Nima Imma
JF-Expert Member
- May 14, 2015
- 2,473
- 3,625
Hellow poleni na majukumu. Ni jioni tulivu namshukuru Mungu nina afya tele
Tumeona hukumu ya viongozi wa CHADEMA na faini za Mamilioni ya mapesa. Basi ile sijakaa sawa nikaona kwenye mitandao hamasa ya michango, namba zikatolewa za kutosha.
Basi giza tororo likazidi na joto likanizidia mana hata hela ya umeme sina nikapitiwa na usingizi nikalala. Asubuhi baada ya shughuli hapa na pale naona michango imetimizwa ya mamilioni ya mapesa. Kigogo kaposti na risiti tena ya kawaida si ile ya EFD tulohamasishwa tuzitumie.
Imenifikirisha mno juu ya hali ngumu niliyonayo ambayo nakosa hela kidogo ya mtaji ili niweze kujiingizia kipato. Maajabu ni kwamba kwa maelezo hela imechangishwa na wananchi
Wapendwa wanaJamii Forum wenzangu hebu naombeni tu mnipe kazi ya kufanya na mimi nipate kipato ama wa kunikopesha mtaji na mimi niweze kuanza biashara. Si mchango wa haya mamilioni hapana ni mtaji tu wa laki 5 kwani nina watu nyuma wananitegemea mnoo.
Natanguliza shukrani zangu za dhati, ila kiukweli bado nafikiria yale mamilioni yaliyochangishwa kwa haraka vile sijui wenzangu wanapataje hela na mimi nakwama wapi!
Sent using Jamii Forums mobile app
Tumeona hukumu ya viongozi wa CHADEMA na faini za Mamilioni ya mapesa. Basi ile sijakaa sawa nikaona kwenye mitandao hamasa ya michango, namba zikatolewa za kutosha.
Basi giza tororo likazidi na joto likanizidia mana hata hela ya umeme sina nikapitiwa na usingizi nikalala. Asubuhi baada ya shughuli hapa na pale naona michango imetimizwa ya mamilioni ya mapesa. Kigogo kaposti na risiti tena ya kawaida si ile ya EFD tulohamasishwa tuzitumie.
Imenifikirisha mno juu ya hali ngumu niliyonayo ambayo nakosa hela kidogo ya mtaji ili niweze kujiingizia kipato. Maajabu ni kwamba kwa maelezo hela imechangishwa na wananchi
Wapendwa wanaJamii Forum wenzangu hebu naombeni tu mnipe kazi ya kufanya na mimi nipate kipato ama wa kunikopesha mtaji na mimi niweze kuanza biashara. Si mchango wa haya mamilioni hapana ni mtaji tu wa laki 5 kwani nina watu nyuma wananitegemea mnoo.
Natanguliza shukrani zangu za dhati, ila kiukweli bado nafikiria yale mamilioni yaliyochangishwa kwa haraka vile sijui wenzangu wanapataje hela na mimi nakwama wapi!
Sent using Jamii Forums mobile app