Kwa ugumu wa maisha nilionao, michango inayoendelea inanifikirisha sana

Nima Imma

JF-Expert Member
May 14, 2015
2,473
3,625
Hellow poleni na majukumu. Ni jioni tulivu namshukuru Mungu nina afya tele

Tumeona hukumu ya viongozi wa CHADEMA na faini za Mamilioni ya mapesa. Basi ile sijakaa sawa nikaona kwenye mitandao hamasa ya michango, namba zikatolewa za kutosha.

Basi giza tororo likazidi na joto likanizidia mana hata hela ya umeme sina nikapitiwa na usingizi nikalala. Asubuhi baada ya shughuli hapa na pale naona michango imetimizwa ya mamilioni ya mapesa. Kigogo kaposti na risiti tena ya kawaida si ile ya EFD tulohamasishwa tuzitumie.

Imenifikirisha mno juu ya hali ngumu niliyonayo ambayo nakosa hela kidogo ya mtaji ili niweze kujiingizia kipato. Maajabu ni kwamba kwa maelezo hela imechangishwa na wananchi

Wapendwa wanaJamii Forum wenzangu hebu naombeni tu mnipe kazi ya kufanya na mimi nipate kipato ama wa kunikopesha mtaji na mimi niweze kuanza biashara. Si mchango wa haya mamilioni hapana ni mtaji tu wa laki 5 kwani nina watu nyuma wananitegemea mnoo.

Natanguliza shukrani zangu za dhati, ila kiukweli bado nafikiria yale mamilioni yaliyochangishwa kwa haraka vile sijui wenzangu wanapataje hela na mimi nakwama wapi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wale ni viongozi na wawakilishi wetu ktk chombo nyeti kwenye mhimili wa nchi, hiki ni chombo kinachoamua mustakabali mpana wa maisha yetu ndio maana jambo hilo la michango limechukua sura ya kitaifa.

Kwa upande mwingine, wewe ni mtu binafsi tu, shida yako ni binafsi tu, kwa manufaa yako binafsi tu. Unachofanya ni sawa na omba omba mwenye afya njema kabisa, unaweza wa kufanya kazi ukakidhi mahitaji yako.

Nikushauri tu, badala ya kuweka kifurushi cha internet ili uwe omba omba wa kidijitali, tumia hela hiyo kama nauli ukatafute kazi.
 
Asante kwa ushauri
Wale ni viongozi na wawakilishi wetu ktk chombo nyeti kwenye mhimili wa nchi, hiki ni chombo kinachoamua mustakabali mpana wa maisha yetu ndio maana jambo hilo la michango limechukua sura ya kitaifa.

Kwa upande mwingine, wewe ni mtu binafsi tu, shida yako ni binafsi tu, kwa manufaa yako binafsi tu. Unachofanya ni sawa na omba omba mwenye afya njema kabisa, unaweza wa kufanya kazi ukakidhi mahitaji yako.

Nikushauri tu, badala ya kuweka kifurushi cha internet ili uwe omba omba wa kidijitali, tumia hela hiyo kama nauli ukatafute kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: fox
Tabia ya pesa inapenda uthamani(value) ndio maana watu smart wanakwambia jiengezee Value ndio pesa itakifata...ni rahisi kwa Maxence Mello kupata uCEO wa AirtelTZ kuliko wewe usie na value, Rahisi MilladAyo kupata mchango wamatibabu akiumwa kuliko wewe, Rahisi Diamond kupata Deals za MaBillion kuliko muuza nazi mtaani.

Value ya Mbowe huwezi ifananisha na yako na value hiyo Mbowe hakuitenheneza Overnight inaelekea kipindi ambacho ndio wazo la ku-engage kwenye politics watu walimuona hana kazi yakufanya ila leo anauwezo wakichangiwa mpaka 500M kwa value aliyoitengeneza.

So usipende Shortcut tafuta vibarua, kazi za Ali ya chini, jiajiri locally ukishapata pesa utaiyengeneza Value yako zaidi.

Portfolio | 2020
 
Ushauri mzuri sana.. Kikubwa aache tamaa!
Tabia ya pesa inapenda uthamani(value) ndio maana watu smart wanakwambia jiengezee Value ndio pesa itakifata...ni rahisi kwa Maxence Mello kupata uCEO wa AirtelTZ kuliko wewe usie na value, Rahisi MilladAyo kupata mchango wamatibabu akiumwa kuliko wewe, Rahisi Diamond kupata Deals za MaBillion kuliko muuza nazi mtaani.

Value ya Mbowe huwezi ifananisha na yako na value hiyo Mbowe hakuitenheneza Overnight inaelekea kipindi ambacho ndio wazo la ku-engage kwenye politics watu walimuona hana kazi yakufanya ila leo anauwezo wakichangiwa mpaka 500M kwa value aliyoitengeneza.

So usipende Shortcut tafuta vibarua, kazi za Ali ya chini, jiajiri locally ukishapata pesa utaiyengeneza Value yako zaidi.

Portfolio | 2020

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo linakuja mkuu kuna watu waliwahi kisaidiwa humu wakabadili ID , WAKAKATAA KABISA KULIPA DENI walilokopeshwa

Leo kuna uzi nimeupitia humu kuna mtu kama anaomba msaada fulani hivi wa kuendesha piki piki kwa mkataba na mm ninayo mpya kbs imetembea miez miwili nikaiweka ndani baada ya kupata ndinga kwa sponsor wangu kutoka ujerumani

Cha ajabu nimepitia uzi mwingine muda mchache nikakuta anainadi aina hiyo hiyo ya piki piki kaweka uzi anaulizia sifa ya hiyo piki piki ...spea zake inauzika kwa urahic

Nikaona kabisa hapa nataka kupigwa huku najiona hivi hivi ...!! Nikashituka mara anauliza plat number ni b au ni c utadhani piki piki imekuwa gari wakati piki piki zilosajiliwa upya huwezi kujua ipi imechoka kwa kuangalia plat number,

Tatizo wengi humu imani zimeshuka kabisa kuna wengine wanajimwambafay kupita maelezo halafu kumbe hawana nyuma wala mbele

Wana Id zaidi ya tatu ......kungekuwa na mfumo mzuri hata miguu ya kuku mpauko asingejinyonga

Wengi wametanguliza usera sana, badala ya utu wanasahau kbs kuna leo na kesho utamchenga leo mwenzako nakujiona umempiga ila kuna siku utahitaji msaada zaidi ya huo

Mkuuu jaribu sana kuomba msaada kwenye kanisa kama ni mkristo ,na kama mwisilamu jaribu kumshirikisha shehe wa msikiti unaabudia ...atakutafutia connection ila humu ....watu wameshakuwa na roho ngumu

sent from toyota Allex
 
UGUMU WA MAISHA + MICHANGO INAYOENDELEA + MATUKIO YANAYOTOKEA NCHINI = TUSIRUDIE MAKOSA YA 2015.
Lakini kumbuka tu, hakuna mwanasiasa nchi hii anaweza kubadilisha hali yako, pambana tu mkuu. Hizi za tusirudie makosa ni propaganda tu ili tubadilishe walaji wa mkate wetu wa taifa, kiuhalisia wewe na mimi ndio tupambane na hali zetu.
 
Lakini kumbuka tu, hakuna mwanasiasa nchi hii anaweza kubadilisha hali yako, pambana tu mkuu. Hizi za tusirudie makosa ni propaganda tu ili tubadilishe walaji wa mkate wetu wa taifa, kiuhalisia wewe na mimi ndio tupambane na hali zetu.
Huo ndio ukweli hakuna mwanasiasa anaweza kuboresha hali yako km usipoamua kupambana mwenyewe

sent from toyota Allex
 
Inamaana pik piki yako ndio aniandalia uzi kabisa?? Duh
Ama kwa kuwa ni ya mkataba ndio mana akataka kujua je? Itaweza kurejesha deni la mkataba na ikabaki na hali nzuri ya yeye kumuingizia kipato?
Tatizo linakuja mkuu kuna watu waliwahi kisaidiwa humu wakabadili ID , WAKAKATAA KABISA KULIPA DENI walilokopeshwa

Leo kuna uzi nimeupitia humu kuna mtu kama anaomba msaada fulani hivi wa kuendesha piki piki kwa mkataba na mm ninayo mpya kbs imetembea miez miwili nikaiweka ndani baada ya kupata ndinga kwa sponsor wangu kutoka ujerumani

Cha ajabu nimepitia uzi mwingine muda mchache nikakuta anainadi aina hiyo hiyo ya piki piki kaweka uzi anaulizia sifa ya hiyo piki piki ...spea zake inauzika kwa urahic

Nikaona kabisa hapa nataka kupigwa huku najiona hivi hivi ...!! Nikashituka mara anauliza plat number ni b au ni c utadhani piki piki imekuwa gari wakati piki piki zilosajiliwa upya huwezi kujua ipi imechoka kwa kuangalia plat number,

Tatizo wengi humu imani zimeshuka kabisa kuna wengine wanajimwambafay kupita maelezo halafu kumbe hawana nyuma wala mbele

Wana Id zaidi ya tatu ......kungekuwa na mfumo mzuri hata miguu ya kuku mpauko asingejinyonga

Wengi wametanguliza usera sana, badala ya utu wanasahau kbs kuna leo na kesho utamchenga leo mwenzako nakujiona umempiga ila kuna siku utahitaji msaada zaidi ya huo

Mkuuu jaribu sana kuomba msaada kwenye kanisa kama ni mkristo ,na kama mwisilamu jaribu kumshirikisha shehe wa msikiti unaabudia ...atakutafutia connection ila humu ....watu wameshakuwa na roho ngumu

sent from toyota Allex

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom