kipindi cha miaka ya karibuni hakuna kabisa majengo yaliyojengwa kwa viwango.
 
Ujenzi wa majiji ya Dar es salaam, Tanga na Mwanza unahistoria ndefu sana. Yalijengwa polepole mwaka kwa mwaka. Lakini lililo la muhimu zaidi ni ubora wa vifaa vya ujenzi vilivyotumika.

Majengo ya zamani kabisa katika Majiji ya Tanga na D'salaam yalijengwa kwa mawe na matumbawe na mengine kwa tofali za kuchoma huku nguzo na migamba ikiwa ni ya mikoko na mivinje iliyokomaa hasa.

Ulipokuja ujenzi wa kutumia tofali za simenti (blocks), tofali zake zilikuwa ni imara sana kutokana na aina ya sementi, kiasi cha mchanganyo wa sementi na mchanga na pia idadi ya siku tofali lilizolazwa katika maji. Majengo ya maghorofa yalijengwa kwa tofali bora pamoja na yale ya kawaida (ofisi na nyumba za viongozi).

Watu binafsi nao walipenda kuwa na tofali bora kama za MECCO au TACONA. Baada ya kipindi kigumu cha kiuchumi ndipo wananchi wakaanza kuchakachua vipimo vya sementi: mchanga na utiaji wa maji.

Ukiingia Tanga, Mwanza na Dar utaona majengo ya toka 1950 hadi 2000 yaliyo katika ubora wake.

Ninachokiona kwasasa Jiji Dodoma majengo mengi kujengwa kwa pupa. Tofali zinazotumika ni za ubora wa chini..hakuna kampuni rasmi yenye kuzalisha tofali bora. Nyingi ya tofali ukinyanyua usawa wa kiuno na kudondosha zinavunjika; ukisugua kwa kijiti zinapukutika upesi. Ni tofali zenye mchanganyiko mmbovu wa mchanga na sementi. Ni tofali zisizokunywa maji ya kutosha.

Majemgo mengi misingi yake ni mifupi bila kuzingatia kuwa mwamba wa maji (water table) wa Dodoma hauko chino sana. Matokeo yake, mwaka mmoja toka jengo lisimame utaona msingi unaanza kumong'ong'onyoka na sakafuyingi kutoa sauti tofauti tofauti unapokanyaga juu yake.

Kama TBA na Halmashauri ya Jiji la Dodoma hawatachukua njia za makusudi katika kudhibiti uzaloshajina utumiaji wa vifaa vya ujenzi vyenye ubora wa chini, iko hatari hatari hata maghorofa yanayojengwa sasa baada ya miaka miwili kuwa na nyufa na mengine kutakiwa kuvunjwa baada ya miaka 10 hivi.

Nawasilisha.
Thanks, very technical observation.
P
 
Ujenzi wa majiji ya Dar es salaam, Tanga na Mwanza unahistoria ndefu sana. Yalijengwa polepole mwaka kwa mwaka. Lakini lililo la muhimu zaidi ni ubora wa vifaa vya ujenzi vilivyotumika.

Majengo ya zamani kabisa katika Majiji ya Tanga na D'salaam yalijengwa kwa mawe na matumbawe na mengine kwa tofali za kuchoma huku nguzo na migamba ikiwa ni ya mikoko na mivinje iliyokomaa hasa.

Ulipokuja ujenzi wa kutumia tofali za simenti (blocks), tofali zake zilikuwa ni imara sana kutokana na aina ya sementi, kiasi cha mchanganyo wa sementi na mchanga na pia idadi ya siku tofali lilizolazwa katika maji. Majengo ya maghorofa yalijengwa kwa tofali bora pamoja na yale ya kawaida (ofisi na nyumba za viongozi).

Watu binafsi nao walipenda kuwa na tofali bora kama za MECCO au TACONA. Baada ya kipindi kigumu cha kiuchumi ndipo wananchi wakaanza kuchakachua vipimo vya sementi: mchanga na utiaji wa maji.

Ukiingia Tanga, Mwanza na Dar utaona majengo ya toka 1950 hadi 2000 yaliyo katika ubora wake.

Ninachokiona kwasasa Jiji Dodoma majengo mengi kujengwa kwa pupa. Tofali zinazotumika ni za ubora wa chini..hakuna kampuni rasmi yenye kuzalisha tofali bora. Nyingi ya tofali ukinyanyua usawa wa kiuno na kudondosha zinavunjika; ukisugua kwa kijiti zinapukutika upesi. Ni tofali zenye mchanganyiko mmbovu wa mchanga na sementi. Ni tofali zisizokunywa maji ya kutosha.

Majemgo mengi misingi yake ni mifupi bila kuzingatia kuwa mwamba wa maji (water table) wa Dodoma hauko chino sana. Matokeo yake, mwaka mmoja toka jengo lisimame utaona msingi unaanza kumong'ong'onyoka na sakafuyingi kutoa sauti tofauti tofauti unapokanyaga juu yake.

Kama TBA na Halmashauri ya Jiji la Dodoma hawatachukua njia za makusudi katika kudhibiti uzaloshajina utumiaji wa vifaa vya ujenzi vyenye ubora wa chini, iko hatari hatari hata maghorofa yanayojengwa sasa baada ya miaka miwili kuwa na nyufa na mengine kutakiwa kuvunjwa baada ya miaka 10 hivi.

Nawasilisha.
Lakini ujenzi si unasu
imamiwa na mainjinia?

Na kwanini serikali yenye ujenzi wa majengo mengi tena kwa muda mrefu siwe na kampuni yake au kutoa tenda kwa constructions kampanies ili zifyatue tofali zenye ubor na standards zilizo sawa??

Baadabya 10 to 20 yrs tutashusha bendera nusu mlingoti kwa hawa watani zangu wagogo.
 
Tofali zile ambazo National Housing ya wakati ule ilitumia kujengea majengo yake zilikuwa zinapakiwa katika malori ya Isuzu yale tani 7. Lori lilikuwa linabeba hadi eneo la ujenzi na kisha kumwaga kama unavyomwagwa mchanga. Hukuti tofali imevunjika wala kugengeneza ufa. Tofali zilitengenezwa na MECCO au TACONA kabla ya zile za Kisarawe Bricks Factory.

Lakini leo, jaribu kumwaga tofali za ujenzi zinazozalishwa Dom na viunga vyake, ka.a hujaambulia vipisi na vumbi.
 
Kama TBA na Halmashauri ya Jiji la Dodoma hawatachukua njia za makusudi katika kudhibiti uzaloshajina utumiaji wa vifaa vya ujenzi vyenye ubora wa chini, iko hatari hatari hata maghorofa yanayojengwa sasa baada ya miaka miwili kuwa na nyufa na mengine kutakiwa kuvunjwa baada ya miaka 10 hivi.

Katika ujenzi wa mji mpya wa Dodoma tunapoteza fursa nyingi, mbali ya hivyo viwango vya ujenzi ulivyozungumzia.
Ujenzi huu ulikuwa ni nafasi nzuri sana ya kujenga mji wa kisasa kabisa, na hasa ukizingatia teknologia zilizopo sasa hivi.

Dodoma ilitakiwa isiwe ya kutegemea nishati ya umeme wa gridi pekee kwa kila matumizi. Mji una jua linalowaka takribani mwaka mzima, kwa nini majengo yake yasijengwe yakiwa na uwezo wa kuitumia nishati hiyo ya jua kwa sehemu kubwa?

Majengo yanayojengwa, kwa nini ujenzi wake usiwe wa kuzingatia matumizi bora ya nishati na ambayo ni endelevu?

Mbali ya nishati, kimazingira, Dodoma sasa hivi ingekuwa na mkakati wa kulinda mazingira kwa njia zote. Pasiwe na maji yanayozagaa tu bila ya mpangilio kila mara mvua zinaponyesha. Pangeweza kujengwa mabawa sehemu maalum ya kukusanya hayo maji na kuyatumia katika umwagiliaji na matumizi mengine.

Dodoma inahitaji upandaji wa miti kubadilisha kabisa muonekano wa mji. Hili lingeweza kutekelezeka kwa kuwahimiza tu wananchi kupanda miti katika makazi yao. Wangesaidiwa tu kupewa miche kazi hiyo ingefanyika bila ya kuwa na gharama kubwa.

Sijaiona "Master Plan" ya mji inayotekelezwa sasa, lakini matumaini yangu ni kwamba mambo ya usafiri/usafirishaji yamezingatiwa vizuri.

Dodoma linaweza kuwa jiji la kipekee sana miaka michache ijayo kama utekelezaji wa ujenzi wake utakuwa umepangiliwa vizuri.

Tayari nimekwishaona dosari ya zile nyumba za ofisi za serikali. Sitarajii kabisa kuona ofisi kama zile miaka ishirini ijayo ndio zikiwa ofisi za wizara na majengo mengine ya kiserikali.

Badala ya kujenga vijumba vile vingi kama walivyofanya, pesa ile wangeiweka pamoja na kujenga "Block" kubwa ambalo lingehudumia wizara mbalimbali kwa pamoja. Halafu baadae wakishatulia vizuri, kila wizara ingeanza kujenga ofisi zao zenye hadhi ya ofisi za serikali.
 
Dodoma yenu eeh?ulitoka nayo mbinguni sio?Kama Nyerere aliyejenga misingi ya Tanzania ya leo (unayotamba nayo humu) angekuwa na roho chafu kama zenu,leo msingeita huo mji "Dodoma yetu",halafu bado mnajinasibu kusimamia misingi ya Nyerere,poor you,stupid!
Afu majamaa yanayochagiza Dodoma ijengwe ili yahamie huko... yamejazana hapa mjini hayataki kuhama kabisa...

Hapana chezea raha ya upepo wa bahari
 
Waswahili wwanasema:-
  • Roma haikujengwa kwa siku moja.

  • Ivumayo haidumu
  • Mtaka yote kwa pupa hukosa yote

  • Mtaka nyingi nasaba hupata mingi misiba
  • Haraka haraka haina baraka
Kusikia Kwa Kenge Hadi Atoke Damu Puani Na Masikioni.
 
Back
Top Bottom