Kwa TANESCO sawa, kwanini sio kwa BASATA na TCRA?

Standards Person

JF-Expert Member
Apr 22, 2021
673
859
Hongera Mh. Kalemani kwa kuwawajibisha watumishi ambao aidha wamehisika kusababisha usumbufu au vyovyote vile.

Pia Mh. Kalemani amekua muungwana kwa kuwaomba radhi Watanzania kwa usumbufu uliojitokeza.

Wakati huohuo waziri mkuu ameenda mbali zaidi kwa kutoa maagizo kwamba wakae pembeni wapishe uchunguzi.

Hoja yangu inakuja kuwa nikwanini BASATA, TFF na TCRA hakuna hata mmoja aliyewajibishwa?

TFF na BASATA walisababisha usumbufu mkubwa na hasara kwa mashabiki na wapenzi wa mpira kwa kuahirisha mechi saa chache kabla ya mpira kuanza. Watu waliondokauwanjani bila kushuhudia mtanange na ukizingatia mtu ametembea kuanzia Kigoma hadi Dar es salaam.

Waziri Mkuu vipi mbona wahusika hakuna aliyewajibika?

Jipu lingine ni TCRA. Bado mambo hayajatulia. Vifurushi vinaisha haraka, bei walijipangia na mtandao unasumbua bado. Kwanini Ndugulile hakuwajibika au kuwajibisha mtu? Huu ni udhaifu mkubwa.

Ushauri wangu nikwamba kusiwe na watu na viatu. Ukiachilia mambo yote hayo bado TCRA wanahitajika wafanye maboresho kwani mtandao unasinzia tofauti na kipindi cha kabla ya uchaguzi.
 
Back
Top Bottom