Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,913
Njia mashuhuri ya meli za kibiashara ya Suez Canal kutokea red sea ni kama kwamba imefungwa kutokana na mashambulio ya Houth.
Meli peke zinazopita bila wasi wasi ni zile zinazotoka ama kuelekea Iran.Nyengine ni zile zinazotoka ama kwenda bahari nyeusi ambako ndiko ziliko bandari kubwa za kusafirisha nafaka za Urusi.
Msafirishaji mmoja wa nafaka ameweka wazi kuwa mmiliki yeyote anayependa kupitisha meli zako hapo hajakatazwa na akipenda anapangiwa njia hiyo.Hata hivyo akasema wengi wao wameamua kupita njia ya mbali na ya gharama kuizunguka Afrika.
Msafirishaji huyo akaongeza kwa kusema mashambulizi ya nchi washirika hayajaweza kuwazuia wanamgambo wa Houth kuzifurusha meli na vile vile hakuna ulinzi wa kuaminika unaowapa matumanini wenye meli kupita eneo hilo.
Meli peke zinazopita bila wasi wasi ni zile zinazotoka ama kuelekea Iran.Nyengine ni zile zinazotoka ama kwenda bahari nyeusi ambako ndiko ziliko bandari kubwa za kusafirisha nafaka za Urusi.
Msafirishaji mmoja wa nafaka ameweka wazi kuwa mmiliki yeyote anayependa kupitisha meli zako hapo hajakatazwa na akipenda anapangiwa njia hiyo.Hata hivyo akasema wengi wao wameamua kupita njia ya mbali na ya gharama kuizunguka Afrika.
Msafirishaji huyo akaongeza kwa kusema mashambulizi ya nchi washirika hayajaweza kuwazuia wanamgambo wa Houth kuzifurusha meli na vile vile hakuna ulinzi wa kuaminika unaowapa matumanini wenye meli kupita eneo hilo.