Kwa Ramani ya Gambia ilivyo ECOWAS wataipiga ndani ya one week!!

Nakuelewa mkuu,
Lakini ukweli ni kwamba hata kama wameombwa na wapiga kura wa Gambia,
Uvamizi wa kijeshi siyo njia sahihi kwa sasa, wangemuwekea vikwazo vya kiuchumi tu.
Lazima atasalimu amri.

Tukiangalia hili jambo kwenye taswira kubwa,
Afrika yetu haitakiwi iige kila kitu kutoka Ulaya na Marekani,
Kama tukianza kuvamiana kijeshi leo, nakuhakikishia haitaishia hapo tu.
Litakuwa ni Zimwi Jipya kuingia barani Afrika mbali na Umasikini, Maradhi na Ujinga.

Utasikia uchaguzi wa Zimbabwe haukuwa huru na haki,
SADC itume kikosi kazi kwenda kumtoa Robert Mugabe.
Utasikia tena Uchaguzi wa Burundi siyo wa huru na haki,
Rwanda na Uganda wanapendekeza EAC itume kikosi kazi kumtoa Nkhurunzinza.

Mwishowe tutakuja kufika sehemu,
Nchi kubwa zenye nguvu zitatumia huo mwamvuli kuvamia nchi nyingine.
Mwaka 1938 Adolf Hitler alivamia Czechoslovakia akisingizia kwamba anaenda kulinda haki za raia wa Czech na Slovakia.
Lakini ukweli ni kwamba alichokifanya Hitler ulikuwa ni Uhalifu wa kivita.

ECOWAS watakuwa ni watu wa hovyo sana kama wakikubali kufanya huu uamuzi,
Hovyo! Hovyooo kabisaaaaa!!!!

Chaguzi za nyuma akiwa rais ni tume za uchaguzi zilizomtangaza kushinda na hapakuwa na shida.

Mwaka jana mwenyekiti wa tume katangaza Jammey kashindwa, Jammey kakubali, baada ya muda Jammey kageuka. Jiulize, huyo mtu kuna uchaguzi wowote wa baadae atakaopokea matokeo ya kushindwa?

Kwa matukio hayo na sababu ulizotoa, tunatengeneza mazoea mabaya pia, yaani rais ashimeshindwa kwa mujibu wa tume, amekubali baada ya muda anakataa, anatangaza hali ya hatari na hivyo kuzuia kuapishwa kwa aliyetangazwa na tume!

Huo ni mwanya kwa wengine katika nchi hiyo na labda Afrika kufanya hivyo au hali inayofanana na hiyo siku za baadaye.
Umetumia neno kuvamia, lakini tambua pia huyo anayeng'ng'ania pia ni mvamizi wa kutumia majeshi.

Vinginevyo turudi tu kwenye mifumo yetu ya enzi ya uchifu na ufalme tujue moja kinyume cha hapo wakorofi washughulikiwe na washughulikiwe kikwelikweli.
 
Sidhani kama unajua jeshi vizuri!kuzungukwa pande zote sio hoja ya ushindi kwenye medani za kijeshi!bali mbinu na uimara wa jeshi husika..mfano mzuri ni rwanda!imezungukwa kila kona na ni ka nchi kadogo lakini kana jeuri kupita maelezo..Hebu tafakari tena!
Compared to which jeshi?
 
Majeshi unifomu tu yale, idadi batalioni 2, hawana navy wala airforce, manowari ya Nigeria iko pale nje ya Banjul, mji mkuu wa Gambia tangu jumamosi, hawajui wafanye nini! Kanchi kenyewe upana km 55 urefu km 300; hata FFU yetu au GSU ya Kenya wanakatiza pale kwa masaa machache sana!
Aha ha ha ha ha!
 
Sidhani kama unajua jeshi vizuri!kuzungukwa pande zote sio hoja ya ushindi kwenye medani za kijeshi!bali mbinu na uimara wa jeshi husika..mfano mzuri ni rwanda!imezungukwa kila kona na ni ka nchi kadogo lakini kana jeuri kupita maelezo..Hebu tafakari tena!
wanajeshi wote wapo 2500,
 
Hivi hakuna njia nyingine yoyote ya kumfanya Jammeh aachie madaraka zaidi ya kumvamia kijeshi?
Gambia ni nchi ndogo sana na uchumi wake ni wa biskuti, mkiwawekea vikwazo miezi mitatu tu ni lazima uvunjike.
Kimkakati uvamizi wa kijeshi ni njia ya mwisho endapo njia nyingine zimeshindwa.
Wanaweza kuvamia The Gambia na kusababisha majanga makubwa zaidi hata ya Jammeh.
Fuatilia vizuri members wa serikali aliyoipindua pamoja na waliopo sasa ndipo utaundua hawa watu wamevumilia upuuzi kwa muda wa miaka 24 na sasa wanasema basi. Waliomo ndani ya Gambia ni waoga sana maana hata wanajeshi walioonyesha kukubaliana na matwakwa ya wananchi katika uchaguzi wa juzi wote wamekamatwa. Wanaoguswa na hali hii ndio wameamua kwamba liwalo na liwe na hawaoni busara ya kuacha jirani zao wakiteswa na kakikundi kadogo ka wahuni na wajinga kwa kisingizio cha nchi huru.
Hebu fikiria rais mteule kafiwa na mwanae juzi lakini mazishi yamefanyika bila uwepo wake!
 
Sidhani kama unajua jeshi vizuri!kuzungukwa pande zote sio hoja ya ushindi kwenye medani za kijeshi!bali mbinu na uimara wa jeshi husika..mfano mzuri ni rwanda!imezungukwa kila kona na ni ka nchi kadogo lakini kana jeuri kupita maelezo..Hebu tafakari tena!
Sifa zingine buana
 
Miaka ishirini inatosha kwa mtu mmoja. Akiondoka sasa hivi atasaidia sana nchi yate and watu wengi wasikufe. Kama ukuweza kuendeleza nchi kwa miaka ishirini hawezi kuisaida hata kama wakimpa miaka arubaini hata fanya chochote.

Wagambia kila siku wanakufa wakitaka kwenda ulaya, engi wanaishi senegal, maisha magumu sana. Kwanini hataki kumpa mtu mwingine nafasi? Watu wangapi wataendelea kufa kwa sababu ya umaskini mkubwa akiendelea kuwa rais. Inabidi wamtoe yeye mwenyewe bila kuwaumiza wananchi wagambia.
wewe ungeweza kumpa mtu aliyehaidi kukushughulikia?
 
Back
Top Bottom